-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mapema kama 1881, fasihi za Wanafunzi wa Biblia zilikuwa zikitolewa kwa watu bila malipo karibu na makanisa—si kwenye milango ya kanisa kabisa bali karibu na hapo ili watu waliokuwa na mwelekeo wa kidini waweze kuzipokea. Wengi wa Wanafunzi wa Biblia waliwapa fasihi hizo watu waliowajua au wakazipeleka kwa posta. Kufikia 1903 Watch Tower likapendekeza kwamba wajitahidi kufikia kila mtu kwa kugawanya trakti nyumba hadi nyumba, badala ya kukazia juu ya wahudhuriaji wa kanisa. Si Wanafunzi wa Biblia wote waliofanya hivyo, lakini wengi waliitikia kwa bidii halisi. Kwa kielelezo iliripotiwa kwamba, katika hesabu fulani ya majiji makubwa katika Marekani, kutia na viunga vyayo kwenda kilometa 16 au zaidi katika kila upande, karibu kila nyumba ilitembelewa. Mamilioni na mamilioni ya trakti, au vijitabu, viligawanywa kwa njia hiyo. Wakati huo Wanafunzi wa Biblia wengi walioshiriki katika kueneza habari njema walifanya hivyo kwa njia mbalimbali ili kugawanya trakti na fasihi nyinginezo.
Wanafunzi wa Biblia wengineo—wachache sana—walitumikia wakiwa makolpota waeneza-evanjeli, wakitumia sehemu kubwa ya wakati wao kihususa kwa kazi hiyo.
-
-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 557]
Makumi ya mamilioni ya trakti hizi yaligawanywa bure, karibu na makanisa, nyumba hadi nyumba, na kwa posta
-