-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 40
Kuponda Kichwa cha Nyoka
Njozi ya 14—Ufunuo 20:1-10
Habari: Kutiwa kwa Shetani ndani ya abiso, Utawala wa Mileani, mtihani wa mwisho kabisa wa wanadamu, na kuharibiwa kwa Shetani
Wakati wa utimizo: Kutoka mwisho wa dhiki kubwa hadi kuharibiwa kwa Shetani
1. Utimizo wa unabii wa kwanza wa Biblia umeendeleaje?
JE! WEWE wakumbuka unabii wa kwanza wa Biblia? Ulitamkwa na Yehova Mungu aliposema kwa Nyoka: “Mimi nitaweka uadui kati ya wewe na mwanamke na kati ya mbegu yako na mbegu yake. Yeye atachubua wewe katika kichwa na wewe utachubua yeye katika kisigino.” (Mwanzo 3:15, NW) Sasa utimizo wa unabii huo waja kwenye upeo wao! Sisi tumefuatilia historia ya vita ya Shetani dhidi ya tengenezo la Yehova la kimbingu lililo kama mwanamke. (Ufunuo 12:1, 9) Mbegu ya kidunia ya Nyoka, pamoja na dini, siasa, na biashara kubwa-kubwa yayo, imerundika mnyanyaso wenye ukatili juu ya mbegu ya mwanamke, Yesu Kristo na wafuasi wake wapakwa-mafuta 144,000, hapa duniani. (Yohana 8:37, 44; Wagalatia 3:16, 29) Shetani alimpiga Yesu kwa kifo chenye maumivu makali. Lakini hiki kilithibitika kuwa kama kidonda cha kisigino, kwa maana Mungu alimfufua Mwana wake mwaminifu siku ya tatu.—Matendo 10:38-40.
2. Shetani huchubuliwaje, na ni jambo gani linaloipata mbegu ya Shetani ya kidunia?
2 Vipi Nyoka na mbegu yake? Wapata 56 W.K. mtume Paulo aliandika barua ndefu kwa Wakristo katika Roma. Katika kuimalizia, yeye aliwatia moyo kwa kusema: “Kwa upande wake, Mungu ambaye hutoa amani ataponda Shetani chini ya nyayo zenu karibuni.” (Warumi 16:20, NW) Hii ni zaidi ya kuchubua juujuu tu. Shetani atapondwapondwa! Hapa Paulo alitumia neno la Kigiriki, syn·triʹbo, hilo linamaanisha kuchubua katika hali kama ya ute, kukanyagakanyaga chini ya nyayo, kuharibu kabisa kwa kupondaponda. Kwa habari ya sehemu ya kibinadamu ya mbegu ya Nyoka, hii inatazamiwa ipatwe na tauni halisi katika siku ya Bwana, ikifikia upeo kwenye dhiki kubwa katika kupondwapondwa kabisa kwa Babuloni Mkubwa na ile mifumo ya kisiasa ya ulimwengu, pamoja na wategemezaji wayo wa kifedha na kivita. (Ufunuo, sura za 18 na 19) Hivyo Yehova analeta kwenye upeo uadui kati ya mbegu mbili. Mbegu ya mwanamke husherehekea ushindi juu ya mbegu ya kidunia ya Nyoka, na mbegu hiyo inakuwa haipo tena!
Shetani Atiwa Ndani ya Abiso
3. Yohana anatuambia ni nini kitakachompata Shetani?
3 Basi, ni nini kilicho akibani kwa ajili ya Shetani mwenyewe na roho waovu wake? Yohana hutuambia: “Na mimi nikaona malaika mmoja akija chini kutoka katika mbingu mwenye ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa katika mkono wake. Na yeye akakamata drakoni, nyoka wa awali kabisa, ambaye ndiye Ibilisi na Shetani, na akamboba yeye kwa miaka elfu moja. Na yeye alimvurumisha ndani ya abiso na akaifunga na akatia kalafati juu yake, ili asipate kuongoza vibaya mataifa tena mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha. Baada ya vitu hivi ni lazima yeye aachwe legelege kwa kitambo kidogo.”—Ufunuo 20:1-3, NW.
4. Ni nani aliye malaika mwenye ufunguo wa abiso, na sisi twajuaje?
4 Malaika huyu ni nani? Ni lazima yeye awe na nguvu nyingi mno kuweza kumwondolea mbali adui mkuu wa Yehova. Yeye ana “ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa.” Je! hiyo haitukumbushi njozi ya mapema zaidi? Ee, ndiyo, yule mfalme juu ya nzige anaitwa “malaika wa abiso”! (Ufunuo 9:11, NW) Kwa hiyo hapa sisi tunaona Mteteaji Mkuu wa Yehova, Yesu Kristo aliyetukuzwa, akitenda. Huyu malaika mkuu ambaye alitupa Shetani kutoka katika mbingu, ambaye alihukumu Babuloni Mkubwa, na ambaye aliondolea mbali “wafalme wa dunia na majeshi yao” kwenye Har–Magedoni hakika hangekaa kando aruhusu malaika mwingine mdogo zaidi apige dharuba kuu hii ya kutia Shetani katika abiso!—Ufunuo 12:7-9; 18:1, 2; 19:11-21, NW.
5. Malaika wa abiso hushughulikaje na Shetani Ibilisi, na kwa nini?
5 Drakoni mkubwa mwenye rangi-moto alipovurumishwa chini kutoka katika mbingu, alisemwa kuwa ndiye “nyoka wa awali kabisa, mmoja ambaye huitwa Ibilisi na Shetani, ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa.” (Ufunuo 12:3, 9, NW) Sasa, wakati wa kukamatwa kwake na kutiwa ndani ya abiso, yeye ameelezwa tena kwa ukamili kuwa ndiye “drakoni, nyoka wa awali kabisa, ambaye ndiye Ibilisi na Shetani.” Huyu ambaye ni mmezaji, mdanganyaji, mchongezi, na mpinzani mwenye sifa mbaya sana anafungwa mnyororo na kuvurumishwa “ndani ya abiso,” ambayo inashindikwa ndi ndi ndi na kutiwa kalafati kikiki, “ili asipate kuongoza vibaya mataifa tena.” Huku kutiwa kwa Shetani ndani ya abiso ni kwa muda wa miaka elfu moja, wakati huo uvutano wake juu ya aina ya binadamu utakuwa haupo tena kama wa mfungwa aliye ndani ya gereza la shimo lenye kina kirefu. Malaika wa abiso anamwondolea mbali kabisa Shetani asiwe na mgusano wowote na Ufalme wa uadilifu. Lo! ni kitulizo kama nini kwa aina ya binadamu!
6. (a) Kuna ithibati gani kwamba roho waovu pia huenda ndani ya abiso? (b) Sasa ni nini kinachoweza kuanza, na kwa nini?
6 Inakuwaje kwa roho waovu? Wao vilevile “wamewekwa kwa ajili ya hukumu.” (2 Petro 2:4, NW) Shetani huitwa “Beelzebubu mtawala wa roho waovu.” (Luka 11:15, 18; Mathayo 10:25, NW) Kwa sababu ya kumwunga mkono Shetani kwa muda mrefu, je! wao wasipasishwe hukumu iyo hiyo? Kwa muda mrefu abiso imekuwa kitu cha kuogopwa na roho waovu hao; pindi moja Yesu alipokabiliana nao, wao “walifuliza kusihi yeye asiagize wao waende ndani ya abiso.” (Luka 8:31, NW) Lakini Shetani anapotiwa ndani ya abiso, kwa hakika malaika zake watavurumishwa ndani ya abiso pamoja naye. (Linga Isaya 24:21, 22.) Baada ya Shetani na roho waovu kutiwa ndani ya abiso, Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo unaweza kuanza.
7. (a) Ni katika hali gani Shetani na roho waovu wake watakuwa wakiwa ndani ya abiso, na sisi twajuaje? (b) Je! Hadesi na abiso ni kitu kile kile? (Ona kielezi cha chini.)
7 Je! Shetani na roho waovu wake watakuwa wakitenda wakiwamo ndani ya abiso? Basi, kumbuka hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, mwenye vichwa saba ambaye “alikuwako, lakini hayuko, na bado yu karibu kupanda nje ya abiso.” (Ufunuo 17:8, NW) Alipokuwa katika abiso, ‘alikuwa hayuko.’ Alikuwa hatendi, hajongei, kwa madhumuni na makusudi yote alikuwa amekufa. Hali kadhalika, mtume Paulo akinena juu ya Yesu, alisema: “‘Ni nani atakayeshuka kuingia ndani ya abiso?’ yaani, kumleta juu Kristo kutoka kwa wafu.” (Warumi 10:7, NW) Akiwa katika abiso hiyo, Yesu alikuwa amekufa.a Basi, inapatana na akili kukata shauri kwamba Shetani na roho waovu wake watakuwa katika hali ya kutotenda kama ya kifo kwa muda wa miaka elfu ya kutiwa kwao ndani ya abiso. Hizo ni taarifa njema kama nini kwa wapenda uadilifu!
Mahakimu kwa Miaka Elfu Moja
8, 9. Sasa Yohana hutuambia nini juu ya wale wanaoketi juu ya viti vya ufalme, nao ni akina nani?
8 Baada ya miaka elfu, Shetani anaachiliwa kutoka katika abiso kwa kitambo kifupi. Kwa nini? Kabla ya kutoa jibu, Yohana anarudisha uangalifu wetu kwenye mwanzo wa kipindi hicho cha wakati. Tunasoma: “Na mimi niliona viti vya ufalme, na kulikuwako wale walioketi juu yavyo, na nguvu za kuhukumu zilipewa kwao.” (Ufunuo 20:4a, NW) Ni nani hawa wanaoketi juu ya viti vya ufalme na kutawala katika mbingu pamoja na Yesu aliyetukuzwa?
9 Wao ni “watakatifu” ambao Danieli alieleza habari yao kuwa wakitawala katika Ufalme pamoja na Mmoja aliye “kama mwana wa binadamu.” (Danieli 7:13, 14, 18, NW) Wao ndio wale wale wazee 24 wanaoketi juu ya viti vya ufalme vya kimbingu katika kuwapo hasa kwa Yehova. (Ufunuo 4:4) Wao ni kutia ndani mitume 12, ambao Yesu aliwapa ahadi hii: “Katika uumbaji-upya wakati Mwana wa binadamu anaketi chini juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu, nyinyi ambao mmefuata mimi mtaketi nyinyi wenyewe pia juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.” (Mathayo 19:28, NW) Wangetia ndani Paulo pia, pamoja na Wakristo Wakorintho ambao walibaki wakiwa waaminifu. (1 Wakorintho 4:8; 6:2, 3) Wao ni kutia ndani, vilevile, washiriki wa kundi la Laodikia ambao walishinda.—Ufunuo 3:21.
10. (a) Sasa Yohana huelezaje habari ya wafalme 144,000? (b) Kutokana na aliyotuambia Yohana mapema zaidi, wafalme 144,000 hutia ndani nani?
10 Viti vya ufalme—144,000 vyote pamoja—vimetayarishwa kwa ajili ya hawa washindi wapakwa-mafuta ambao ‘wamenunuliwa kutoka miongoni mwa aina ya binadamu wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.’ (Ufunuo 14:1, 4, NW) “Ndiyo,” aendelea Yohana, “mimi niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kwa Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakuwa wameabudu wala hayawani-mwitu wala mfano wake na ambao hawakuwa wamepokea alama juu ya kipaji cha uso wao na juu ya mkono wao.” (Ufunuo 20:4b, NW) Miongoni mwa wafalme hao, basi, wamo wale Wakristo wafia-imani ambao mapema zaidi, wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha kwanza, walimwuliza Yehova angengoja muda gani zaidi ili alipize kisasi cha damu yao. Wakati huo, walipewa joho jeupe na kuambiwa wangojee kitambo kidogo. Lakini sasa kisasi cha damu yao kimekwisha lipizwa kupitia kuteketezwa kwa Babuloni Mkubwa, na mataifa kuharibiwa na Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, na Shetani kutiwa ndani ya abiso.—Ufunuo 6:9-11; 17:16; 19:15, 16, NW.
11. (a) Sisi tuueleweje usemi “waliouawa kwa shoka”? (b) Ni kwa nini inaweza kusemwa kwamba wote 144,000 walikufa kifo cha dhabihu?
11 Je! mahakimu wa kifalme hawa wote 144,000 ‘waliuawa kwa shoka’ kimwili? Yaelekea, ni wachache wao kwa kulinganisha waliouawa hivyo kwa maana halisi. Ingawa hivyo, usemi huu bila shaka unakusudiwa kutia ndani Wakristo wapakwa-mafuta wote waliovumilia ufia-imani kwa njia moja au nyingine.b (Mathayo 10:22, 28) Kwa hakika, Shetani angependa wote wauawe kwa shoka, lakini, kwa kweli, si ndugu wote wapakwa-mafuta wa Yesu wanaokufa wakiwa wafia-imani. Wengi wao huuawa na ugonjwa au uzee. Hata hivyo, hao pia ni wa kile kikundi ambacho Yohana anaona sasa. Kifo cha wao wote, kwa maana fulani, ni cha dhabihu. (Warumi 6:3-5) Kwa kuongezea, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa sehemu ya ulimwengu. Kwa sababu hiyo, wao wote wamechukiwa na ulimwengu, maana yake, wakawa wafu katika macho yao. (Yohana 15:19; 1 Wakorintho 4:13) Hakuna hata mmoja wao aliyeabudu hayawani-mwitu au mfano wake, na walipokufa, hakuna hata mmoja wao aliyechukua alama ya hayawani. Wao wote walikufa wakiwa washindi.—1 Yohana 5:4; Ufunuo 2:7; 3:12; 12:11.
12. Yohana anaripoti nini juu ya wafalme 144,000, na kuja kwao kwenye uhai kunatukia lini?
12 Sasa washindi hawa waishi tena! Yohana aripoti: “Na wao wakaja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu moja.” (Ufunuo 20:4c, NW) Je! hii inamaanisha kwamba mahakimu hawa hawafufuliwi mpaka baada ya uharibifu wa mataifa na Shetani na roho waovu wake kutiwa ndani ya abiso? Hapana. Walio wengi wao tayari wako hai sana, kwa kuwa walipanda farasi pamoja na Yesu dhidi ya mataifa kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 2:26, 27; 19:14) Kweli kweli, Paulo alionyesha kwamba ufufuo wao unaanza upesi baada ya kuwapo kwa Yesu kuanza katika 1914 na kwamba baadhi yao hufufuliwa mbele ya wengine. (1 Wakorintho 15:51-54; 1 Wathesalonike 4:15-17) Kwa hiyo, kuja kwao kwenye uhai kunatukia kwa kipindi fulani cha wakati wanapopokea mmoja mmoja zawadi ya uhai usioweza kufa katika mbingu.—2 Wathesalonike 1:7; 2 Petro 3:11-14.
13. (a) Inatupasa tuoneje miaka elfu ambayo katika hiyo 144,000 hutawala, na kwa nini? (b) Papiasi wa Hierapolisi aliionaje miaka elfu? (Ona kielezi cha chini.)
13 Kutawala na kuhukumu kwao kutakuwa kwa miaka elfu moja. Je! hii ni miaka elfu moja halisi, au inatupasa tuione kwa njia ya ufananisho kuwa ni kipindi kirefu cha wakati, kisichodhihirishwa? “Maelfu” yaweza kumaanisha hesabu kubwa isiyodhihirishwa, kama vile kwenye 1 Samweli 21:11. Lakini hapa “elfu” ni halisi, kwa kuwa inaonekana mara tatu katika Ufunuo 20:5-7 kama ile “miaka elfu.” Paulo aliita wakati huu wa hukumu “siku moja” alipotaarifu: “Yeye [Mungu] ameweka siku moja ambayo katika hiyo yeye anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa kwa uadilifu.” (Matendo 17:31, NW) Kwa kuwa Petro anatuambia kwamba siku moja kwa Yehova ni kama miaka elfu moja, inafaa kwamba hii Siku ya Hukumu iwe miaka elfu moja halisi.c—2 Petro 3:8, NW.
Mabaki ya Wafu
14. (a) Yohana hupachika taarifa gani juu ya “mabaki ya wafu”? (b) Semi za mtume Paulo zinanururishaje usemi ‘kuja kwenye uhai’?
14 Ingawa hivyo, hawa wafalme watahukumu nani ikiwa, kama vile mtume Yohana anapachika hapa, “(mabaki ya wafu hayakuja kwenye uhai mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha)”? (Ufunuo 20:5a, NW) Tena, usemi huu ‘kuja kwenye uhai’ wapasa ueleweke kulingana na muktadha. Usemi huu unaweza kuwa na maana tofautitofauti katika hali tofautitofauti. Mathalani, Paulo alisema juu ya Wakristo wenzake wapakwa-mafuta: “Ni nyinyi Mungu alifanya kuwa hai ingawa nyinyi mlikuwa wafu katika madhambi yenu.” (Waefeso 2:1, NW) Ndiyo, Wakristo wapakwa-mafuta kwa roho ‘walifanywa kuwa hai,’ hata katika karne ya kwanza, wakijulishwa kuwa waadilifu kwa msingi wa imani yao katika dhabihu ya Yesu.—Warumi 3:23, 24.
15. (a) Mashahidi wa kabla ya Ukristo walifurahia msimamo gani pamoja na Mungu? (b) Kondoo wengine ‘hujaje kwenye uhai,’ na ni wakati gani wao watamiliki dunia kwa maana iliyo kamili zaidi sana?
15 Hali moja na hiyo, mashahidi wa Yehova wa kabla ya Ukristo walijulishwa wazi kuwa waadilifu kwa habari ya kuwa na urafiki na Mungu; na Abrahamu, Isaka, na Yakobo walisemwa kuwa ‘wakiishi’ hata ingawa walikuwa wafu kimwili. (Mathayo 22:31, 32; Yakobo 2:21, 23) Hata hivyo, wao na wale wengine wote ambao wanafufuliwa, pamoja na umati mkubwa wa kondoo wengine waaminifu ambao wataokoka Har–Magedoni na watoto wowote ambao huenda wakazaliwa kwa hawa katika ulimwengu mpya, itakuwa ni lazima bado wainuliwe kwenye ukamilifu wa kibinadamu. Hilo litatimizwa na Kristo na wafalme na makuhani washirika wake wakati wa Siku ya Hukumu ya miaka elfu, kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. Kufikia mwisho wa hiyo Siku, “mabaki ya wafu” yatakuwa yamekwisha ‘kuja kwenye uhai’ katika maana ya kwamba watakuwa binadamu wakamilifu. Wanapoupita mtihani, Mungu atajulisha wazi kuwa wanastahili kuishi milele, wakiwa waadilifu katika maana iliyo kamili kabisa. Wataona utimizo kamili wa ahadi: “Waadilifu wenyewe watamiliki dunia, na wao wataishi milele juu yayo.” (Zaburi 37:29, NW) Lo! ni wenye kupendeza kama nini wakati ujao, kwa ajili ya aina ya binadamu yenye utii!
Ule Ufufuo wa Kwanza
16. Yohana huelezaje habari ya ufufuo wanaoupata wale wanaotawala pamoja na Kristo, na kwa nini?
16 Kurudi sasa kwa wale ambao ‘walikuja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo,’ Yohana aandika: “Huu ndio ufufuo wa kwanza.” (Ufunuo 20:5b) Ni wa kwanza jinsi gani? Ni “ufufuo wa kwanza” kwa habari ya wakati, kwa maana wale wanaoupata ni “matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 14:4, NW) Pia ni wa kwanza kwa umaana, kwa kuwa wale wanaoushiriki wanakuwa watawala wenzi wa Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu na wanahukumu mabaki ya aina ya binadamu. Kwa kumalizia, ni wa kwanza katika ubora. Isipokuwa Yesu Kristo mwenyewe, hao wanaoinuliwa katika ufufuo wa kwanza ndio viumbe pekee wanaosemwa katika Biblia kuwa wanapokea kutokufa.—1 Wakorintho 15:53; 1 Timotheo 6:16.
17. (a) Yohana huelezaje habari ya taraja lenye kubarikiwa la Wakristo wapakwa-mafuta? (b) “Kifo cha pili” ni nini, na kwa nini “hakina mamlaka” juu ya washindi 144,000?
17 Ni taraja lenye baraka kama nini kwa ajili ya hawa wapakwa-mafuta! Kama anavyojulisha wazi Yohana? “Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hawa kifo cha pili hakina mamlaka.” (Ufunuo 20:6a, NW) Kama vile Yesu alivyoahidi Wakristo katika Smirna, washindi hawa ambao wanashiriki “ufufuo wa kwanza” hawatakuwa katika hatari ya kupata dhara kutoka “kifo cha pili,” ambacho humaanisha utowesho, uharibifu pasi na tumaini la ufufuo. (Ufunuo 2:11; 20:14, NW) Kifo cha pili “hakina mamlaka” juu ya washindi kama hao, kwa maana wao watakuwa wamekwisha kuvaa kutofisidika na kutokufa.—1 Wakorintho 15:53.
18. Yohana anasema nini sasa juu ya watawala wapya wa dunia, nao watatimiza nini?
18 Ni tofauti kama nini na wafalme wa dunia wakati wa muda wa mamlaka ya Shetani! Hawa wametawala kwa muda usiozidi miaka 50 au 60 na walio wengi wao kwa miaka michache tu. Wengi wao wamekandamiza aina ya binadamu. Kwa vyovyote, mataifa yangenufaikaje daima chini ya watawala wenye kubadilika sikuzote na sera zenye kubadilika sikuzote? Kwa kutofautisha, Yohana husema kwa habari ya watawala wapya wa dunia: “Lakini wao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja na yeye kwa miaka elfu.” (Ufunuo 20:6b, NW) Wakiwa pamoja na Yesu, watafanyiza serikali iliyo pekee kwa miaka elfu moja. Utumishi wao wa kikuhani, katika kutumia ubora wa dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya Yesu, utainua binadamu watiifu wafikie ukamilifu wa kiroho, kiadili na kimwili. Utumishi wao wa kifalme utatokeza kujengwa kwa jamii ya kibinadamu ya tufe lote inayoonyesha uadilifu na utakatifu wa Yehova. Wakiwa mahakimu kwa miaka elfu moja, wao, pamoja na Yesu, wataongoza kwa upendo wanadamu waitikifu kuelekea mradi wa uhai wa milele.—Yohana 3:16.
Mtihani wa Mwisho
19. Kufikia mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu hali ya dunia na ya aina ya binadamu itakuwaje, na sasa Yesu anafanya nini?
19 Kufikia mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu, dunia yote itakuwa imekuja kushabihi Edeni ya awali kabisa. Itakuwa ni Paradiso halisi. Aina ya binadamu iliyo kamilifu haitahitaji tena kuhani mkuu wa kuiombea mbele za Mungu, kwa kuwa alama zote za dhambi ya Adamu zitakuwa zimekwisha kuondolewa na adui ya mwisho, kifo, kuletwa kwenye si kitu. Ufalme wa Kristo utakuwa umekwisha kufikia kusudi la Mungu la kuumba ulimwengu mmoja wenye serikali moja. Kufikia hatua hii, Yesu ‘akabidhi ufalme kwa Mungu na Baba yake.’—1 Wakorintho 15:22-26, NW; Warumi 15:12.
20. Yohana anatuambia ni nini kitakachotukia unapokuwa wakati wa ule mtihani wa mwisho?
20 Sasa ni wakati wa mtihani wa mwisho kabisa. Je! ulimwengu huo mkamilifu wa aina ya binadamu utasimama imara katika ukamilifu wao, tofauti na wale binadamu wa kwanza katika Edeni? Yohana atuambia yanayotukia: “Sasa mara miaka elfu inapokwisha, Shetani ataachwa legelege nje ya gereza lake, na yeye ataenda nje kuongoza vibaya yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu, kukusanya hayo pamoja kwenye vita. Hesabu ya hawa ni kama mchanga wa bahari. Na wao walisonga mbele juu ya upana wa dunia na kuzingira kambi ya watakatifu na jiji lenye kupendwa.”—Ufunuo 20:7-9a, NW.
21. Kwa jitihada yake ya mwisho, Shetani anaendeleaje, na kwa nini haipasi kutushangaza kwamba wengine watafuata Shetani hata baada ya Utawala wa Miaka Elfu?
21 Jitihada ya mwisho ya Shetani itakuwaje? Yeye anadanganya “yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu,” na kuyaongoza kwenye “vita.” Ni nani angeweza kuchukua upande wa Shetani baada ya miaka elfu moja ya utawala wa kitheokrasi wenye shangwe, wenye kujenga? Basi, usisahau kwamba Shetani aliweza kuongoza vibaya Adamu na Hawa wakamilifu walipokuwa wakifurahia uhai katika Paradiso ya Edeni. Na yeye aliweza kupotosha malaika wa kimbingu ambao walikuwa wameona matokeo mabaya ya uasi wa awali kabisa. (2 Petro 2:4; Yuda 6) Kwa hiyo tusishangae kwa vile baadhi ya wanadamu wakamilifu watarubuniwa wafuate Shetani hata baada ya utawala wa Ufalme wa Mungu wa miaka elfu wenye kupendeza.
22. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na usemi “yale mataifa katika kona nne za dunia”? (b) Kwa nini waasi huitwa “Gogu na Magogu”?
22 Biblia huwaita waasi hawa “mataifa katika kona nne za dunia.” Hii haimaanishi kwamba aina ya binadamu itakuwa imekwisha gawanyikana-gawanyikana tena na kuwa mataifa yaliyo pekee. Inaonyesha tu kwamba hawa watajitenga wenyewe kutoka kwa wale washikamanifu, na waadilifu wa Yehova na kudhihirisha roho ile ile mbaya ambayo mataifa yanaonyesha leo. Wao ‘watafikiria njama yenye kudhuru,’ kama alivyofanya Gogu wa Magogu katika unabii wa Ezekieli, wakiwa na mradi wa kuharibu serikali ya kitheokrasi iliyo duniani. (Ezekieli 38:3, 10-12, NW) Kwa sababu hiyo, wao huitwa “Gogu na Magogu.”
23. Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba hesabu ya waasi ni “kama mchanga wa bahari”?
23 Hesabu ya wale wanaojiunga na Shetani katika uasi wake itakuwa “kama mchanga wa bahari.” Huo ni wingi gani? Hakuna hesabu iliyotangulia kuwekwa rasmi. (Linga Yoshua 11:4; Waamuzi 7:12.) Hesabu ya mwisho yenye jumla ya waasi itategemea jinsi kila mtu mmoja mmoja atakavyotenda kwa kuitikia hila za ujanja za Shetani. Ingawa hivyo, pasi na shaka, watakuwa hesabu kubwa, kwa kuwa watahisi ni wenye nguvu vya kutosha kushinda “kambi ya watakatifu na jiji lenye kupendwa.”
24. (a) Ni nini lililo “jiji lenye kupendwa” nalo linaweza kuzingirwaje? (b) Ni nini kinachowakilishwa na “kambi ya watakatifu”?
24 “Jiji lenye kupendwa” lazima liwe jiji ambalo Yesu Kristo aliyetukuzwa anasema juu yalo kwa wafuasi wake kwenye Ufunuo 3:12 na ambalo yeye anaita “jiji la Mungu wangu, Yerusalemu jipya ambalo hushuka kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu wangu.” Kwa kuwa hili ni tengenezo la kimbingu, kani hizo za kidunia zingewezaje ‘kulizingira’? Ni kwa vile wao huzingira “kambi ya watakatifu.” Kambi huwa nje ya jiji; kwa hiyo, “kambi ya watakatifu” lazima iwakilishe wale walio duniani nje ya mahali pa kimbingu pa Yerusalemu Jipya ambao kwa ushikamanifu hutegemeza mpango wa Yehova wa kiserikali. Wakati waasi hao walio chini ya Shetani wanaposhambulia wale waaminifu, Bwana Yesu huona hilo kuwa ni shambulio juu ya yeye. (Mathayo 25:40, 45) “Yale mataifa” yatajaribu kufutilia mbali yote ambayo Yerusalemu Jipya la kimbingu limetimiza katika kufanya dunia paradiso. Hivyo kwa kushambulia “kambi ya watakatifu,” wao wanashambulia pia “jiji lenye kupendwa.”
Ziwa la Moto na Salfa
25. Yohana anaelezaje tokeo la shambulio la waasi juu ya “kambi ya watakatifu,” na litamaanisha nini kwa Shetani?
25 Je! jitihada hii ya mwisho kabisa ya Shetani itafaulu? Hakika sivyo—kama vile shambulio ambalo Gogu wa Magogu anatazamiwa kufanya juu ya Israeli wa kiroho katika siku yetu halitafaulu! (Ezekieli 38:18-23) Yohana anaeleza waziwazi tokeo: “Lakini moto ulikuja chini kutoka katika mbingu na ukameza wao. Na Ibilisi ambaye alikuwa anawaongoza vibaya alivurumishwa ndani ya ziwa la moto na salfa, ambamo wote wawili hayawani-mwitu na nabii bandia tayari walikuwa.” (Ufunuo 20:9b-10a, NW) Badala ya kutiwa ndani ya abiso tu, wakati huu Shetani, nyoka wa awali kabisa, atapondwapondwa kikweli asiweko, atasagwasagwa tikitiki, atoweshwe kabisa kabisa kana kwamba kwa moto.
26. Ni kwa nini “ziwa la moto na salfa” haviwezi kuwa mahali halisi pa mateso?
26 Sisi tumekwisha ona kwamba hilo “ziwa la moto na salfa” halingeweza kuwa mahali halisi pa mateso. (Ufunuo 19:20) Ikiwa Shetani angepaswa apate mateso yenye maumivu makali humo kwa umilele wote, Yehova angelazimika kumhifadhi hai. Hata hivyo, uhai ni zawadi, si adhabu. Kifo ndicho adhabu ya dhambi, na kulingana na Biblia, viumbe wafu hawahisi maumivu. (Warumi 6:23; Mhubiri 9:5, 10) Waaidha, tunasoma baadaye kwamba kifo chenyewe, pamoja na Hadesi, vinatupwa ndani ya ziwa ilo hilo la moto na salfa. Hakika, Kifo na Hadesi haviwezi kuona umivu.—Ufunuo 20:14.
27. Kilichopata Sodoma na Gomora hutusaidiaje sisi kuelewa usemi wa ziwa la moto na salfa?
27 Yote haya yanaongezea kani lile oni la kwamba ziwa la moto na salfa ni la ufananisho. Na zaidi, mtajo wa moto na salfa hurudisha akilini hukumu ya Sodoma na Gomora ya kale, yaliyoharibiwa na Mungu kwa sababu ya uovu wayo mkubwa sana. Wakati wayo ulipofika, “Yehova alifanya mvua inye salfa na moto kutoka kwa Yehova, kutoka katika mbingu, juu ya Sodoma na Gomora.” (Mwanzo 19:24, NW) Kilichopata majiji hayo kinaitwa “adhabu ya kihukumu ya moto wa milele.” (Yuda 7, NW) Hata hivyo, majiji hayo hayakupatwa na mateso ya milele. Badala ya hivyo, yalifutiliwa mbali, yakaondolewa kabisa kwa wakati wote, pamoja na wakazi wayo wafasiki. Majiji hayo hayako leo, na hakuna yeyote anayeweza kusema kwa uhakika mahali yalipokuwa.
28. Ziwa la moto na salfa ni nini, na ni jinsi gani si kama kifo, Hadesi, na abiso?
28 Kupatana na hili, Biblia yenyewe hueleza maana ya ziwa la moto na salfa: “Hii humaanisha kifo cha pili, ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14, NW) Kwa wazi ni sawa na Gehena ambayo Yesu alisema juu yayo, mahali waovu wanapobaki wameharibiwa, si kuteswa milele. (Mathayo 10:28) Ni uharibifu kabisa, ulio kamili bila tumaini la ufufuo. Hivyo, ingawa kuna funguo za kifo, Hadesi na abiso, hakuna mtajo wa ufunguo wa kufungua ziwa la moto na salfa. (Ufunuo 1:18; 20:1) Halitaachilia kamwe mateka walo.—Linga Marko 9:43-47.
Kuteswa Mchana na Usiku Milele
29, 30. Yohana anasema nini juu ya Ibilisi pamoja na hayawani-mwitu na nabii bandia, nalo hili lielewekeje?
29 Akirejezea Ibilisi pamoja na hayawani-mwitu na nabii bandia, sasa Yohana hutuambia: “Na wao watateswa mchana na usiku milele na milele.” (Ufunuo 20:10b, NW) Hili lingeweza kumaanisha nini? Kama ilivyokwisha kutajwa, si kimantiki kusema kwamba mifananisho, kama vile hayawani-mwitu na nabii bandia, pamoja na kifo na Hadesi, ingeweza kupatwa na teso kwa njia halisi. Kwa sababu hiyo, sisi hatuna sababu ya kuitikadi kwamba Shetani atakuwa akiteseka kwa umilele wote. Yeye apaswa kutoweshwa.
30 Neno la Kigiriki ambalo limetumiwa hapa kwa “tesa,” ba·sa·niʹzo, humaanisha kwanza kabisa “kutahini (madini) kwa kipimio.” “Kuhoji kwa kutumia teso” ni maana ya pili. (The New Thayer’s Greek-English Lexicon of the New Testament) Katika muktadha, utumizi wa neno hili la Kigiriki huonyesha kwamba kinachompata Shetani kitatumika, kwa umilele wote, kuwa kipimio juu ya suala la uhalali na uadilifu wa utawala wa Yehova. Suala hilo la utawala wa enzi kuu litakuwa limekwisha malizwa mara moja kwa wakati wote. Kukaidi enzi kuu ya Yehova hakutahitaji tena kamwe kutahiniwe kwa kipindi kirefu cha wakati ili kuthibitishwe kuwa kosa.—Linga Zaburi 92:1, 15.
31. Maneno mawili ya Kigiriki yanayohusiana na lile linalomaanisha “teso” hutusaidiaje kuelewa adhabu anayopata Shetani Ibilisi?
31 Kwa kuongezea, neno linalohusiana ba·sa·ni·stesʹ, “mtesi,” linatumiwa katika Biblia kumaanisha “mtunza-jela.” (Mathayo 18:34, Kingdom Interlinear) Kupatana na hili, Shetani atatiwa gerezani milele katika ziwa la moto; hataachiliwa kamwe. Kwa kumalizia, katika Septuagint ya Kigiriki ambayo Yohana aliijua vizuri, neno linalohusiana baʹsa·nos linatumiwa kurejezea utwezo unaoongoza kwenye kifo. (Ezekieli 32:24, 30) Hilo linatusaidia kuona kwamba adhabu anayopata Shetani ni kifo chenye kutweza, cha milele katika ziwa la moto na salfa. Kazi zake zinakufa pamoja naye.—1 Yohana 3:8
32. Ni adhabu gani ambayo roho waovu watapata na sisi twajuaje?
32 Tena, roho waovu hawatajwi katika mstari huu. Je! wao wataachiliwa pamoja na Shetani mwishoni mwa miaka elfu na kisha wapate adhabu ya kifo cha milele pamoja naye? Ithibati inajibu ndiyo. Katika fumbo la maneno juu ya kondoo na mbuzi, Yesu alisema kwamba mbuzi wangeenda zao waingie “katika moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake.” (Mathayo 25:41, NW) Usemi “moto wa milele” lazima urejezee ziwa la moto na salfa ambamo Shetani anavurumishwa. Malaika za Ibilisi walitupwa nje kutoka katika mbingu pamoja naye. Kwa wazi, walienda ndani ya abiso pamoja naye mwanzoni mwa Utawala wa Miaka Elfu. Kwa kupatana, basi, wao wataharibiwa pia pamoja naye katika ziwa la moto na salfa.—Mathayo 8:29.
33. Ni habari gani ya mwisho ya Mwanzo 3:15 itakayotimizwa wakati huo, na sasa roho ya Yehova yavuta uangalifu wa Yohana kwenye jambo gani?
33 Kwa njia hii, fasili ya mwisho ya unabii uliorekodiwa kwenye Mwanzo 3:15 inatimizwa. Shetani anapovurumishwa ndani ya hilo ziwa la moto, yeye atakuwa mfu kama nyoka ambaye kichwa chake kimesagwa chini ya kisigino cha chuma. Yeye na roho waovu wake watakuwa wameenda milele. Hawatajwi zaidi ya hapo katika kitabu cha Ufunuo. Sasa, ikiwa imekwisha ondolea mbali hawa kiunabii, roho ya Yehova inavuta uangalifu kwenye jambo lenye upendezi wa umuhimu kwa wale ambao hupokea tumaini la kidunia: Utawala wa kimbingu wa “Mfalme wa wafalme” na “wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye” utaitokezea nini aina ya kibinadamu? (Ufunuo 17:14, NW) Ili kujibu, Yohana anaturudisha tena kwenye mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu.
[Maelezo ya Chini]
a Maandiko mengine husema kwamba Yesu alikuwa katika Hadesi alipokuwa mfu. (Matendo 2:31, NW) Hata hivyo, haitupasi kukata maneno kwamba Hadesi na abiso sikuzote ni kitu kile kile. Ingawa hayawani-mwitu na Shetani huenda ndani ya abiso, ni wanadamu pekee ndio husemwa kuwa wanaenda kwenye Hadesi, wanamokuwa wamelala katika kifo mpaka ufufuo wao.—Ayubu 14:13; Ufunuo 20:13, NW.
b Shoka (Kigiriki, peʹle·kus) laonekana kuwa ndilo lililokuwa chombo cha kimapokeo cha kufisha katika Roma, ingawa kufikia siku ya Yohana upanga ulitumiwa kikawaida zaidi. (Matendo 12:2) Kwa hiyo, neno la Kigiriki lililotumiwa hapa, pe·pe·le·kis·meʹnon (“-liouawa kwa shoka”), lamaanisha tu “-liouawa.”
c Kwa kupendeza, Papiasi wa Hierapolisi, ambaye anaeleweka kuwa alipokea mengine ya maarifa ya Biblia yake kutoka kwa wanafunzi wa Yohana, mwandikaji wa Ufunuo, anaripotiwa na mwanahistoria wa karne ya nne Eusebio kuwa aliitikadi katika Utawala wa Miaka Elfu halisi wa Kristo (ijapokuwa Eusebio hakuafikiana naye hata kidogo).—The History of the Church, Eusebio, 3, 39.
-
-
Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 41
Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
Njozi ya 15—Ufunuo 20:11–21:8
Habari: Ufufuo wa watu wote, Siku ya Hukumu, na baraka za mbingu mpya na dunia mpya
Wakati wa utimizo: Utawala wa Miaka Elfu
1. (a) Aina ya binadamu ilipoteza nini wakati Adamu na Hawa walipofanya dhambi? (b) Ni kusudi gani la Mungu ambalo halijabadilika, na twajuaje?
TUKIWA wanadamu, tuliumbwa tuishi milele. Kama Adamu na Hawa wangalitii amri za Mungu, hawangalikufa. (Mwanzo 1:28; 2:8, 16, 17; Mhubiri 3:10, 11) Lakini walipofanya dhambi, walipoteza ukamilifu na uhai kwa ajili yao wenyewe na pia kwa ajili ya wazao wao, na kifo kikaja kutawala juu ya aina ya binadamu kikiwa adui asiyehurumia. (Warumi 5:12, 14; 1 Wakorintho 15:26) Hata hivyo, kusudi la Mungu la kuwa na wanadamu wakamilifu wakiishi milele juu ya dunia paradiso halikubadilika. Kwa sababu ya upendo wake mwingi kwa aina ya binadamu, yeye alituma duniani Mwana wake mzaliwa pekee, Yesu, ambaye alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu uwe ukombozi kwa ajili ya “wengi” wa wazao wa Adamu. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Sasa Yesu anaweza kutumia huu ubora wa kisheria wa dhabihu yake ili kurudisha wanadamu wenye kuitikadi kwenye ukamilifu wa uhai katika dunia paradiso. (1 Petro 3:18; 1 Yohana 2:2) Aina ya binadamu ina sababu tukufu kama nini ya ‘kujawa na shangwe na kushangilia’!—Isaya 25:8, 9, NW.
2. Yohana anaripoti nini kwenye Ufunuo 20:11, na “kiti cha ufalme kikubwa cheupe” ni nini?
2 Shetani akiwa amefungiwa ndani ya abiso, Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu unaanza. Sasa ni “siku” ambayo katika hiyo Mungu “anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa kwa uadilifu kwa mtu mmoja ambaye yeye ameweka rasmi.” (Matendo 17:31, NW; 2 Petro 3:8) Yohana ajulisha wazi: “Na mimi nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na mmoja aliyeketi juu yacho. Kutoka mbele zake dunia na mbingu zikakimbilia mbali, na mahali hapakupatikana kwa ajili yazo.” (Ufunuo 20:11, NW) Hiki “kiti cha ufalme kikubwa cheupe” ni nini? Hakiwezi kuwa kingine kuliko kikalio cha hukumu cha “Mungu Hakimu wa wote.” (Waebrania 12:23, NW) Sasa yeye atahukumu aina ya binadamu kwa habari ya ni nani atanufaika na dhabihu ya ukombozi ya Yesu.—Marko 10:45.
3. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba kiti cha ufalme cha Mungu kinasemwa kuwa “kikubwa” na “cheupe”? (b) Ni nani watakuwa wakihukumu kwenye Siku ya Hukumu, na kwa msingi gani?
3 Kiti cha ufalme cha Mungu ni “kikubwa,” kikikazia ukuu wa Yehova akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, na ni “cheupe,” kuvuta uangalifu kwenye uadilifu wake usio na kasoro. Yeye ndiye Hakimu wa mwisho kabisa wa aina ya binadamu. (Zaburi 19:7-11; Isaya 33:22; 51:5, 8) Hata hivyo, yeye amempa Yesu Kristo wakala wa kufanya kazi ya kuhukumu: “Baba hahukumu yeyote kabisa, bali yeye ameaminisha Mwana kuhukumu kote.” (Yohana 5:22, NW) Pamoja na Yesu ni washirika wake 144,000, ambao “nguvu za kuhukumu zilipewa kwao . . . kwa miaka elfu moja.” (Ufunuo 20:4, NW) Hata hivyo, viwango vya Yehova ndivyo vinaamua kitakachompata kila mtu mmoja mmoja wakati wa Siku ya Hukumu.
4. Maana yake nini kwamba “dunia na mbingu zikakimbilia mbali”?
4 Ni jinsi gani “dunia na mbingu zikakimbilia mbali”? Hii ni mbingu ile ile ambayo iliondoka kama hati-kunjo wakati wa kufunguliwa kifungo cha sita—serikali za kibinadamu zenye kutawala ambazo “zimewekwa akiba kwa ajili ya moto na zinawekwa kwa ajili ya siku ya hukumu na ya kuharibiwa kwa watu wasiohofu Mungu.” (Ufunuo 6:14; 2 Petro 3:7, NW) Dunia ni mfumo wa mambo uliopangwa kitengenezo ulio chini ya utawala huu. (Ufunuo 8:7) Uharibifu wa hayawani-mwitu na wafalme wa dunia na majeshi yao, pamoja na wale waliopokea alama ya hayawani-mwitu na wale waliotoa ibada kwa mfano wake, hutia alama ya kukimbilia mbali kwa hii mbingu na dunia. (Ufunuo 19:19-21) Hukumu ikiwa imetekelezwa juu ya dunia na mbingu za Shetani, Hakimu Mkuu aamuru kuwe na Siku ya Hukumu nyingine.
Siku ya Hukumu ya Miaka Elfu
5. Baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali, ni nani wanaobaki kuhukumiwa?
5 Ni nani wanaobaki wahukumiwe baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali? Si mabaki wapakwa-mafuta wa 144,000, kwa maana hawa wamekwisha hukumiwa na kutiwa muhuri. Ikiwa wapakwa-mafuta wowote bado watakuwa duniani baada ya Har–Magedoni, lazima wafe muda mfupi baada ya hapo na kupokea thawabu yao ya kimbingu kwa ufufuo. (1 Petro 4:17; Ufunuo 7:2-4) Hata hivyo, mamilioni ya umati mkubwa ambayo sasa yametoka katika dhiki kubwa yanasimama kwa wazi “mbele ya kiti cha ufalme.” Hawa wamekwisha kuhesabiwa kuwa waadilifu kwa ajili ya kuokolewa kwa sababu ya imani yao katika damu iliyomwagwa ya Yesu, lakini hukumu yao lazima iendelee kupitia muda wote wa miaka elfu kadiri Yesu aendeleavyo kuwaongoza kwenye “vibubujiko vya maji ya uhai.” Kisha, wakiwa wamekwisha rudishwa kwenye ukamilifu wa kibinadamu na baada ya hapo kutahiniwa, wao watajulishwa wazi kuwa waadilifu katika maana iliyo kamili zaidi sana. (Ufunuo 7:9, 10, 14, 17, NW) Watoto ambao huenda wakaokoka dhiki kubwa na watoto wowote wanaozaliwa kwa umati mkubwa wakati wa Mileani hali kadhalika watahitaji kuhukumiwa wakati wa miaka elfu.—Linga Mwanzo 1:28; 9:7; 1 Wakorintho 7:14.
6. (a) Ni msongamano gani anaoona Yohana, na ni nini linaloonyeshwa na maneno “wakubwa na wadogo”? (b) Mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu pasipo shaka yatatokezwaje?
6 Hata hivyo, Yohana aona msongamano mwingine wenye hesabu kubwa zaidi sana kuliko umati mkubwa wenye kuokoka. Utakuwa na hesabu yenye kufika maelfu ya mamiloni! “Na mimi nikaona wafu, wakubwa na wadogo, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na hati-kunjo zilifunguliwa.” (Ufunuo 20:12a, NW) “Wakubwa na wadogo” hutia ndani walio mashuhuri pamoja na wasio mashuhuri sana wa wanadamu ambao wameishi na wakafa kwenye dunia hii wakati wa miaka 6,000 iliyopita. Katika Gospeli ambayo Yohana aliandika muda mfupi baada ya Ufunuo, Yesu alisema kwa habari ya Baba yake: “Naye akampa [Yesu] amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:27-29) Ni mradi mkubwa ajabu kama nini—kutangua vifo na makaburi ya muda wote wa historia! Hapana shaka hayo mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu watatokezwa hatua kwa hatua hivi kwamba umati mkubwa—ambao ni wachache sana kwa kulinganisha—utaweza kushughulikia matatizo ambayo huenda yatazuka kwa sababu huenda mwanzoni wafufuliwa wakaelekea kufuata mtindo wao wa maisha ya kale, pamoja na udhaifu wa mnofu wao na mielekeo.
Nani Wanainuliwa na Kuhukumiwa?
7, 8. (a) Ni hati-kunjo gani inayofunguliwa, na ni jambo gani linalotukia baada ya hapo? (b) Ni kwa akina nani hakutakuwa na ufufuo?
7 Yohana anaongeza: “Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na wafu walihukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao. Na bahari ikatoa wafu wale walio ndani yayo na kifo na Hadesi vikatoa wafu wale walio ndani yavyo na wao walihukumiwa mmoja mmoja kulingana na matendo yao.” (Ufunuo 20:12b, 13, NW) Tamasha yenye kusisimua kweli kweli! ‘Bahari, kifo, na Hadesi’ kila mojapo inatimiza sehemu, lakini angalia kwamba semi hizi si za pekee baina yazo zenyewe.a Wakati Yona alipokuwa tumboni mwa samaki mmoja na kwa hiyo akawa katikati ya bahari, yeye alisema juu yake mwenyewe kuwa alikuwa katika Sheoli, au Hadesi. (Yona 2:2) Ikiwa mtu anashikwa na kifo cha Adamu, basi yaelekea yeye pia yumo katika Hadesi. Maneno haya ya kiunabii yanatoa uhakikisho imara kwamba hakuna hata mmoja atakayekosa kuonwa.
8 Bila shaka, kuna hesabu isiyojulikana ambayo haitafufuliwa. Miongoni mwa hawa wangekuwa waandishi na Mafarisayo waliomkataa Yesu na mitume, “mtu wa uasi-sheria” wa kidini, na Wakristo wapakwa-mafuta “ambao wameangukia mbali.” (2 Wathesalonike 2:3; Waebrania 6:4-6; Mathayo 23:29-33, NW) Yesu alisema pia juu ya watu walio kama mbuzi wakati wa mwisho wa huu ulimwengu ambao huenda ndani ya “moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake,” yaani, “kukatiliwa mbali milele.” (Mathayo 25:41, 46, NW) Hakuna ufufuo kwa hao!
9. Mtume Paulo anaonyeshaje kwamba baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo, na hao wanatia ndani akina nani?
9 Kwa upande mwingine, baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo huu. Mtume Paulo alionyesha hivyo wakati aliposema: “Mimi nina tumaini kuelekea Mungu . . . kwamba kutakuja kuwa na ufufuo wa wote walio waadilifu na wasio waadilifu.” (Matendo 24:15, NW) Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, “walio waadilifu” watatia ndani wanaume na wanawake waaminifu wa kale—Abrahamu, Rahabu, na wengine wengi—ambao walijulishwa wazi kuwa waadilifu kwa habari ya kuwa na urafiki na Mungu. (Yakobo 2:21, 23, 25) Katika kikundi iki hiki watakuwamo wale kondoo wengine waadilifu ambao walikufa wakiwa waaminifu kwa Yehova katika nyakati za ki-siku-hizi. Yaelekea, washika ukamilifu wote hao watafufuliwa mapema katika Utawala wa Mileani wa Yesu. (Ayubu 14:13-15; 27:5; Danieli 12:13; Waebrania 11:35, 39, 40) Pasi na shaka wengi wa hawa waadilifu waliofufuliwa watapewa migawo ya pendeleo la pekee katika kusimamia kazi kubwa mno ya urudisho katika Paradiso.—Zaburi 45:16; linga Isaya 32:1, 16-18; 61:5; 65:21-23.
10. Kati ya wale watakaofufuliwa, ni nani “wasio waadilifu”?
10 Ingawa hivyo, ni nani “wasio waadilifu” wanaotajwa katika Matendo 24:15, NW? Hawa wangetia ndani matungamo ya aina ya binadamu ambayo yamekufa muda wote wa historia, hasa wale ambao waliishi katika ‘nyakati za ujinga.’ (Matendo 17:30) Hawa, kwa sababu ya mahali walipozaliwa au wakati walimoishi, hawakuwa na fursa ya kujifunza kutii penzi la Yehova. Kwa kuongezea, huenda kukawa na baadhi ya waliosikia ujumbe wa wokovu lakini ambao hawakuitikia kikamili katika wakati huo au ambao walikufa kabla ya wao kuendelea kufikia wakfu na ubatizo. Katika ufufuo watu kama hao watahitaji kufanya marekebisho zaidi katika kufikiri na mwendo wao wa maisha ikiwa wao watanufaika na fursa hii kwa ajili ya kupata uhai wa milele.
Hati-Kunjo ya Uhai
11. (a) “Hati-kunjo ya uhai” ni nini, na ni majina ya nani yaliyorekodiwa katika hati-kunjo hii? (b) Ni kwa nini hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu?
11 Yohana husema juu ya “hati-kunjo ya uhai.” Hayo ni maandishi ya wale walio katika mstari wa kupokea uhai wa milele kutoka kwa Yehova. Majina ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu, ya umati mkubwa, na ya watu waaminifu wa kale, kama vile Musa, yameandikwa katika hati-kunjo hii. (Kutoka 32:32, 33; Danieli 12:1; Ufunuo 3:5, NW) Bado kufikia hapa, hakuna hata mmoja wa wale “wasio waadilifu” waliofufuliwa aliye na jina lake limeandikwa katika hati-kunjo ya uhai. Kwa hiyo hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu kuruhusu kuandikwa kwa majina ya wengine ambao wanakuja kustahili. Wale ambao majina yao hayapati kuandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai ‘wanavurumishwa ndani ya ziwa la moto.’—Ufunuo 20:15, NW; linga Waebrania 3:19.
12. Ni nini kitakachoamua kama mtu ataandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa, na Hakimu mwekwa wa Yehova aliwekaje kielelezo?
12 Basi, ni nini kitakachoamua kama mtu anapata kuandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa wakati huo? Sababisho kuu litakuwa lile lile kama lilivyokuwa katika siku ya Adamu na Hawa: utii kwa Yehova. Kama vile mtume Yohana alivyoandikia Wakristo wenzake wapendwa: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.” (1 Yohana 2:4-7, 17, NW) Kwa habari ya utii, Hakimu mwekwa wa Yehova aliweka kielelezo: “Ingawa [Yesu] alikuwa Mwana, yeye alijifunza kutii kutokana na vitu ambavyo yeye aliteseka; na baada ya yeye kuwa amefanywa mkamilifu, yeye alipata kuwa mwenye daraka la wokovu wa milele kwa wale wote wanaotii yeye.”—Waebrania 5:8, 9, NW.
Kufungua Hati-Kunjo Nyingine
13. Ni lazima wafufuliwa waonyesheje utii wao, na ni kanuni gani ambazo lazima wafuate?
13 Ni lazima hawa wafufuliwa waonyesheje utii wao? Yesu mwenyewe alielekeza kwenye amri mbili kubwa, akisema: “Ya kwanza ni, ‘Sikia O Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo mzima wote na kwa nafsi nzima yote na kwa akili nzima zote na kwa uthabiti mzima wote.’ Ya pili ni hii, ‘Lazima wewe upende jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Marko 12:29-31, NW) Pia kuna kanuni za Yehova zilizoimarishwa vizuri ambazo lazima wafuate, kama vile kukataa katakata kuiba, kusema uwongo, kuua kimakusudi, na utovu wa adili.—1 Timotheo 1:8-11; Ufunuo 21:8.
14. Ni hati-kunjo gani nyingine zinazofunguliwa, na ni mambo gani yaliyomo?
14 Hata hivyo, ndipo Yohana ametoka tu kutaja hati-kunjo nyingine ambazo zitafunguliwa wakati wa Utawala wa Mileani. (Ufunuo 20:12) Hizi zitakuwa nini? Nyakati fulani, Yehova ametoa maagizo yaliyo waziwazi katika hali maalumu. Mathalani, katika siku ya Musa yeye aliandaa mfululizo wa sheria zenye mambo mengi-mengi ambazo zilimaanisha uhai kwa Waisraeli ikiwa wangetii. (Kumbukumbu 4:40; 32:45-47) Wakati wa karne ya kwanza, maagizo mapya yalitolewa kusaidia waaminifu kufuata kanuni za Yehova chini ya mfumo wa mambo wa Kikristo. (Mathayo 28:19, 20; Yohana 13:34; 15:9, 10) Sasa Yohana anaripoti kwamba wafu ‘watahukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao.’ Kwa wazi, basi, kufunguliwa kwa hati-kunjo hizi kutatangaza matakwa ya Yehova yenye mambo mengi-mengi kwa ajili ya aina ya binadamu wakati wa miaka elfu. Kwa kutumia katika maisha yao virekebi na amri za hati-kunjo hizo, wanadamu watiifu wataweza kurefusha siku zao, wakifikia mwishowe uhai wa milele.
15. Ni kampeni ya kielimu ya aina gani itakayohitajiwa wakati wa ufufuo, na yaelekea ufufuo utaendeleaje?
15 Ni kampeni iliyopanuka kama nini ya elimu ya kitheokrasi itakayohitajiwa! Katika 2005 Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote walikuwa wakiongoza, kwa wastani, mafunzo ya Biblia 6,061,534 katika mahali pa namna namna. Lakini wakati wa ufufuo, mamilioni yasiyohesabika ya mafunzo, msingi wayo ukiwa Biblia na hati-kunjo mpya, yataongozwa bila shaka! Watu wote wa Mungu watahitaji kuwa walimu na kujitahidi wenyewe. Wafufuliwa, kadiri waendeleavyo, pasipo shaka watashiriki programu hii iliyo kubwa mno ya kufundisha. Yaelekea, ufufuo utaendelea katika njia ya kwamba wale walio hai watapata kuwa na shangwe ya kukaribisha na kufundisha washiriki wa jamaa wa zamani na watu waliojuana nao, ambao, nao kwa zamu yao, watapata kukaribisha na kufundisha wengine. (Linga 1 Wakorintho 15:19-28, 58.) Wale Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni sita ambao ni watendaji katika kueneza ukweli leo wanaweka msingi mwema kwa ajili ya mapendeleo wanayotumainia kupata katika wakati wa ufufuo.—Isaya 50:4; 54:13.
16. (a) Ni majina ya nani ambayo hayataandikwa katika hati-kunjo, au kitabu, ya uhai? (b) Ni nani wale ambao ufufuo wao utathibitika kuwa “wa uhai”?
16 Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, Yesu alisema kwamba ‘wale waliofanya mema hutoka na kuja kwenye ufufuo wa uhai, wale waliozoea vitu vibaya sana kwenye ufufuo wa hukumu.’ Hapa “uhai” na “hukumu” hutofautiana, kuonyesha kwamba wale wafufuliwa ambao ‘huzoea vitu vibaya sana’ baada ya kufundishwa katika Maandiko na hati-kunjo zilizovuviwa huhukumiwa kuwa hawastahili uhai. Majina yao hayataandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai. (Yohana 5:29, NW) Inaweza kuwa hivyo pia kwa wowote ambao hapo kwanza walifuata mwendo wa uaminifu lakini ambao, kwa sababu fulani, wanakengeuka katika wakati wa Utawala wa Miaka Elfu. Majina yanaweza kufutwa. (Kutoka 32:32, 33) Kwa upande mwingine, wale ambao kwa kutii hufuata vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo watatunza majina yao katika rekodi iliyoandikwa, hati-kunjo ya uhai, na kuendelea kuishi. Kwa wao, ufufuo utakuwa umethibitika kuwa “wa uhai.”
Mwisho wa Kifo na Hadesi
17. (a) Ni tendo gani zuri ajabu ambalo Yohana anaeleza? (b) Hadesi inaachwa tupu lini? (c) Kifo cha Adamu ‘kitavurumishwa ndani ya ziwa la moto lini’?
17 Kisha, Yohana anaeleza jambo fulani ambalo kweli ni zuri ajabu! “Na kifo na Hadesi vilivurumishwa ndani ya ziwa la moto. Hii humaanisha kifo cha pili, ziwa la moto. Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kitabu cha uhai alivurumishwa ndani ya ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14, 15, NW) Kufikia mwisho wa Siku ya Hukumu ya mileani, “kifo na Hadesi” vinaondolewa kabisa. Ni kwa nini hili lahusisha miaka elfu moja? Hadesi, ambalo ni kaburi la ujumla la aina ya binadamu, inaachwa ikiwa tupu wakati mtu wa mwisho aliye katika kumbukumbu la Mungu anapofufuliwa. Lakini maadamu binadamu wowote wanatiwa waa na dhambi iliyorithiwa, kifo cha Adamu kingali kipo pamoja nao. Wale wote wanaofufuliwa duniani, pamoja na umati mkubwa unaookoka Har–Magedoni, watahitaji kutii yaliyoandikwa katika hati-kunjo mpaka ubora wa dhabihu ya Yesu uwe umetumiwa kikamili ukiondoa magonjwa, uzee, na udhaifu mwingine uliorithiwa. Ndipo kifo cha Adamu, pamoja na Hadesi, ‘vinapovurumishwa ndani ya ziwa la moto.’ Vitakuwa vimeenda milele!
18. (a) Mtume Paulo anaelezaje habari ya fanikio la utawala wa Yesu akiwa Mfalme? (b) Yesu hufanya nini na jamaa ya kibinadamu kamilifu? (c) Kunatukia vitu gani vingine mwishoni mwa miaka elfu?
18 Hivyo, programu ambayo mtume Paulo anaeleza katika barua yake kwa Wakorintho itafikia ukamilisho: “Kwa maana lazima [Yesu] atawale akiwa mfalme mpaka Mungu ameweka maadui wote chini ya nyayo zake. Akiwa ndiye adui wa mwisho, kifo [cha Adamu] kitaletwa kwenye si kitu.” Kwafuata nini? “Wakati vitu vyote vitakuwa vimetiishwa kwake, ndipo Mwana mwenyewe pia atajitiisha mwenyewe kwa Mmoja ambaye alitiisha vitu vyote kwake.” Kwa maneno mengine, Yesu ‘amkabidhi ufalme Mungu na Baba yake.’ (1 Wakorintho 15:24-28, NW) Ndiyo, Yesu, akiwa amekwisha shinda kifo cha Adamu kupitia ubora wa dhabihu ya ukombozi wake, atakabidhi Baba yake, Yehova, jamaa ya kibinadamu kamilifu. Kwa wazi ni hapa mwishoni mwa miaka elfu, ndipo Shetani anaachiliwa na mtihani wa mwisho kabisa unafanyika kuamua ni majina ya nani yatabaki daima yamerekodiwa katika hati-kunjo ya uhai. “Jitahidini wenyewe kisulubu” ili jina lenu liwe miongoni mwayo!—Luka 13:24; Ufunuo 20:5, NW.
[Maelezo ya Chini]
a Wale wanaofufuliwa kutoka katika bahari hawangetia ndani wakazi wafisadi wa dunia walioangamia katika Gharika ya siku ya Noa; uharibifu huo ulikuwa wa kukata maneno, kama utakavyokuwa utekelezo wa hukumu ya Yehova katika dhiki kubwa.—Mathayo 25:41, 46; 2 Petro 3:5-7.
-
-
Mbingu Mpya na Dunia MpyaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 42
Mbingu Mpya na Dunia Mpya
1. Yohana anaeleza nini wakati malaika anapomrudisha kwenye mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu?
NJOZI hii tukufu inaendelea kukunjuka malaika anaporudisha Yohana kwenye mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu. Yeye anaeleza habari gani? “Na mimi nikaona mbingu mpya na dunia mpya; kwa kuwa mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza zilikuwa zimepitilia mbali, na bahari haipo tena.” (Ufunuo 21:1, NW) Mandhari yenye kuvutia yaonekana!
2. (a) Unabii wa Isaya juu ya mbingu mpya na dunia mpya ulitimizwaje juu ya Wayahudi waliorudishwa katika 537 K.W.K.? (b) Twajuaje kwamba kutakuwa na utimizo zaidi wa unabii wa Isaya, na ahadi hii inatimizwaje?
2 Mamia ya miaka kabla ya siku ya Yohana, Yehova alikuwa amesema kwa Isaya: “Kwa maana hapa mimi naumba mbingu mpya na dunia mpya; na vitu vya kwanza havitarudishwa kwenye akili, wala havitakuja juu kuingia ndani ya moyo.” (Isaya 65:17; 66:22, NW) Unabii huu ulitimizwa kwanza wakati Wayahudi waaminifu waliporudi Yerusalemu katika 537 K.W.K. baada ya uhamisho wao wa miaka 70 katika Babuloni. Katika urudisho huo, wao walifanyiza jamii iliyosafishwa, “dunia mpya,” chini ya mfumo mpya wa kiserikali, “mbingu mpya.” Hata hivyo, mtume Petro alielekeza kwenye utimizo zaidi wa unabii huo, akisema: “Lakini kuna mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizi uadilifu wapasa kukaa.” (2 Petro 3:13, NW) Yohana sasa anaonyesha kwamba ahadi hii inatimizwa wakati wa siku ya Bwana. “Mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza,” mfumo wa mambo uliopangwa kitengenezo wa Shetani ukiwa na muundo wao wa kiserikali wenye kuongozwa na Shetani na roho waovu wake, utapitilia mbali. “Bahari” yenye msukosuko ya aina ya binadamu yenye uovu, yenye kuasi itakoma kuwako. Mahali pazo patachukuliwa na “mbingu mpya na dunia mpya”—jamii mpya ya kidunia chini ya serikali mpya, Ufalme wa Mungu.—Linga Ufunuo 20:11.
3. (a) Yohana anaeleza habari ya nini, na Yerusalemu Jipya ni nini? (b) Yerusalemu Jipya ‘hujaje chini kutoka katika mbingu’?
3 Yohana anaendelea: “Mimi nikaona pia jiji takatifu, Yerusalemu Jipya, likija chini kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu na limetayarishwa kama bibi-arusi aliyerembwa kwa ajili ya mume wake.” (Ufunuo 21:2, NW) Yerusalemu jipya ni bibi-arusi wa Kristo, ambaye walio washiriki wake ni Wakristo wapakwa-mafuta ambao hubaki wakiwa waaminifu mpaka kifo na ambao huinuliwa wakawe wafalme na makuhani pamoja na Yesu aliyetukuzwa. (Ufunuo 3:12; 20:6) Kama vile Yerusalemu la kidunia lilivyopata kuwa kao la serikali katika Israeli wa kale, Yerusalemu Jipya lenye uzuri mwingi mno na Bwana-arusi wake huwa ndiyo serikali ya mfumo mpya wa mambo. Hii ndiyo mbingu mpya. ‘Bibi-arusi huja chini kutoka katika mbingu,’ si kihalisi, bali katika maana ya kuelekeza uangalifu kwenye dunia. Bibi-arusi wa Mwana-Kondoo atakuwa mwenzi-msaidizi wake wa kifalme katika kuendesha serikali yenye uadilifu juu ya aina ya binadamu yote. Baraka kweli kweli kwa dunia mpya!
4. Ni ahadi gani anayofanya Mungu inayofanana na ile aliyofanya kwa taifa jipya lililofanyizwa?
4 Yohana atuambia zaidi: “Pamoja na hayo mimi nilisikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema ya Mungu i pamoja na aina ya binadamu, na yeye atakaa pamoja na wao, na wao watakuwa vikundi vya watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja na wao.’” (Ufunuo 20:3, NW) Yehova alipofanya agano la Sheria pamoja na taifa la Israeli ambalo wakati huo lilikuwa jipya, yeye aliahidi: “Kwa hakika mimi nitaweka tabenakulo yangu katikati yenu nyinyi, na nafsi yangu haitakirihi nyinyi. Na mimi nitatembea kweli kweli katikati ya nyinyi na kujithibitisha mwenyewe kuwa Mungu wenu, na nyinyi, kwa upande wenu, mtajithibitisha wenyewe kuwa watu wangu.” (Walawi 26:11, 12, NW) Yehova anafanya sasa ahadi inayofanana na hiyo kwa wanadamu waaminifu. Wakati wa Siku ya Hukumu ya miaka elfu, wao watakuwa watu maalumu sana kwake.
5. (a) Mungu atakaaje na aina ya binadamu wakati wa Utawala wa Mileani? (b) Mungu atakaaje miongoni mwa aina ya binadamu baada ya Utawala wa Miaka Elfu?
5 Wakati wa Utawala wa Mileani, Yehova ‘atakaa’ miongoni mwa aina ya binadamu katika mpango wa muda, yeye akiwakilishwa na Mwana wake wa kifalme, Yesu Kristo. Hata hivyo, mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu, wakati Yesu anapomkabidhi Baba yake Ufalme, hakutahitajika mwakilishi au mwombezi wa kifalme. Yehova atakaa kiroho pamoja na “vikundi vya watu wake” katika njia ya kudumu na ya moja kwa moja. (Linga Yohana 4:23, 24.) Ni pendeleo la hali ya juu kama nini kwa ubinadamu uliorudishwa!
6, 7. (a) Ni ahadi zipi tukufu anazofumbua Yohana, na ni akina nani watakaofurahia baraka hizo? (b) Isaya anaelezaje habari ya paradiso ambayo ni ya kiroho na kimwili pia?
6 Yohana aendelea kusema: “Na yeye atapangusa kabisa kila chozi kutoka macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala hakutakuwapo kuomboleza wala kuguta wala umivu tena. Vitu vya kwanza vimepitilia mbali.” (Ufunuo 21:4, NW) Kwa mara nyingine tena, tunakumbushwa juu ya ahadi zilizovuviwa za mapema zaidi. Isaya alitazamia pia wakati ambapo kifo na kuomboleza vingekuwa havipo tena na mahali pa kihoro pangechukuliwa na mchachawo. (Isaya 25:8, 35:10; 51:11; 65:19) Yohana anathibitisha sasa kwamba ahadi hizi zina utimizo mzuri ajabu wakati wa Siku ya Hukumu ya miaka elfu. Kwanza umati mkubwa utajifurahisha baraka. “Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha ufalme,” akiendelea kuwachunga, “ataelekeza wao kwenye vibubujiko vya maji ya uhai. Na Mungu atapangusa kabisa kila chozi kutoka macho yao.” (Ufunuo 7:9, 17, NW) Lakini hatimaye wale wote ambao wamefufuliwa na kujizoeza imani katika mpango wa Yehova watakuwako pamoja nao, wakijifurahisha paradiso ambayo ni ya kiroho na kimwili pia.
7 “Ndipo,” asema Isaya, “macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.” Naam, “ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba” kwa nderemo. (Isaya 35:5, 6) Wakati huo, pia, “watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” (Isaya 65:21, 22) Kwa hiyo hawatang’olewa mizizi kutoka dunia.
8. Yehova mwenyewe anasema nini kwa habari ya kutegemeka kwa ahadi hizi tukufu?
8 Ni maono ya kimbele yaliyo mazuri kama nini yanayojaa akili zetu tutafakaripo juu ya ahadi hizi! Maandalizi mazuri ajabu yako akibani kwa ajili ya aina ya binadamu yenye uaminifu chini ya serikali yenye upendo ya kimbingu. Je! ahadi hizi ni nzuri mno zisiweze kuwa za kweli? Je! ni ndoto tu za mzee aliyehamishwa kwenye kisiwa cha Patmosi? Yehova mwenyewe anajibu: “Na Mmoja aketiye juu ya kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Mimi ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Pia, yeye asema: ‘Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’ Na yeye akasema kwa mimi: ‘Yamekwisha tukia! Mimi ndiye Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.’”—Ufunuo 21:5, 6a, NW.
9. Ni kwa nini baraka hizi za wakati ujao zinaweza kuonwa kuwa ni hakika kabisa zitatimizwa?
9 Ni kana kwamba Yehova mwenyewe alikuwa akitia saini ya dhamana au taitodidi kwenye baraka hizi za wakati ujao kwa ajili ya aina ya binadamu yenye uaminifu. Ni nani anayeweza kuthubutu kushuku Mdhamini kama huyo? Kwani, ahadi hizi za Yehova ni hakika sana hivi kwamba yeye hunena kama tayari zilitimia: “Yamekwisha tukia!” Je! Yehova siye “Alfa na Omega . . . , Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako na ambaye anakuja, yule Mweza Yote”? (Ufunuo 1:8, NW) Kweli kweli ndiye! Yeye mwenyewe hujulisha wazi: “Mimi ndiye wa kwanza na mimi ndiye wa mwisho, na mbali na mimi hakuna Mungu.” (Isaya 44:6, NW) Akiwa hivyo, yeye anaweza kuvuvia unabii na kuutimiza katika kila jambo dogo-dogo. Jinsi inavyoimarisha imani! Kwa hiyo yeye aahidi: “Tazama! Mimi ninafanya vitu vyote kuwa vipya”? Badala ya kushuku kama maajabu haya yatatukia kweli kweli, hakika ingetupasa tuwe tukitaka kujua: ‘Mimi binafsi inanipasa kufanya nini ili kurithi baraka hizo?’
“Maji” kwa Wenye Kiu
10. Ni “maji” gani ambayo Yehova anatoa, nayo yanasimamia nini?
10 Yehova mwenyewe ndiye anayejulisha wazi: “Yeyote anayeona kiu mimi nitampa kutoka kibubujiko cha maji ya uhai bure.” (Ufunuo 21:6b, NW) Ili kuzima kiu hicho, lazima mtu awe anaona uhitaji wake wa kiroho na awe na nia ya kukubali “maji” ambayo Yehova huandaa. (Isaya 55:1; Mathayo 5:3) “Maji” yapi? Yesu mwenyewe alijibu swali hilo alipokuwa akitoa ushahidi kwa mwanamke kando ya kisima katika Samaria. Yeye alimwambia: “Yeyote ambaye hunywa kutoka maji ambayo mimi nitampa yeye hataona kiu kamwe hata, lakini maji ambayo mimi nitampa yeye yatakuwa ndani ya yeye kibubujiko cha maji kikibubujika kupatia uhai wa milele.” Hicho “kibubujiko cha maji ya uhai” hutiririka kutoka kwa Mungu kupitia Kristo akiwa andalio lake kwa ajili ya kurudisha aina ya binadamu kwenye uhai mkamilifu. Kama mwanamke Msamaria, yatupasa sisi kuwa wenye hamu nyingi kama nini kunywa sana kutokana na kibubujiko hicho! Na kama mwanamke huyo, yatupasa kuwa tayari kama nini kuacha mapendezi ya kidunia na kupendelea kuwaambia wengine habari njema!—Yohana 4:14, 15, 28, 29, NW.
Wale Wanaoshinda
11. Ni ahadi gani ambayo Yehova anafanya, na maneno hayo yanatumika kwa nani kwanza?
11 Wale wanaokunywa ya hayo “maji” yenye kuburudisha lazima pia washinde, kama Yehova aendeleavyo kusema: “Yeyote ambaye anashinda atarithi vitu hivi, na mimi nitakuwa Mungu wake na yeye atakuwa mwana wangu.” (Ufunuo 21:7, NW) Ahadi hii inafanana na ile inayopatikana katika jumbe kwenye makundi saba; kwa sababu hiyo, maneno haya lazima yahusu kwanza wanafunzi wapakwa-mafuta. (Ufunuo 2:7, 11, 17, 26-28; 3:5, 12, 21, NW) Ndugu za kiroho za Kristo katika enzi zote wametazamia kwa hamu nyingi kuwa sehemu ya Yerusalemu Jipya. Wakishinda kama alivyoshinda Yesu, matumaini yao yatatimizwa.—Yohana 16:33.
12. Ahadi ya Yehova kwenye Ufunuo 21:7 itatimizwaje kuelekea umati mkubwa?
12 Umati mkubwa kutoka mataifa yote pia watazamia ahadi hii. Lazima wao pia washinde, wakitumikia Mungu kishikamanifu mpaka watoke katika dhiki kubwa. Ndipo wao watakapoingia katika urithi wao wa kidunia, ‘ufalme uliotayarishwa kwa ajili yao tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.’ (Mathayo 25:34, NW) Hawa pamoja na wengine wa kondoo wa Bwana wa kidunia ambao hupita mtihani mwishoni mwa miaka elfu huitwa “watakatifu.” (Ufunuo (20:9) Watafurahia uhusiano mtakatifu na wa kibaba na kimwana pamoja na Muumba wao, Yehova Mungu, wakiwa washiriki wa tengenezo lake la ulimwengu wote mzima.—Isaya 66:22; Yohana 20:31; Warumi 8:21.
13, 14. Ili kurithi ahadi tukufu za Mungu, ni mazoea gani ambayo ni lazima sisi tuepuke kwa dhati, na kwa nini?
13 Wakiwa na tazamio tukufu hili, ni jambo la maana kama nini kwamba Mashahidi wa Yehova sasa wabaki wakiwa safi bila vitu vyenye kunajisi vya ulimwengu wa Shetani! Sisi twahitaji kuwa imara, wenye dhati, na wenye kuazimia kwamba Ibilisi hatatuburuta kamwe na kutuingiza ndani ya kampuni ambayo Yehova mwenyewe anaeleza hapa? “Lakini kwa habari ya waoga na wale bila imani na wale ambao ni wenye kunyarafisha kwa uchafu wao na wauaji kimakusudi na waasherati na wale ambao huzoea uwasiliano na roho na waabudu sanamu na waongo wote, aria yao itakuwa katika ziwa ambalo huwaka moto na salfa. Hii humaanisha kifo cha pili.” (Ufunuo 21:8, NW) Ndiyo, yeye ambaye angekuwa mrithi lazima aepuke mazoea ambayo yamechafua huu mfumo wa mambo wa kale. Lazima yeye ashinde kwa kubaki akiwa mwaminifu usoni mwa mibano yote na vishawishi.—Warumi 8:35-39.
14 Jumuiya ya Wakristo, ijapokuwa inadai kuwa bibi-arusi wa Kristo, inatambuliwa kwa mazoea yenye kunyarafisha ambayo Yohana anaeleza hapa. Kwa hiyo inaenda kwenye uharibifu wa milele pamoja na sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa. (Ufunuo 18:8, 21) Hali kadhalika, wowote wa wapakwa-mafuta au wa umati mkubwa ambao huchukua mazoea kama hayo ya kufanya maovu, au kuanza kutia moyo yafanywe, wakabili uharibifu wa milele. Wakiendelea na matendo haya, hawatarithi ahadi hizi. Na katika dunia mpya, wowote wanaojaribu kuleta mazoea kama hayo wataharibiwa kwa kasi sana, wakiingia ndani ya kifo cha pili bila tumaini la ufufuo.—Isaya 65:20.
15. Ni nani wenye kutokeza wakiwa washindi, na Ufunuo unaletwa kwenye upeo wa hali ya juu sana kwa njozi gani?
15 Wenye kutokeza sana wakiwa washindi ni Mwana-Kondoo, Yesu Kristo, na bibi-arusi wake wa 144,000, Yerusalemu Jipya. Inafaa kama nini, basi, kwamba Ufunuo uletwe kwenye upeo wa hali ya juu sana kwa mwono wa mwisho, wa Yerusalemu Jipya wenye kupita ubora wote! Sasa Yohana anaeleza habari ya njozi nyingine moja ya mwisho.
-
-
Mbingu Mpya na Dunia MpyaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 302]
Katika jamii ya dunia mpya, kutakuwako kazi na ushirika wenye kujaa shangwe kwa wote
-
-
Jiji Lenye Uzuri wa Kung’aaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 43
Jiji Lenye Uzuri wa Kung’aa
Njozi ya 16—Ufunuo 21:9–22:5
Habari: Elezo la Yerusalemu Jipya
Wakati wa utimizo: Baada ya dhiki kubwa na Shetani kutiwa ndani ya abiso
1, 2. (a) Ni wapi malaika mmoja anakopeleka Yohana akaone Yerusalemu Jipya, na sisi tunaona tofauti gani hapa? (b) Ni kwa nini huu ndio upeo mtukufu wa Ufunuo?
MALAIKA alikuwa amempeleka Yohana jangwani akamwonyeshe Babuloni Mkubwa. Sasa mmojapo wa kikundi icho hicho cha kimalaika anaongoza Yohana kwenda kwenye mlima mrefu sana. Lo! anaona kitu tofauti kama nini! Hapa hapana jiji chafu, lenye ukosefu wa adili kama kahaba wa Kibabuloni, bali Yerusalemu Jipya—lenye kutakata, la kiroho, takatifu—nalo linashuka kutoka katika mbingu yenyewe.—Ufunuo 17:1, 5.
2 Hata Yerusalemu la kidunia halikuwa na utukufu kama huu. Yohana atuambia: “Na akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba yaliyojaa tauni saba za mwisho, na yeye akanena na mimi na kusema: ‘Njoo hapa, mimi nitaonyesha wewe bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.’ Kwa hiyo yeye akapeleka mimi mbali katika nguvu za roho kwenye mlima mkubwa na mrefu sana, na yeye akaonyesha mimi jiji takatifu Yerusalemu likija chini kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu na likiwa na utukufu wa Mungu.” (Ufunuo 21:9-11a, NW) Kutoka mahali hapo penye kufaa pa mlima huo mrefu kama mnara, Yohana anakagua jiji zuri katika vijambo vyalo vyote vyenye kupendeza. Watu wa imani wamekuwa na taraja lenye hamu nyingi la kuja kwalo tangu aina ya binadamu ilipoanguka ndani ya dhambi na kifo. Hatimaye ndilo hili! (Warumi 8:19; 1 Wakorintho 15:22, 23; Waebrania 11:39, 40) Ni jiji la kiroho zuri mno, lenye kufanyizwa kwa washika ukamilifu washikamanifu 144,000, lenye uzuri wa kung’aa katika utakatifu walo na likirudisha utukufu wenyewe wa Yehova. Huu ndio upeo mtukufu wa Ufunuo!
3. Yohana anaelezaje uzuri wa Yerusalemu Jipya?
3 Yerusalemu Jipya ni lenye kutia kimako kwa uzuri walo: “Mnururisho walo ulikuwa kama jiwe la thamani kubwa mno, kama jiwe la yaspa lenye kung’aa kwa uangavu sana kama fuwele. Lilikuwa lina ukuta mkubwa na ulioinuka juu sana na lilikuwa lina malango kumi na mawili, na kwenye malango malaika kumi na wawili, na majina yalikuwa yamechorwa ambayo ni yale ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli. Katika mashariki kulikuwa na malango matatu, na kaskazini malango matatu, na kusini malango matatu, na magharibi malango matatu. Ukuta wa jiji ulikuwa pia na mawe ya msingi kumi na mawili, na juu yayo majina kumi na mawili ya mitume wa Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 21:11b-14, NW) Inafaa kama nini kwamba gezo la kwanza ambalo Yohana anarekodi ni la uangavu wenye kuwaka! Lenye kung’aa kama bibi-arusi mpya, Yerusalemu Jipya linakuwa mwenzi anayefaa kwa Kristo. Huwaka kikweli, kama inavyoufaa uumbaji wa “Baba wa mianga ya kimbingu.”—Yakobo 1:17, NW.
4. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yerusalemu Jipya si taifa la Israeli wa mnofu?
4 Kwenye malango yalo 12, yamechorwa majina ya makabila 12 ya Israeli. Kwa hiyo, jiji hili la ufananisho ni lenye 144,000, waliotiwa muhuri “kutoka kila kabila la wana wa Israeli.” (Ufunuo 7:4-8, NW) Kupatana na hili, juu ya mawe ya msingi 12 yako majina ya wale mitume 12 wa Mwana-Kondoo. Ndiyo, Yerusalemu Jipya si taifa la kimnofu lenye kuasisiwa juu ya wana 12 wa Yakobo. Ni Israeli wa kiroho, lenye kuasisiwa juu ya “mitume na manabii.”—Waefeso 2:20, NW.
5. Ni nini kinachomaanishwa na “ukuta mkubwa na ulioinuka juu sana” wa Yerusalemu Jipya na uhakika wa kwamba malaika wanawekwa kwenye kila mwingilio?
5 Jiji hili la ufananisho lina ukuta mkubwa mno. Katika nyakati za kale, kuta za jiji zilijengwa kwa ajili ya usalama na ili kuzuia maadui. Ukuta wa Yerusalemu Jipya “mkubwa na ulioinuka juu sana” huonyesha kwamba li salama kiroho. Hakuna adui ya uadilifu, hakuna yeyote aliye mchafu na asiye haki, atakayeweza kupata kuingia. (Ufunuo 21:27) Lakini kwa wale wanaoruhusiwa waingie ndani, kuingia ndani ya jiji hili lenye uzuri ni kama kuingia Paradiso. (Ufunuo 2:7) Baada ya Adamu kutolewa nje, makerubi waliwekwa kwenye upande wa mbele wa Paradiso hiyo ya kwanza kabisa kuzuia nje wanadamu wachafu. (Mwanzo 3:24) Hali moja na hiyo, malaika wamewekwa kwenye kila mwingilio wa Yerusalemu jiji takatifu ili kuhakikisha usalama wa kiroho wa jiji. Kweli kweli, katika muda wote wa siku za mwisho, malaika wamekuwa wakilinda kundi la Wakristo wapakwa-mafuta, ambalo huwa Yerusalemu Jipya ili lisipatwe na uchafu wa Kibabuloni.—Mathayo 13:41.
Kulipima Jiji
6. (a) Yohana anaelezaje kupimwa kwa jiji, na kupimwa huku kunaonyesha nini? (b) Ni nini kinachoweza kueleza kwamba kipimo kilichotumiwa kilikuwa “kulingana na kipimo cha binadamu, wakati uo huo cha malaika”? (Ona kielezi cha chini.)
6 Yohana aendelea na simulizi lake: “Sasa mmoja ambaye alikuwa akinena na mimi alikuwa akishika mwanzi wa dhahabu ukiwa kipimo, ili kwamba yeye apate kupima jiji na malango yalo na ukuta walo. Na jiji lina miraba minne, na urefu walo ni mkubwa kama upana walo. Na yeye akapima jiji kwa mwanzi, farlong’i elfu kumi na mbili; urefu na upana walo na kimo vi sawa. Pia, yeye akapima ukuta walo, kyubiti mia moja na arobaini na nne, kulingana na kipimo cha binadamu, wakati uo huo cha malaika.” (Ufunuo 21:15-17, NW) Wakati patakatifu pa hekalu palipopimwa, hilo lilidhaminia utimizo wa makusudi ya Yehova juu yapo. (Ufunuo 11:1) Sasa, kupimwa kwa Yerusalemu Jipya na malaika huonyesha jinsi makusudi ya Yehova kwa habari ya jiji hili tukufu yasivyoweza kubadilika.a
7. Ni jambo gani lenye kutokeza kuhusu vipimo vya jiji hilo?
7 Hili ni jiji lenye kutokeza kama nini! Mchemraba kamilifu farlong’i 12,000 (kilometa zapata 2,220) katika mzingo, likizungukwa na ukuta wa kyubiti 144, au meta 64, za kimo. Hakuna jiji halisi lingeweza kuwa na vipimo kama hivyo. Lingefunika eneo lenye ukubwa wa takribani mara 14 ya Israeli ya ki-siku-hizi, na lingeenda juu kama mnara kwa takribani kilometa 560 kuingia ndani ya anga la juu zaidi! Ufunuo ulitolewa kwa ishara. Kwa hiyo, vipimo hivi vinatuambia nini juu ya Yerusalemu Jipya la kimbingu?
8. Ni nini kinachomaanishwa na (a) kuta za jiji za juu zenye kyubiti 144? (b) kipimo cha jiji chenye farlong’i 12,000? (c) jiji kuwa na umbo la mchemraba mkamilifu?
8 Kuta za juu zenye kyubiti 144 hutukumbusha kwamba jiji limefanyizwa kwa wana wa Mungu waliolelewa kiroho. Tarakimu 12 inayoonekana katika vipimo vya jiji—vyenye farlong’i 12,000 za urefu, upana, na kimo zikiwa sawa—hutumiwa kitamathali katika mazingira ya kitengenezo katika unabii wa Biblia. Kwa sababu hiyo, Yerusalemu Jipya ni mpango wa kitengenezo uliobuniwa vizuri sana kwa ajili ya kutimiza kusudi la Mungu la milele. Yerusalemu Jipya, pamoja na Mfalme Yesu Kristo, ni tengenezo la Ufalme wa Yehova. Halafu kuna umbo la jiji: mchemraba mkamilifu. Katika hekalu la Solomoni, Patakatifu Zaidi Sana, ulimokuwa uwakilisho wa kimfano wa kuwapo kwa Yehova, mlikuwamo mchemraba mkamilifu. (1 Wafalme 6:19, 20) Basi, inafaa kama nini kwamba Yerusalemu Jipya, likimulikwa na utukufu wa Yehova mwenyewe, huonwa kuwa mchemraba mkamilifu, wa kadiri kubwa! Vipimo vyalo vyote ni vyenye kusawazika kikamilifu. Ni jiji lisilo na kasoro za ukawaida, au taksiri.—Ufunuo 21:22.
Vifaa vya Ujenzi Vyenye Thamani
9. Yohana anaelezaje vifaa vya ujenzi vya jiji?
9 Yohana aendeleza elezo lake: “Sasa muundo wa ukuta walo ulikuwa yaspa, na jiji lilikuwa dhahabu safi kama kioo changavu. Misingi ya kuta za jiji ilikuwa imerembwa kwa kila namna ya jiwe la thamani: msingi wa kwanza ulikuwa yaspa, wa pili safirosi, ule wa tatu kalkedoni, wa nne emeraldi, wa tano sardoniksi, wa sita sardiosi, wa saba krisolito, wa nane berulosi, wa tisa topazi, wa kumi krisoprasosi, wa kumi na moja hayakintho-buluu, ule wa kumi na mbili amethistosi. Pia, malango kumi na mawili yalikuwa lulu kumi na mbili; kila lango lilikuwa limefanyizwa kwa lulu moja. Na njia pana ya jiji ilikuwa dhahabu safi, kama kioo chenye kuona ndani.”—Ufunuo 21:18-21, NW.
10. Ni nini kinachomaanishwa na uhakika wa kwamba jiji limejengwa kwa yaspa, dhahabu, na “kila namna ya jiwe la thamani”?
10 Mjengo wa jiji ni wenye uzuri wa kung’aa kikweli. Badala ya vifaa vya ujenzi vya kidunia, visivyodumu kama udongo-mnamo au jiwe, sisi tunasoma juu ya yaspa, dhahabu iliyosafishwa, na “kila namna ya jiwe la thamani.” Lo! jinsi hivyo vinavyotaswiri vifaa vya ujenzi vya kimbingu! Hakuna kitu kingeweza kuwa na uzuri mno zaidi ya hilo. Sanduku la agano la kale lilikuwa limefunikwa kwa dhahabu safi, na katika Biblia elementi hii mara nyingi huwakilisha vitu ambavyo ni vizuri na vyenye thamani. (Kutoka 25:11; Mithali 25:11; Isaya 60:6, 17) Lakini Yerusalemu Jipya zima, na hata njia pana yalo, vimejengwa kwa “dhahabu safi kama kioo changavu,” kutaswiri uzuri na thamani asilia inayoshinda wazo.
11. Ni nini kinachohakikisha kwamba wale wanaojumlika kuwa Yerusalemu Jipya watawaka kwa ubora ulio wa juu zaidi sana wa usafi wa kiroho?
11 Hakuna msafishaji vito binadamu anayeweza kutokeza dhahabu yenye usafi hivyo. Lakini Yehova ndiye Msafishaji Stadi. Yeye huketi “akiwa msafishaji na mtakasaji fedha,” na yeye husafisha washiriki waaminifu mmoja mmoja wa Israeli wa kiroho “kama dhahabu na kama fedha,” akiondoa kutoka kwao taka zote. Watu mmoja mmoja ambao wamesafishwa na kutakaswa kikweli, hao pekee ndio mwishowe watajumlika kuwa Yerusalemu Jipya, na katika njia hii Yehova hujenga jiji kwa vifaa vya ujenzi vilivyo hai ambavyo huwaka kwa ubora wa juu zaidi sana wa usafi wa kiroho.—Malaki 3:3, 4, NW.
12. Ni nini kinachoashiriwa na uhakika wa kwamba (a) misingi ya jiji imerembwa kwa vito vya thamani 12? (b) malango ya jiji ni lulu?
12 Hata misingi ya jiji ni mizuri, ikiwa imerembwa kwa vito vya thamani 12. Hii hukumbusha akilini kuhani mkuu wa Kiyahudi, ambaye katika siku za kisherehe alivalia efodi iliyotiwa njumu za mawe yenye thamani tofautitofauti 12 ambayo kidogo yafanana na haya ambayo yameelezwa hapa. (Kutoka 28:15-21) Hakika si sadifa! Badala ya hivyo, hukazia utendaji wa kikuhani wa Yerusalemu Jipya, ambalo Yesu, Kuhani Mkuu, ndiye “taa” yalo. (Ufunuo 20:6; 21:23; Waebrania 8:1) Pia, zile manufaa za huduma ya Yesu ya ukuhani-mkuu huwasilishwa kwa aina ya binadamu kupitia Yerusalemu Jipya. (Ufunuo 22:1, 2) Malango 12 ya jiji, kila moja likiwa lulu moja ya uzuri mkubwa, hukumbusha kielezi cha Yesu kilichofananisha Ufalme na lulu moja ya thamani kubwa. Wote ambao huingia kupitia malango haya watakuwa wamekwisha onyesha uthamini wa kweli kwa ajili ya thamani za kiroho.—Mathayo 13:45, 46; linga Ayubu 28:12, 17, 18.
Jiji la Nuru
13. Halafu, Yohana anasema nini kwa habari ya Yerusalemu Jipya, na kwa nini jiji halihitaji hekalu lolote halisi?
13 Wakati wa Solomoni, lililokuwa lenye kutokeza zaidi katika Yerusalemu ni hekalu lililojengwa mahali palipoinuka zaidi sana pa jiji katika Mlima Moria kuelekea kaskazini. Lakini vipi Yerusalemu Jipya? Yohana asema: “Na mimi sikuona hekalu ndani yalo, kwa maana Yehova Mungu Mweza Yote ndiye hekalu lalo, pia Mwana-Kondoo. Na jiji hilo halina uhitaji wa jua wala mwezi kung’aa juu yalo, kwa maana utukufu wa Mungu ulilinururisha, na taa yalo ilikuwa ni Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 21:22, 23, NW) Kwa kweli, hakuna haja ya kujenga hekalu halisi hapa. Hekalu la kale la Kiyahudi lilikuwa kigezo, na uhalisi wa kigezo hicho, hekalu kubwa la kiroho, umekuwako tangu Yehova alipompaka mafuta Yesu awe Kuhani Mkuu katika 29 W.K. (Mathayo 3:16, 17; Waebrania 9:11, 12, 23, 24) Pia hekalu hutangulia kudokezea jamii ya kikuhani ikitoa dhabihu kwa Yehova kwa ajili ya watu. Lakini wale wote ambao wanajumlika kuwa Yerusalemu Jipya ni makuhani. (Ufunuo 20:6) Na dhabihu kubwa, uhai mkamilifu wa kibinadamu wa Yesu, umekwisha tolewa mara moja kwa wakati wote. (Waebrania 9:27, 28) Na zaidi, Yehova anafikilika kibinafsi na yeyote anayeishi katika jiji.
14. (a) Ni kwa nini Yerusalemu Jipya halihitaji jua na mwezi kung’aa juu yalo? (b) Unabii wa Isaya ulitabiri nini kwa habari ya tengenezo la ulimwengu wote mzima la Yehova, na Yerusalemu Jipya lahusikaje katika hili?
14 Utukufu wa Yehova ulipopita karibu na Musa kwenye Mlima Sinai, ulifanya uso wa Musa kung’aa kwa uangavu mkubwa sana hivi kwamba yeye alilazimika kuufunika usionwe na Waisraeli wenzake. (Kutoka 34:4-7, 29, 30, 33) Basi, wewe unaweza kuwazia uangavu wa jiji ambalo hunururishwa daima na utukufu wa Yehova? Jiji kama hilo halingeweza kuwa na wakati wa usiku. Halingekuwa na uhitaji wa jua wala mwezi halisi. Lingekuwa likitoa nuru kwa umilele. (Linga 1 Timotheo 6:16.) Yerusalemu Jipya huoshwa na aina kama hiyo ya uangavu wenye kung’aa. Kweli kweli, bibi-arusi huyu pamoja na Bwana-arusi Mfalme wake wanakuwa ndio jiji kuu la tengenezo la Yehova la ulimwengu wote mzima—“mwanamke” wake, “Yerusalemu juu”—ambaye kwa habari zake Isaya aliandika hivi: “Kwako wewe jua halitathibitika tena kuwa nuru wakati wa mchana, na kwa uangavu mwezi wenyewe hautakupa wewe nuru tena. Na lazima Yehova awe kwako wewe nuru yenye kudumu kwa wakati usio dhahiri, na Mungu wako uzuri wako. Jua lako halitashuka tena, wala mwezi wako hautafifia; kwa maana Yehova mwenyewe atakuwa kwa ajili yako nuru yenye kudumu kwa wakati usio dhahiri, na siku za kuomboleza kwako zitakuwa zimekwisha kuja kwenye utimilifu.”—Isaya 60:1, 19, 20; Wagalatia 4:26, NW.
Nuru kwa Ajili ya Mataifa
15. Ni maneno gani ya Ufunuo juu ya Yerusalemu Jipya ambayo ni kama ya unabii wa Isaya?
15 Unabii uu huu ulitabiri pia: “Na mataifa kwa hakika yataenda kwenye nuru yako, na wafalme kwa uangavu wa kung’aa kwako.” (Isaya 60:3, NW) Ufunuo unaonyesha kwamba maneno haya yangetia ndani Yerusalemu Jipya: “Na mataifa yatatembea kwa njia ya nuru yalo, na wafalme wa dunia wataleta utukufu wao ndani yalo. Na malango yalo hayatafungwa hata kidogo mchana, kwa maana usiku hautakuwa huko. Na wao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yalo.”—Ufunuo 21:24-26, NW.
16. Ni nani walio “mataifa” ambayo yatatembea kwa njia ya nuru ya Yerusalemu Jipya?
16 Ni nani walio “mataifa” haya yanayotembea kwa njia ya nuru ya Yerusalemu Jipya? Hao ni watu, waliokuwa wakati mmoja sehemu ya mataifa ya huu ulimwengu mbovu, ambao huitikia nuru inayotolewa kupitia jiji hili tukufu la kimbingu. Wa kwanza kabisa katika hao ni umati mkubwa, ambao tayari umetoka katika “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi” na ambao huabudu Mungu mchana na usiku wakiwa kampuni moja na jamii ya Yohana. (Ufunuo 7:9, 15, NW) Baada ya Yerusalemu Jipya kuja chini kutoka katika mbingu na Yesu kutumia funguo za kifo na za Hadesi kufufua wafu, wao wataungwa na mamilioni zaidi, ambao hapo awali walitoka katika “mataifa,” wanaokuja kumpenda Yehova na Mwana wake, Mume wa Yerusalemu Jipya aliye mithili ya Mwana-Kondoo.—Ufunuo 1:18.
17. Ni nani walio “wafalme wa dunia” ambao ‘huleta utukufu wao’ ndani ya Yerusalemu Jipya?
17 Basi, ni nani wale “wafalme wa dunia” ambao ‘wanaleta utukufu wao ndani yalo’? Wao si wafalme halisi wa dunia wakiwa kikundi, kwa maana wao wanaenda chini kwenye uharibifu wakipiga vita dhidi ya Ufalme wa Mungu kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16; 19:17, 18) Je! wafalme wangeweza kuwa watu mashuhuri wa mataifa wanaokuwa sehemu ya umati mkubwa, au je! wao ni wafalme waliofufuliwa ambao wanatii Ufalme wa Mungu katika ulimwengu mpya? (Mathayo 12:42) Hata, kwa sababu kwa sehemu iliyo kubwa, utukufu wa wafalme kama hao ulikuwa wa kilimwengu na tangu hapo umefifia. Basi, “wafalme wa dunia,” wanaoleta utukufu wao ndani ya Yerusalemu Jipya lazima wawe 144,000, ambao ‘walinunuliwa kutoka kila kabila na ulimi na kikundi cha watu na taifa’ wakatawale wakiwa wafalme pamoja na Mwana-Kondoo, Yesu Kristo. (Ufunuo 5:9, 10; 22:5, NW) Wanaleta utukufu wao waliopewa na Mungu ndani ya jiji waongezee mng’ao walo.
18. (a) Ni nani ambao hawataruhusiwa kuingia katika Yerusalemu Jipya? (b) Ni nani pekee watakaoruhusiwa kuingia ndani ya hilo jiji?
18 Yohana aendelea: “Lakini kitu chochote kisicho kitakatifu na yeyote ambaye huendeleza kitu cha kunyarafisha na uwongo hataingia ndani yalo kwa vyovyote; ila wale tu walioandikwa katika hati-kunjo ya uhai ya Mwana-Kondoo. (Ufunuo 21:27, NW) Hakuna kitu kilichotiwa waa na mfumo wa mambo wa Shetani kinachoweza kuwa sehemu ya Yerusalemu Jipya. Hata ingawa malango yalo yanafunguliwa daima, hakuna yeyote “ambaye huendeleza kitu cha kunyarafisha na uwongo” atakayeruhusiwa kuingia. Hakutakuwa na waasi-imani katika jiji hilo wala mshiriki yeyote wa Babuloni Mkubwa. Na ikiwa wowote wanajaribu kuchafua jiji kwa kufisidi washiriki walo wa wakati ujao wakiwa wangali duniani, jitihada zao zinafanywa kuwa za bure. (Mathayo 13:41-43) “Wale tu walioandikwa katika hati-kunjo ya uhai ya Mwana-Kondoo,” 144,000 ndio mwishowe huingia ndani ya Yerusalemu Jipya.b—Ufunuo 13:8; Danieli 12:3, NW.
Mto wa Maji ya Uhai
19. (a) Yohana huelezaje Yerusalemu Jipya likiwasilisha baraka kwa aina ya binadamu? (b) “Mto wa maji ya uhai” hutiririka lini, na twajuaje?
19 Lile jiji lenye uzuri wa kung’aa litawasilisha baraka tukufu kwa aina ya binadamu duniani. Hilo ndilo Yohana anafuata kujifunza: “Na yeye akanionyesha mto wa maji ya uhai, mwangavu kama fuwele ukitiririka nje kutoka kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kuteremka chini katikati ya njia pana yalo.” (Ufunuo 22:1, 2a, NW) “Mto” huu hutiririka lini? Kwa kuwa huo hutiririka “nje kutoka kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo,” hiyo ingeweza kuwa tu baada ya siku ya Bwana kuanza katika 1914. Huo ndio uliokuwa wakati wa lile tukio lililotolewa habari kwa kupulizwa kwa tarumbeta ya saba na tangazo tukufu: “Sasa kumetukia wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake.” (Ufunuo 11:15; 12:10, NW) Katika nyakati za mwisho, roho na bibi-arusi wamekuwa wakiwaalika watu wenye mwelekeo unaofaa wanywe maji ya uhai bure. Maji ya mto huo yataendelea kupatikana kwa ajili ya watu kama hao mpaka mwisho wa mfumo huu wa mambo na, baadaye kuendelea katika ulimwengu mpya, wakati Yerusalemu Jipya ‘linapokuja chini kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu.’—Ufunuo 21:2, NW.
20. Ni nini kinachoonyesha kwamba kipimo fulani cha maji ya uhai tayari kinapatikana?
20 Hii si mara ya kwanza ambapo maji yenye kutoa uhai yametolewa kwa aina ya binadamu. Alipokuwa duniani, Yesu alisema juu ya maji ambayo yalitoa uhai wa milele. (Yohana 4:10-14; 7:37, 38) Na zaidi, Yohana anakaribia kusikia mwaliko wenye upendo: “Roho na bibi-arusi hufuliza kusema: ‘Njoo!’ Na acha yeyote anayesikia aseme: ‘Njoo!’ Na acha yeyote anayeona kiu aje; acha yeyote ambaye anataka atwae maji ya uhai bure.” (Ufunuo 22:17, NW) Mwaliko huo huvumishwa hata sasa, kuonyesha kwamba tayari kipimo fulani cha maji ya uhai kinapatikana. Lakini katika ulimwengu mpya, maji hayo yatatiririka kutoka katika kiti cha ufalme cha Mungu na kupitia Yerusalemu Jipya yakiwa mto halisi.
21. Ni nini kinachowakilishwa na “mto wa maji ya uhai,” na njozi ya Ezekieli ya mto huu hutusaidiaje kujua?
21 Huu “mto wa maji ya uhai” ni nini? Maji halisi ni elementi muhimu kwa uhai. Mtu anaweza kuendelea kuishi bila chakula kwa majuma kadhaa, lakini bila maji yeye atakufa kwa muda kama wa juma moja. Pia maji ni kitu kinachosafisha na ni muhimu kwa afya. Hivyo, maji ya uhai lazima yawakilishe kitu fulani cha maana kabisa kwa uhai na afya ya aina ya binadamu. Nabii Ezekieli alionyeshwa pia njozi moja ya huu “mto wa maji ya uhai,” na katika njozi yake, mto huo ulitiririka kwenda nje kutoka hekalu na kuteremka chini kuingia ndani ya ile Baharifu. Kisha, muujiza wa miujiza! Mkusanyiko huo wa maji yasiyo na uhai, uliojaa kemikali uligeuzwa kuwa maji matamu yenye kujaa samaki! (Ezekieli 47:1-12) Ndiyo, mto wa kinjozi unakumbusha kitu fulani ambacho hapo awali kilikuwa kifu, kuthibitisha kwamba mto wa maji ya uhai ni picha ya uandalizi wa Mungu kupitia Yesu Kristo kwa ajili ya kurudisha uhai mkamilifu kwa jamii ya kibinadamu ‘yenye ufu.’ Mto huu ni “mwangavu kama fuwele,” kuonyesha usafi na utakatifu wa uandalizi wa Mungu. Si kama “maji” ya Jumuiya ya Wakristo yenye madoa ya damu, yenye kuleta kifo.—Ufunuo 8:10, 11.
22. (a) Mto hutoka wapi, na kwa nini hili lafaa? (b) Ni nini kinachohusishwa katika maji ya uhai, na mto huu wa ufananisho unatia ndani nini?
22 Huo mto hutoka kwenye “kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.” Hii inafaa, kwa kuwa msingi wa maandalizi yenye kutoa uhai ya Yehova ni dhabihu ya ukombozi, na hiyo iliandaliwa kwa sababu Yehova “alipenda ulimwengu kadiri hiyo hivi kwamba yeye alitoa Mwana mzaliwa-pekee wake, ili kwamba kila mmoja anayejizoeza imani katika yeye asipate kuharibiwa bali awe na uhai wa milele.” (Yohana 3:16, NW) Maji ya uhai huhusisha pia Neno la Mungu, ambalo husemwa kuwa maji katika Biblia. (Waefeso 5:26) Hata hivyo, mto wa maji ya uhai hutia ndani si ukweli tu bali pia kila uandalizi mwingine wa Yehova, wenye kutegemea dhabihu ya Yesu, kwa ajili ya kuponesha wanadamu watiifu kutoka dhambi na kifo na kuwapa uhai wa milele.—Yohana 1:29; 1 Yohana 2:1, 2.
23. (a) Ni kwa nini inafaa kwamba mto wa maji ya uhai hutiririka kupitia njia pana ya Yerusalemu Jipya? (b) Ni ahadi gani ya kimungu aliyopewa Abrahamu itatimizwa wakati maji ya uhai yatatiririka kwa utele?
23 Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu, manufaa za ule ukombozi zitatumiwa kikamili kupitia ukuhani wa Yesu na makuhani walio chini yake 144,000. Kwa kufaa, basi, mto wa maji ya uhai hutiririka kupitia katikati ya njia pana ya Yerusalemu Jipya. Walio washiriki walo ni Israeli wa kiroho, ambao pamoja na Yesu hujumlika kuwa mbegu ya kweli ya Abrahamu. (Wagalatia 3:16, 29) Kwa hiyo, maji ya uhai yanapotiririka kwa utele kupitia katikati ya njia pana ya jiji la ufananisho, “mataifa yote ya dunia” yatapata fursa kamili ya kujibarikia yenyewe kwa njia ya mbegu ya Abrahamu. Ahadi ya Yehova kwa Abrahamu itatimizwa kikamili.—Mwanzo 22:17, 18.
Miti ya Uhai
24. Yohana anaona nini sasa katika pande zote mbili za mto wa maji ya uhai, nayo ni picha ya nini?
24 Katika njozi ya Ezekieli, mto hata ukawa mvo, na nabii akaona ikikua katika pande zao zote mbili namna zote za miti yenye kuzaa matunda. (Ezekieli 47:12) Lakini Yohana anaona nini? Hili: “Na upande huu wa mto na upande ule kulikuwa na miti ya uhai ikifanyiza mazao kumi na mawili ya tunda, ikitoa matunda yayo kila mwezi. Na majani ya miti yalikuwa kwa ajili ya kuponeshwa kwa mataifa.” (Ufunuo 22:2b, NW) Hii “miti ya uhai” lazima pia iwe picha ya uandalizi wa Yehova kwa ajili ya kutoa uhai wa milele kwa aina ya binadamu tiifu.
25. Ni uandalizi gani ulio tele ambao Yehova hufanyia binadamu waitikivu katika Paradiso ya tufe lote?
25 Lo! ni uandalizi tele kama nini ambao Yehova anafanyia binadamu waitikivu! Si kwamba wanaweza kushiriki tu hayo maji ya uhai yenye kuburudisha bali waweza wakatunda kutoka miti hiyo namna namna yenye kuendelea ya matunda yenye kudumisha uhai. Oh, laiti wazazi wetu wa kwanza wangalitosheka na uandalizi unaofanana na huu ‘wenye kutamanika’ katika Paradiso ya Edeni! (Mwanzo 2:9) Lakini sasa Paradiso ya tufe lote ipo hapa, na Yehova hata hufanya uandalizi kupitia majani ya miti hiyo ya ufananisho kwa ajili ya “kuponeshwa kwa mataifa.”c Ukiwa wa hali ya juu zaidi kuliko dawa yoyote, ya miti-shamba au nyingineyo, ambayo hutolewa leo, utumizi wenye kutuliza wa majani hayo ya ufananisho utainua aina ya binadamu yenye kuitikadi kwenye ukamilifu wa kiroho na kimwili.
26. Yamkini pia miti ya uhai inatia ndani nini, na kwa nini?
26 Miti hiyo, ikiwa inatiliwa maji vizuri na mto, huenda kwa kuongezea ikatia ndani washiriki 144,000 wa mke wa Mwana-Kondoo. Wanapokuwa duniani hao pia wanakunywa kutokana na uandalizi wa Mungu kwa ajili ya uhai kupitia Yesu Kristo. Ndugu hao za Yesu waliozaliwa kwa roho wanaitwa kiunabii “miti mikubwa ya uadilifu.” (Isaya 61:1-3, NW; Ufunuo 21:6) Tayari wao wamefanyiza tunda jingi la kiroho kwa sifa ya Yehova. (Mathayo 21:43) Na wakati wa Utawala wa Miaka Elfu, watashiriki sehemu ya kutoa maandalizi ya ukombozi ambayo yatatumika kwa “kuponeshwa kwa mataifa” dhambi na kifo.—Linga 1 Yohana 1:7.
Hakuna Usiku Tena
27. Ni baraka zipi zaidi anazotaja Yohana kwa ajili ya wale wanaopendelewa kuingia ndani ya Yerusalemu Jipya, na ni kwa nini inasemwa kwamba “hakutakuwa tena na laana yoyote”?
27 Kuingia ndani ya Yerusalemu Jipya—hakika, hakungeweza kuwa na pendeleo zuri ajabu kupita hilo! Fikiri tu—hao ambao wakati mmoja walikuwa binadamu dhalili, wasiokamilika watafuata Yesu kuingia ndani ya mbingu wakawe sehemu ya mpango huo mtukufu! (Yohana 14:2) Yohana hutoa wazo moja la baraka zitakazofurahiwa na hawa, akisema: “Na hakutakuwa tena na laana yoyote. Bali kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo vitakuwa ndani ya jiji, na watumwa wake watatolea yeye utumishi mtakatifu; na wao wataona uso wake, na jina lake litakuwa juu ya vipaji vya nyuso zao.” (Ufunuo 22:3, 4, NW) Wakati ukuhani wa Kiisraeli ulipopata kuwa mfisadi, ulipatwa na laana ya Yehova. (Malaki 2:2) “Nyumba” isiyo na imani ya Yerusalemu ilitamkwa na Yesu imeachwa. (Mathayo 23:37-39) Lakini katika Yerusalemu Jipya, “hakutakuwa tena na laana yoyote.” (Linga Zekaria 14:11.) Wakaaji walo wote wamekwisha tahiniwa katika moto wa majaribu hapa duniani, na wakiwa wamekwisha pata ushindi, watakuwa ‘wamekwisha vaa kutofisidika na kutokufa.’ Kwa habari yao, Yehova anajua, kama vile alivyojua kwa habari ya Yesu, kwamba hawataangukia mbali kamwe. (1 Wakorintho 15:53, 57) Na zaidi, “kiti cha ufalme na cha Mwana-Kondoo” kitakuwa huko, kufanya jiji hilo kuwa salama kwa umilele wote.
28. Ni kwa nini washiriki wa Yerusalemu Jipya wana jina la Mungu limeandikwa juu ya kipaji cha uso wao, na ni taraja gani lenye kusisimua lililo mbele yao?
28 Kama Yohana mwenyewe, washiriki wote wa wakati ujao wa hilo jiji la kimbingu ni “watumwa” wa Mungu. Wakiwa hivyo, wana jina la Mungu likiwa limeandikwa kwa kuonekana wazi juu ya kipaji cha uso wao, kumtambulisha yeye kuwa Mwenye wao. (Ufunuo 1:1; 3:12) Wao watalihesabu kuwa pendeleo lisilokadirika kumtolea utumishi mtakatifu wakiwa sehemu ya Yerusalemu Jipya. Yesu alipokuwa duniani, aliwapa ahadi yenye kusisimua hao waliotazamiwa kuwa watawala, akisema: “Wenye furaha ni wale walio safi katika moyo, kwa kuwa wao wataona Mungu.” (Mathayo 5:8, NW) Jinsi hawa watumwa watakuwa wenye furaha kumwona na kumwabudu Yehova kihalisi na kinaganaga!
29. Ni kwa nini Yohana husema juu ya Yerusalemu Jipya kwamba “usiku utakuwa hauko tena”?
29 Yohana aendelea: “Pia, usiku utakuwa hauko tena, na wao hawana uhitaji wa nuru ya taa wala wao hawana nuru ya jua, kwa sababu Yehova Mungu atatoa nuru juu yao.” (Ufunuo 22:5a, NW) Yerusalemu la kale, kama jiji jingine lolote duniani, lilitegemea jua kuwa nuru wakati wa mchana na nuru ya mwezi na nuru ya kubuniwa wakati wa usiku. Lakini katika Yerusalemu Jipya la kimbingu kutoa nuru kama huko kutakuwa si kwa lazima kabisa. Jiji hilo litamulikwa na Yehova mwenyewe. “Usiku” huenda ukatumiwa pia katika maana ya kitamathali, kurejezea janga au mtenganisho na Yehova. (Mika 3:6; Yohana 9:4; Warumi 13:11, 12) Hakungeweza kuwa na usiku wa aina hiyo katika kuwapo kwenye utukufu na kwenye kung’aa kwa Mungu mweza yote.
30. Yohana anamaliziaje njozi nzuri mno, na Ufunuo unatuhakikishia nini?
30 Yohana anafunga njozi hii nzuri mno kwa kusema kwa habari ya hawa watumwa wa Mungu: “Na wao watatawala wakiwa wafalme milele na milele.” (Ufunuo 22:5b, NW) Ni kweli, mwishoni mwa miaka elfu, manufaa za ukombozi zitakuwa zimekwisha tumiwa kwa utimilifu, na Yesu atamtolea Baba yake jamii ya kibinadamu iliyokamilishwa. (1 Wakorintho 15:25-28) Analofikiria Yehova kwa ajili ya Yesu na 144,000 baada ya hapo, sisi hatujui. Lakini Ufunuo unatuhakikishia kwamba utumishi mtakatifu wao uliopendelewa kwa Yehova utaendelea kwa umilele wote.
Upeo Wenye Furaha wa Ufunuo
31. (a) Ni upeo gani unaotiwa alama na njozi ya Yerusalemu Jipya? (b) Yerusalemu Jipya hutimiza nini kwa ajili ya waaminifu wengine wa aina ya binadamu?
31 Utimizo wa njozi hii ya Yerusalemu Jipya, mke wa Mwana-Kondoo, ndio upeo wenye furaha ambao kwao Ufunuo unaelekeza, na kwa kufaa hivyo. Wakristo wenzi wa Yohana wa karne ya kwanza ambao kwanza ndio waliopelekewa kitabu walitazamia kuingia ndani ya jiji hilo wakiwa roho watawala wenzi pamoja na Yesu Kristo. Baki la Wakristo wapakwa-mafuta ambao wangali hai leo duniani wana tumaini ilo hilo. Hivyo Ufunuo unasonga mbele kuelekea upeo wao mtukufu, wakati bibi-arusi aliyekamilika anapoungana na Mwana-Kondoo. Kisha, kwa njia ya Yerusalemu Jipya, manufaa za dhabihu ya ukombozi ya Yesu zitatumiwa juu ya aina ya binadamu, hivi kwamba hatimaye waaminifu wote wataingia ndani ya uhai wa milele. Katika njia hiyo bibi-arusi, Yerusalemu Jipya, akiwa msaidizi-mwenzi mshikamanifu wa Bwana-arusi Mfalme wake, atashiriki katika kujenga kwa umilele dunia mpya yenye uadilifu—yote hayo kwa utukufu wa Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu wetu.—Mathayo 20:28; Yohana 10:10, 16; Warumi 16:27.
32, 33. Tumejifunza nini kutokana na Ufunuo, na itikio letu la kutoka moyoni limepaswa kuwa nini?
32 Basi, tunahisi shangwe kama nini tunapokaribia kufunga mazungumzo yetu juu ya kitabu cha Ufunuo! Tumeona jitihada za mwisho za Shetani na mbegu yake zikibatilishwa kabisa na hukumu zenye uadilifu za Yehova zikifikilizwa mpaka utimilifu. Babuloni Mkubwa lazima aondoke asiweko milele, akifuatwa na elementi fisadi mno nyingine zote za ulimwengu wa Shetani. Shetani mwenyewe na roho waovu wake watatiwa ndani ya abiso na baadaye kuharibiwa. Yerusalemu Jipya litatawala pamoja na Kristo kutoka katika mbingu huku ufufuo na hukumu zikiwa zinaendelea, na mwishowe aina ya binadamu iliyokamilishwa itakuja kufurahia uhai wa milele katika dunia Paradiso. Jinsi Ufunuo unavyotaswiri kwa wazi sana vitu hivi vyote! Jinsi inavyoimarisha azimio letu la ‘kujulisha wazi hizi habari njema za milele kuwa taarifa teremeshi kwa kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu’ walio duniani leo! (Ufunuo 14:6, 7, NW) Je! wewe unajitumikisha mwenyewe kwa ukamili katika kazi hii kubwa?
33 Mioyo yetu ikiwa inajaa asante hivyo, acheni sisi tuangalie maneno ya kumalizia ya Ufunuo.
[Maelezo ya Chini]
a Uhakika wa kwamba kipimo kilichotumiwa kilikuwa “kulingana na kipimo cha binadamu, wakati uo huo cha malaika” huenda ukahusiana na uhakika wa kwamba jiji hilo linafanyizwa kwa 144,000, ambao awali walikuwa binadamu lakini ambao huwa viumbe vya roho miongoni mwa malaika.
b Angalia kwamba “hati-kunjo ya uhai ya Mwana-Kondoo” ina majina ya 144,000 tu wa Israeli wa kiroho. Hivyo inatofautiana na “hati-kunjo ya uhai” ambayo inatia ndani wale ambao wanapokea uhai wa milele duniani.—Ufunuo 20:12, NW.
-