Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na wafu walihukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao.

  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Ufunuo 20:12b,

  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Hati-Kunjo ya Uhai

      11. (a) “Hati-kunjo ya uhai” ni nini, na ni majina ya nani yaliyorekodiwa katika hati-kunjo hii? (b) Ni kwa nini hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu?

      11 Yohana husema juu ya “hati-kunjo ya uhai.” Hayo ni maandishi ya wale walio katika mstari wa kupokea uhai wa milele kutoka kwa Yehova. Majina ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu, ya umati mkubwa, na ya watu waaminifu wa kale, kama vile Musa, yameandikwa katika hati-kunjo hii. (Kutoka 32:32, 33; Danieli 12:1; Ufunuo 3:5, NW) Bado kufikia hapa, hakuna hata mmoja wa wale “wasio waadilifu” waliofufuliwa aliye na jina lake limeandikwa katika hati-kunjo ya uhai. Kwa hiyo hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu kuruhusu kuandikwa kwa majina ya wengine ambao wanakuja kustahili. Wale ambao majina yao hayapati kuandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai ‘wanavurumishwa ndani ya ziwa la moto.’—Ufunuo 20:15, NW; linga Waebrania 3:19.

      12. Ni nini kitakachoamua kama mtu ataandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa, na Hakimu mwekwa wa Yehova aliwekaje kielelezo?

      12 Basi, ni nini kitakachoamua kama mtu anapata kuandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa wakati huo? Sababisho kuu litakuwa lile lile kama lilivyokuwa katika siku ya Adamu na Hawa: utii kwa Yehova. Kama vile mtume Yohana alivyoandikia Wakristo wenzake wapendwa: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.” (1 Yohana 2:4-7, 17, NW) Kwa habari ya utii, Hakimu mwekwa wa Yehova aliweka kielelezo: “Ingawa [Yesu] alikuwa Mwana, yeye alijifunza kutii kutokana na vitu ambavyo yeye aliteseka; na baada ya yeye kuwa amefanywa mkamilifu, yeye alipata kuwa mwenye daraka la wokovu wa milele kwa wale wote wanaotii yeye.”—Waebrania 5:8, 9, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki