Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Tito, kwa Filemoni, na kwa Waebrania
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 15
    • MTUME Paulo anatembelea kisiwa cha Krete muda mfupi baada ya kuachiliwa huru kutoka gerezani huko Roma mwaka wa 61 W.K., baada ya kumaliza kifungo chake cha kwanza. Anapoona hali ya kiroho ya makutaniko katika kisiwa hicho, anamwacha Tito huko ili ayatie nguvu. Baadaye, inaelekea akiwa Makedonia, Paulo anamwandikia Tito barua ya kumwongoza katika madaraka yake na ambayo inaonyesha kwamba mtume Paulo alimpa mamlaka ya kutimiza madaraka hayo.

  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Tito, kwa Filemoni, na kwa Waebrania
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 15
    • ENDELEA KUWA NA AFYA NZURI YA KIROHO

      (Tito 1:1–3:15)

      Baada ya kutoa mwongozo kuhusu ‘kuwekwa rasmi kwa wanaume wazee katika jiji baada ya jiji,’ Paulo anamshauri Tito ‘aendelee kuwakaripia kwa ukali [watu watundu], ili wawe na afya katika imani.’ Anayashauri makutaniko yote huko Krete ‘yakatae kabisa kutomwogopa Mungu na yaishi kwa utimamu wa akili.’—Tito 1:5, 10-13; 2:12.

      Paulo anatoa mashauri zaidi ya kuwasaidia ndugu wa Krete waendelee kuwa na afya nzuri ya kiroho. Anamwagiza Tito ‘aepuke maswali ya upumbavu na mapigano juu ya Sheria.’—Tito 3:9.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      1:15—“Vitu vyote” vinaweza jinsi gani kuwa “safi kwa watu safi” na visivyo safi “kwa watu waliotiwa unajisi na wasio na imani”? Ili kupata jibu ni lazima tuelewe Paulo alimaanisha nini aliposema “vitu vyote.” Hakuwa akizungumza kuhusu vitu ambavyo vinashutumiwa moja kwa moja katika Neno la Mungu lililoandikwa, bali alikuwa akizungumza kuhusu mambo ambayo Maandiko yanawaruhusu watu wajifanyie maamuzi ya kibinafsi. Mtu ambaye anafikiri kupatana na viwango vya Mungu, anaona vitu hivyo kuwa safi. Yeye ni tofauti na mtu ambaye fikira zake zimepotoka na dhamiri yake imetiwa unajisi.a

      3:5—Wakristo watiwa-mafuta ‘wanaokolewa jinsi gani kupitia kuoshwa’ na ‘kufanywa kuwa wapya kwa roho takatifu’? ‘Wanaokolewa kupitia kuoshwa’ katika maana ya kwamba Mungu amewaosha, au amewatakasa, kwa damu ya Yesu kwa msingi wa dhabihu ya fidia. ‘Wanafanywa kuwa wapya kwa roho takatifu’ kwa sababu wamekuwa “kiumbe kipya” wakiwa wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho.—2 Kor. 5:17.

      Mambo Tunayojifunza:

      1:10-13; 2:15. Ni lazima waangalizi Wakristo wawe jasiri wanaporekebisha makosa katika kutaniko.

      2:3-5. Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, dada Wakristo wakomavu leo wanahitaji ‘kuwa wenye tabia ya kumhofu Mungu, si wachongezi, wala si watumwa wa divai nyingi sana, wawe walimu wa yaliyo mema.’ Wakifanya hivyo, watafaulu kuwafundisha faraghani “wanawake vijana” katika kutaniko.

      3:8, 14. Kukaza ‘akili zetu juu ya kudumisha matendo yaliyo mazuri’ ni ‘jambo zuri na lenye faida’ kwa sababu linatusaidia kuzaa matunda katika utumishi wa Mungu na kujitenga na ulimwengu mwovu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki