Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mwaka huo, Ropati Uili, aliyekuwa daktari, alirudi Tokelau baada ya kufuzu kutoka katika shule ya kitiba nchini Fiji. Emmau, mke wa Ropati, alikuwa Shahidi aliyebatizwa, naye Ropati alikuwa amejifunza na Mashahidi wa Yehova kwa muda mfupi akiwa Fiji.f

      Akiwa Tokelau, Ropati aligundua kwamba daktari mwingine pamoja na mke wake, Iona na Luisa Tinielu, walikuwa Mashahidi waliobatizwa. Pia alikutana na mtu mwingine anayependezwa, Nanumea Foua, ambaye watu wake wa ukoo walikuwa Mashahidi wa Yehova. Wanaume hao watatu walipanga kufanya kwa ukawaida mikutano ya Biblia na hotuba za watu wote na muda si muda hudhurio likafikia 25. Pamoja na familia zao walianza kuwahuburia wengine kwa njia zisizo rasmi.

      Hata hivyo, si kila mtu aliyependezwa na utendaji huo wa kitheokrasi. Kufuatia uchochezi wa padri wa London Missionary Society, baraza la wazee wa kijiji liliwaita wanaume hao watatu. “Walituamuru tuache kufanya mikutano yetu,” akumbuka Ropati, “na kusema kwamba tusipoacha, watatuteketeza tukiwa hai katika nyumba zetu au kutuingiza katika mtumbwi na kutufukuza twende zetu. Tulijaribu kujadiliana nao kwa kutumia Maandiko, lakini hawakutaka kusikia lolote. Walitazamia tutii mamlaka yao hata iweje.” Baada ya kusikia uamuzi wao wa mwisho, familia hizo ziliamua kufanya mikutano yao kisiri ili kuepuka matatizo.

      Hata hivyo, upinzani huo ulikuwa mwanzo tu. Miaka 12 baadaye, wakati ambapo dadake Ropati na mume wake walipoikubali kweli na kujiuzulu kutoka katika kanisa lao, wazee wa kijiji waliwafukuza Mashahidi wote kijijini humo. “Usiku huo,” aandika Ropati, “kila familia ilifunga virago vyake na kuvipakia kwenye mashua ndogo, na kutafuta makimbilio katika kijiji kikubwa zaidi kisiwani humo. Nyumba zao na mashamba yao yaliporwa na jirani zao.”

      Licha ya minyanyaso hiyo, wahubiri hao waliendelea kukutanika pamoja ili kuabudu. “Wakijifanya kana kwamba walikuwa wakienda matembezi mwishoni mwa juma,” Ropati aeleza, “Jumamosi asubuhi familia hizo zilikuwa zikisafiri kwa mtumbwi kwenda katika kisiwa kidogo kisicho na watu wengi na kurudi Jumapili jioni baada ya kufanya mikutano yao.” Wakati huo, familia kadhaa pia zilifunga safari ndefu kwa mashua kutoka Tokelau hadi Samoa kuhudhuria makusanyiko ya wilaya ya kila mwaka.

      Hatimaye, kwa sababu ya upinzani huo usiokoma, familia hizo ziliamua kuhamia New Zealand.

  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • f Ropati alibatizwa baadaye alipozuru New Zealand.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki