-
Ufalme “Ambao Hautaangamizwa Milele”Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
Malengo ya Ufalme Yatatimizwaje?
11. (a) Ufalme wa Kimesiya utatimizaje kusudi la Yehova kwa dunia? (b) Ufalme huo utawafaidije wakazi wa dunia?
11 Ufalme wa Kimesiya utatimiza kabisa kusudi la Mungu la awali kwa dunia. (Mwanzo 1:28; 2:8, 9, 15) Kufikia sasa, wanadamu wameshindwa kutimiza kusudi hilo. Hata hivyo, ‘dunia ijayo itakayokaliwa’ itatawaliwa na Mwana wa binadamu, Yesu Kristo. Wote watakaookoka hukumu ya Yehova dhidi ya ulimwengu huu wa kale watafanya kazi kwa umoja chini ya Kristo akiwa Mfalme. Watafurahia kutii maagizo yake na kuifanya dunia yote iwe paradiso. (Waebrania 2:5-9) Wanadamu wote watafurahia kazi ya mikono yao, watafurahia chakula tele kitakachokuwapo duniani.—Zaburi 72:1, 7, 8, 16-19; Isaya 65:21, 22.
12. Raia wa Ufalme watafanywaje wawe wakamilifu kiakili na kimwili?
12 Adamu na Hawa waliumbwa wakiwa wakamilifu, na Mungu alikusudia wazao wao wajaze dunia, wote wakiwa wakamilifu kiakili na kimwili. Kusudi hilo litatimizwa kwa utukufu hivi karibuni Ufalme utakapotawala. Ili kusudi hilo litimie ni lazima Kristo ambaye ni Mfalme na Kuhani Mkuu aondoe athari zote za dhambi. Kwa subira, atawasaidia raia wake watiifu wafaidike na dhabihu aliyotoa ili kulipia dhambi, yaani, uhai wake wa kibinadamu.
13. Ni baraka gani zitakazoletwa na utawala wa Ufalme?
13 Ufalme utawaletea wakazi wa dunia baraka nyingi sana. “Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba.” (Isaya 35:5, 6) Mwili ambao umeumbuliwa na uzee au magonjwa utakuwa laini kuliko mwili wa mtoto, magonjwa sugu yatatoweka na watu watakuwa na afya bora kabisa. “Nyama ya mwili wake itakuwa laini kuliko ya mtoto; huzirudia siku za ujana wake.” (Ayubu 33:25) Siku itafika ambapo hakuna mtu atakuwa na sababu ya kusema, “Mimi mgonjwa.” Kwa nini? Kwa sababu wanadamu wanaomcha Mungu wataondolewa dhambi yenye kulemea na matokeo yake yenye kuhuzunisha. (Isaya 33:24; Luka 13:11-13) Naam, Mungu “atafuta kabisa kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:4.
14. Kuwa mkamilifu kwahusisha nini?
14 Hata hivyo, kuwa mkamilifu hakumaanishi kuwa tu na afya nzuri ya kimwili na ya kiakili. Kwahusisha pia kuiga sifa za Yehova kikamili, kwa sababu tuliumbwa ‘kwa mfano na sura ya Mungu.’ (Mwanzo 1:26) Tutahitaji kuelimishwa sana ili tufaulu kufanya hivyo. “Uadilifu utakaa” katika ulimwengu huo mpya. Kwa hiyo ‘watu wakaao duniani watajifunza haki,’ kama Isaya alivyotabiri. (2 Petro 3:13; Isaya 26:9) Sifa hiyo huleta amani—kati ya watu wa makabila yote, kati ya marafiki, katika familia, na zaidi ya yote, kati yetu na Mungu. (Zaburi 85:10-13; Isaya 32:17) Wale wanaojifunza uadilifu watafundishwa mapenzi ya Mungu hatua kwa hatua. Upendo wa Yehova unapoingia moyoni mwao, watafuata njia zake maishani mwao. Wataweza kusema kama Yesu alivyosema, ‘Sikuzote mimi hufanya mambo yale yanayompendeza Baba yangu.’ (Yohana 8:29) Maisha yatafurahisha sana wanadamu wote watakapofanya hivyo.
-
-
Ufalme “Ambao Hautaangamizwa Milele”Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
Ufalme wa Miaka Elfu
16. (a) Kristo atatawala kwa muda gani? (b) Ni mambo gani mazuri yatakayotimizwa wakati huo na baadaye?
16 Baada ya Shetani na mashetani wake kufungwa, Yesu Kristo na warithi wenzake 144,000 watatawala wakiwa wafalme na makuhani kwa miaka elfu. (Ufunuo 20:6) Katika kipindi hicho, wanadamu watasaidiwa kufikia ukamilifu, na dhambi na kifo kilichosababishwa na Adamu vitakomeshwa milele. Mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu, baada ya kutimiza kikamili kazi yake akiwa Mfalme-Kuhani wa Kimesiya, Yesu ‘atamkabidhi Baba yake ufalme, ili Mungu apate kuwa vitu vyote kwa kila mtu.’ (1 Wakorintho 15:24-28) Wakati huo, Shetani atafunguliwa kwa muda mfupi ili awajaribu wanadamu waliokombolewa ili ijulikane kama wanaunga mkono enzi kuu ya Yehova au la. Baada ya jaribu hilo la mwisho, Yehova atamharibu Shetani na waasi waliomuunga mkono. (Ufunuo 20:7-10) Wale waliounga mkono enzi kuu ya Yehova—haki yake ya kutawala—watakuwa wamethibitisha kwamba wao ni waaminifu kabisa kwa Mungu. Kisha watakuwa na uhusiano unaofaa na Yehova, wakiwa wana na binti zake, na atawapa kibali cha kuishi milele.—Waroma 8:21.
-