-
Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa TimotheoMnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
Miaka kumi hivi baadaye, Paulo yuko Makedonia na Timotheo yuko Efeso. Paulo anamwandikia Timotheo na kumtia moyo abaki Efeso ili aendelee kuwasaidia ndugu na dada wadumishe uhusiano wao mzuri pamoja na Yehova ingawa kuna uvutano wa walimu wa uwongo ndani ya kutaniko.
-
-
Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa TimotheoMnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
“LINDA LILILOWEKWA AMANA KWAKO”
Paulo anamwagiza Timotheo ‘aendelee kupigana vita vizuri; akishika imani na dhamiri njema.’ Mtume huyo anataja sifa za kustahili kwa wanaume ambao wanawekwa rasmi katika kutaniko. Pia, Paulo anamwagiza Timotheo ‘kukataa hadithi za uwongo ambazo huchafua mambo matakatifu.’—1 Tim. 1:18, 19; 3:1-10, 12, 13; 4:7.
Paulo anaandika hivi: “Usimkemee kwa ukali mwanamume mzee.” Anamhimiza Timotheo: “Linda lililowekwa amana kwako, ukigeuka mbali kutoka kwenye maneno matupu ambayo huchafua mambo matakatifu na kutoka kwenye maneno yanayopingana ya ule unaoitwa kwa uwongo ‘ujuzi.’”—1 Tim. 5:1; 6:20.
Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:
1:18; 4:14—Ni “matabiri” gani yaliyotolewa kumhusu Timotheo? Huenda ulikuwa unabii mbalimbali kuhusu madaraka ya wakati ujao ya Timotheo katika kutaniko la Kikristo, ambao ulitolewa chini ya mwongozo wa roho ya Mungu Paulo alipotembelea Listra wakati wa safari yake ya pili ya umishonari. (Mdo. 16:1, 2) Wakitegemea “matabiri” hayo, wanaume wazee wa kutaniko hilo ‘waliweka mikono yao’ juu ya kijana Timotheo, wakamweka kando kwa ajili ya utumishi wa pekee.
2:15—Ni kwa njia gani mwanamke ‘anabaki salama kupitia kuzaa watoto’? Kuzaa watoto, kuwalea watoto wake, na kutunza nyumba kunamfanya mwanamke awe “salama” kwa kutokosa jambo la kufanya na hivyo kuwa ‘mwenye kupiga porojo na mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.’—1 Tim. 5:11-15.
3:16—Siri takatifu ya ujitoaji-kimungu ni nini? Kwa miaka mingi, haikujulikana ikiwa wanadamu wanaweza kutii kwa ukamilifu au kutotii enzi kuu ya Yehova. Yesu alijibu swali hilo kwa kudumisha utimilifu mkamilifu kwa Mungu mpaka kufikia kifo chake.
6:15, 16—Je, maneno haya yanamhusu Yehova Mungu au Yesu Kristo? Maneno hayo yanahusu yule ambaye ufunuo wake unazungumziwa, yaani, Yesu Kristo. (1 Tim. 6:14) Akilinganishwa na wanadamu wanaotawala wakiwa wafalme na mabwana, Yesu ndiye “Mwenye Uwezo Mkubwa aliye wa pekee,” na ni yeye peke yake aliye na kutoweza kufa. (Dan. 7:14; Rom. 6:9) Tangu alipopanda katika mbingu zisizoonekana, hakuna mwanadamu duniani ‘anayeweza kumwona’ kwa macho halisi.
Mambo Tunayojifunza:
4:15. Hata ikiwa tumeamini na kuwa Wakristo hivi karibuni au kwa miaka mingi, tunapaswa kujitahidi kuendelea kufanya maendeleo ya kiroho na kuimarisha uhusiano wetu pamoja na Yehova.
6:2. Ikiwa tunamfanyia kazi mwamini mwenzetu, badala ya sisi kujipatia faida kutokana na kazi hiyo, tunapaswa kujitahidi kumfanyia kazi kwa utayari zaidi hata kuliko vile tungemfanyia mtu asiye mwamini.
-