-
“Nilitaka Tu Kuchukua Barua Zangu”Amkeni!—2011 | Juni
-
-
Fikiria kisa cha Hafeni.
Hafeni alizaliwa nchini Zambia na kulelewa katika kambi za wakimbizi katika nchi jirani. “Nilikuwa na hasira,” akasema, “kwa sababu ya ukatili na ukosefu wa haki ambao familia yetu na nyingine zilikuwa zimetendewa.” Kwa hiyo, akajiunga na kikundi cha wanamgambo ambacho wazazi wake walishirikiana nacho.
Akifikiria kuhusu nyakati hizo, Hafeni anaendelea kusema: “Jambo lenye kusikitisha zaidi ni madhara ya kihisia unayopata kwa kuishi kama mkimbizi. Watoto walitenganishwa na mama, baba, na ndugu na dada zao. Wale wenye umri mkubwa walienda kupigana. Wengi wao hawakurudi. Sikuwahi kumwona baba yangu, hata katika picha. Ninachojua tu ni kwamba alikufa vitani. Bado ninakumbwa na maumivu makali ya kihisia hadi leo.”
-
-
Kwa Nini Watu Fulani Hutenda kwa Jeuri?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
JOSEBA, anayeishi nchini Hispania, aliulizwa kwa nini alijiunga na kikundi cha wanamgambo. “Ukandamizaji na ukosefu wa haki tuliopatwa nao ulikuwa mwingi,” akasema. “Katika jiji kubwa la Bilbao, ambako nilikuwa nikiishi, polisi walikuwa wakija, wanawapiga watu, na kuwakamata.”
Joseba anaendelea kusema: “Asubuhi moja nilikamatwa kwa kueleza waziwazi hisia zangu kuhusu mbinu hizo za polisi. Nilikasirika sana hivi kwamba nilitaka kufanya jambo fulani—ujeuri wa aina fulani—ili kutuliza hali hiyo.”
-
-
Kwa Nini Watu Fulani Hutenda kwa Jeuri?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
Kwa mfano, Hafeni, aliyetajwa katika habari inayotangulia alisema hivi: “Tulinyang’anywa ardhi yetu isivyo haki. Wanyama hupigana ili kutetea maeneo yao, kwa hiyo lilionekana kuwa jambo linalopatana na akili kupigania ardhi na haki zetu.”
-
-
Kwa Nini Watu Fulani Hutenda kwa Jeuri?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
Hisia za Jeuri Zimekolea Mioyoni Mwao
Joseba aliyetajwa mapema, alitendewa vibaya sana alipokamatwa. Anasema: “Ukatili huo ulinihakikishia kwamba nilikuwa na haki ya kutenda kwa chuki. Iwapo ningekufa ili kuleta mabadiliko, ingekuwa sawa.”
-
-
Kwa Nini Watu Fulani Hutenda kwa Jeuri?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
“Tulipokuwa kwenye kambi za wakimbizi,” Hafeni anasema, “kulikuwa na mikutano ya wanamgambo iliyotufundisha kwamba kila wakati wazungu walikuwa wakitafuta njia za kuwakandamiza watu weusi.” Kulikuwa na matokeo gani?
Aliendelea kusema hivi: “Chuki yangu kuelekea wazungu iliongezeka. Sikumwamini yeyote kati yao. Mwishowe, singeweza kuvumilia zaidi na nikajiambia kwamba lazima kizazi chetu kichukue hatua.”
-
-
Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Usio na Ugaidi?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
Kitabu Kinachoweza Kubadili Moyo
Katika miaka ya 1990, Hafeni, alianza kuchunguza mafundisho yake ya kidini na akaamua kutafuta Biblia. Anasema hivi: “Nilianza kwa kuchunguza Injili [vitabu vya Biblia vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana], ambavyo vilikuwa na masimulizi ya maisha ya Yesu. Nilipokuwa nikisoma, nilipendezwa upesi na utu wa Yesu na njia yake ya kushughulika na watu kwa fadhili na bila ubaguzi. Hilo liligusa sana moyo wangu.”
Hafeni anasema kwamba alipoendelea kusoma, “andiko moja la Biblia lilinisaidia kabisa kuelewa jinsi Mungu anavyohisi—Matendo 10:34 na 35.” Linasema hivi: “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”
Hafeni anasema hivi: “Nilifikia mkataa kwamba wanadamu ndio wanaosababisha ubaguzi wa kikabila, kitaifa, na kijamii. Nilikuja kutambua kwamba ujumbe wa Biblia unaweza kubadili jinsi watu wanavyofikiri na kwamba jambo muhimu zaidi maishani ni kuwa na msimamo mzuri mbele za Mungu. Hilo ni muhimu zaidi kuliko kupigana kwa niaba ya watu wa kabila, jamii, au rangi fulani.”
Joseba, aliyenukuliwa katika habari iliyotangulia, alikuwa anasimamia kikundi kidogo cha kikosi maalumu kilichopanga kulipua kituo kimoja cha polisi. “Lakini kabla ya kutekeleza shambulizi hilo,” anaeleza Joseba, “nilikamatwa na nikafungwa gerezani kwa miaka miwili.” Baadaye, mke wake, Luci, akaanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Mwishowe, Joseba alianza kushiriki katika mazungumzo hayo.
Joseba anasema hivi: “Kadiri nilivyojifunza mengi zaidi kumhusu Yesu, ndivyo alivyokuja kuwa kielelezo changu. Nilipendezwa hasa na maneno haya yake: ‘Wale wote wanaouchukua upanga wataangamia kwa upanga.’ Nilijua kwamba maneno hayo yalikuwa ya kweli.” (Mathayo 26:52) Joseba alisema hivi: “Kumwua mtu kunawachochea watu wa familia yake wawe na chuki na tamaa ya kulipiza kisasi. Jeuri inasababisha maumivu tu, haitokezi ulimwengu bora.” Joseba alianza kufanya mabadiliko katika kufikiri kwake.
Hafeni na Joseba walijionea kwamba mafundisho ya Biblia yanaweza kubadili maisha ya mtu.
-
-
Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Usio na Ugaidi?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
Undugu Unaochochewa na Upendo
Hafeni alipoanza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova, alichochewa sana kuona jinsi watu wa jamii tofauti-tofauti walivyoshirikiana kwa upatano. “Ilisisimua sana kuketi kando ya wazungu,” anasema. “Sikuwahi kufikiri kwamba katika maisha yangu ningewahi kumwita mzungu ndugu yangu. Hilo lilinisadikisha kabisa kwamba lazima Mashahidi wawe ndio wenye dini ya kweli, kwa kuwa walikuwa na umoja kati yao ambao nilitamani na walikuwa na upendo kati yao licha ya tofauti za kijamii.”
-
-
Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Usio na Ugaidi?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
Kama ilivyotajwa katika habari ya kwanza, karibu Andre afe katika bomu lililowaua baadhi ya rafiki zake. Lilikuwa limetegwa hapo na kikundi fulani cha wanamgambo. Baada ya hapo alijifunza na kufuata mashauri ya Biblia kwamba mtu anapaswa ‘kusamehe kwa hiari.’ (Wakolosai 3:13) Baadaye, Hafeni, ambaye baada ya miaka mingi alikuja kuwa mshiriki wa kikundi hichohicho, alijifunza kufuata kanuni za Biblia na akaacha matendo ya jeuri. (Zaburi 11:5) Sasa, wote wawili ni Mashahidi wa Yehova na wanafanya kazi pamoja katika ofisi ya tafsiri ya Mashahidi katika nchi moja ya Afrika.
-
-
Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Usio na Ugaidi?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
[Blabu katika ukurasa wa 7]
Hafeni na Joseba walijionea kwamba mafundisho ya Biblia yanaweza kubadili maisha ya mtu
-
-
Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Usio na Ugaidi?Amkeni!—2011 | Juni
-
-
[Picha katika ukurasa wa 8]
Kufuata kanuni za Biblia kuliwasaidia Hafeni na Andre kupendana kikweli
-