Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
    • Timotheo​—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia

      “JE, UKO tayari?” Je, umewahi kuulizwa swali hilo?— Mtu aliyekuuliza swali hilo alitaka kujua ikiwa ulikuwa umejitayarisha. Kwa mfano, huenda mtu huyo alikuwa akiuliza hivi: ‘Je, vitabu vyako viko tayari? Umepitia masomo yako?’ Kama tutakavyoona, Timotheo alikuwa tayari.

      Timotheo alikuwa mwenye nia pia. Unajua hilo linamaanisha nini?— Timotheo alipoombwa amtumikie Mungu, alikuwa na mtazamo kama wa mtumishi mwingine wa Mungu, ambaye alisema: “Mimi hapa! Nitume mimi.” (Isaya 6:8) Kwa kuwa alikuwa tayari na mwenye nia ya kutumikia, Timotheo aliishi maisha yenye kusisimua.

  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
    • Timotheo alifurahi hata zaidi alipoombwa aandamane na Paulo na Sila. Timotheo alikubali. Alikuwa tayari na mwenye nia ya kuandamana nao.—Matendo 15:40–16:5.

  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
    • Paulo aliwahangaikia waamini wapya wa Thesalonike, hivyo akamtuma Timotheo arudi huko. Unajua ni kwa nini?— Baadaye Paulo aliwaeleza hivi Wakristo waliokuwa Thesalonike: ‘Kusudi awaimarishe ninyi na kuwafariji ili yeyote asivunjike moyo.’ Unajua kwa nini Paulo alimpa Timotheo mgawo huo hatari?— Ni kwa sababu wapinzani hawakumjua vizuri Timotheo, na pia kwa sababu alikuwa mwenye nia ya kwenda. Alihitaji kuwa na ujasiri mwingi!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki