Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uwezo wa Kusema kwa Lugha Je, Unatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 1
    • Uwezo wa Kusema kwa Lugha Je, Unatoka kwa Mungu?

      “SIELEWI,” anasema Devon. “Kila juma, watu wengi katika kanisa langu huonekana kupokea roho takatifu na kusema kwa lugha mbalimbali kimuujiza. Baadhi yao wanaishi maisha mapotovu. Mimi hujitahidi kuishi kupatana na kanuni za Biblia. Lakini hata nisali kwa bidii kadiri gani, mimi sipati zawadi hiyo ya roho. Kwa nini iwe hivyo?”

      Gabriel naye ni mshiriki wa kanisa ambalo waumini wake huonekana kupokea roho takatifu na kusema kwa lugha mbalimbali. Yeye anasema, “Jambo linalonisumbua ni moja. Wakati ninaposali, watu wengine hunikatiza kwa sala wanazotoa kwa sauti kubwa wakitumia maneno ambayo siyaelewi wala wao wenyewe hawayaelewi. Hakuna mtu ambaye hufaidika na sala hizo. Lakini ikiwa zawadi inatokana na roho ya Mungu, si inapaswa kuwa na manufaa?”

      Mambo ambayo Devon na Gabriel wamejionea yanatokeza swali lenye kuamsha fikira, Je, ni kweli kwamba uwezo wa kusema kwa lugha, kama ilivyo katika makanisa fulani leo, unatoka kwa Mungu? Ili kujibu swali hilo, inafaa kuchunguza jinsi zawadi ya kimuujiza ya kuzungumza kwa lugha ilivyotumiwa kati ya Wakristo wa karne ya kwanza.

  • Uwezo wa Kusema kwa Lugha Je, Unatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 1
    • Kusema kwa Lugha Leo, Je, Ni Ishara ya Kuungwa Mkono na Mungu?

      Ungeweka ishara wapi ili kuwasaidia watu wengi iwezekanavyo katika eneo lako? Ndani ya jengo dogo? Hapana! Simulizi kuhusu siku ya Pentekoste linasema kuwa “umati” wa wapita-njia waliona ishara wakati wanafunzi walipozungumza kwa lugha mbalimbali kimuujiza. Kwa sababu hiyo, “nafsi karibu elfu tatu zikaongezwa” katika kutaniko la Kikristo siku hiyo! (Matendo 2:5, 6, 41) Ikiwa leo watu wanaodai kusema kwa lugha wanafanya hivyo tu ndani ya kanisa, jambo hilo linaweza jinsi gani kuwa ishara inayoonekana waziwazi na umati wa wasioamini?

      Neno la Mungu linataja uasherati na “matendo [mengine] ya mwili” kuwa yanapingana na utendaji wa roho takatifu, na kuongeza kwamba “wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Wagalatia 5:17-21) Iwapo unawaona watu wenye mwenendo mpotovu wakisema kwa lugha, huenda kwa kufaa ukauliza, ‘Je, hilo si jambo lisilowezekana—hata lenye kupotosha—kwa Mungu kuwapa roho takatifu watu walio na mazoea ya kufanya mambo ambayo yanashutumiwa na Neno lake?’ Hilo ni kama kuweka ishara ya barabarani inayopotosha watu.

      Je, Kusema kwa Lugha Leo Kunatumiwa Kueneza Habari Njema?

      Namna gani kuhusu lile kusudi lingine la zawadi ya kusema kwa lugha katika karne ya kwanza? Je, kusema kwa lugha katika makanisa leo kunachangia kuenezwa kwa habari njema kwa watu wa lugha mbalimbali? Kumbuka kwamba watazamaji waliokuwa Yerusalemu siku ya Pentekoste 33W.K., walitoka katika nchi nyingi, na walielewa vizuri lugha zilizozungumzwa kimuujiza na wanafunzi. Tofauti na hilo wale wanaosema kwa lugha leo, kwa kawaida husema mambo yasiyoweza kueleweka na yeyote.

      Bila shaka, wale wanaosema kwa lugha leo wanafanya hivyo kwa njia tofauti kabisa na jinsi wafuasi wa mapema wa Yesu waliopewa zawadi ya roho takatifu walivyofanya. Hata hakuna uthibitisho wenye kutegemeka kwamba kuna yeyote aliyepokea nguvu hizo za kimuujiza baada ya mitume kufa. Jambo hilo haliwashangazi wasomaji wa Biblia. Kuhusu zawadi za kimuujiza, kutia ndani kusema kwa lugha, mtume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu kutabiri hivi: “Zitakoma.” (1 Wakorintho 13:8)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki