Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Nyota Yaanguka Kutoka Mbinguni

      28. Kunakuwa nini wakati malaika wa tatu anapopuliza tarumbeta yake?

      28 “Na malaika wa tatu akapuliza tarumbeta yake. Na nyota kubwa yenye kuwaka kama taa ikaanguka kutoka mbinguni, na ikaanguka juu ya theluthi moja ya mito na juu ya vibubujiko vya maji. Na jina la nyota linaitwa Pakanga. Na theluthi ya maji ikageuka kuwa pakanga, na wengi wa wanadamu wakafa kwa hayo maji, kwa sababu haya yalikuwa yamefanywa kuwa machungu.” (Ufunuo 8:10, 11, NW) Hapa tena, sehemu nyingine za Biblia hutusaidia kujua jinsi andiko hili linavyotumika katika siku ya Bwana.

      29. Ni nini kinachotimiza mfananisho wa “nyota kubwa yenye kuwaka kama taa,” na kwa nini?

      29 Sisi tumekwisha kutana na mfananisho wa nyota katika jumbe za Yesu kwa yale makundi saba, ambazo katika hizo zile nyota saba hufananisha wale wazee katika makundi.b (Ufunuo 1:20) “Nyota” zilizopakwa mafuta, pamoja na wengine wote wa wapakwa-mafuta, wanakaa katika mahali pa kimbingu katika maana ya kiroho kutoka wakati ambao wao wanatiwa muhuri kwa roho takatifu hiyo ikiwa dalili ya urithi wao wa kimbingu. (Waefeso 2:6, 7) Hata hivyo, mtume Paulo alionya kwamba kutoka miongoni mwa hao wenye mfano wa nyota wangekuja waasi-imani, wanafaraka, ambao wangeongoza kundi vibaya. (Matendo 20:29, 30) Utoaminifu kama huo ungetokeza uasi-imani mkubwa, na hao wazee walioanguka wangekuja kuwa jumuiya ya “mtu wa kuasi” ambaye angejiinua mwenyewe kwenye cheo kama cha Mungu miongoni mwa aina ya binadamu. (2 Wathesalonike 2:3, 4) Maonyo ya Paulo yalitimizwa wakati viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipotokea katika ulimwengu. Kikundi hiki kinawakilishwa vizuri na ule ufananisho wa “nyota moja kubwa ikiwaka kama taa.”

      30. (a) Wakati mfalme wa Babuloni alipoambiwa ameanguka kutoka mbinguni, ni nini kilichomaanishwa? (b) Anguko kutoka mbinguni laweza kurejezea nini?

      30 Yohana anaona nyota hii hususa ikianguka kutoka mbinguni. Jinsi gani? Yaliyompata mfalme mmoja wa kale hutusaidia sisi kuelewa. Akisema kwa mfalme wa Babuloni, nabii Isaya alisema: “O jinsi wewe umeanguka kutoka mbinguni, wewe mwenye kung’aa, mwana wa mapambazuko! Jinsi wewe umekatwa chini kwenye dunia, wewe ambaye ulikuwa ukiondoa uwezo wa mataifa!” (Isaya 14:12, NW) Unabii huu ulitimizwa wakati Babuloni ilipoangushwa na majeshi ya Sairasi, naye mfalme wayo akashuka ghafula kutoka utawala wa ulimwengu mpaka kwenye ushinde wenye kuaibisha. Hivyo, anguko kutoka mbinguni laweza kurejezea kupoteza cheo cha juu na kuanguka kwenye aibu.

      31. (a) Ni lini viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoanguka kutoka cheo cha “kimbingu”? (b) Maji ambayo viongozi wa kidini wanatoa yamegeukaje yakawa “pakanga,” na kukiwa na tokeo gani kwa wengi?

      31 Wakati viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoasi Ukristo wa kweli, wao walianguka kutoka cheo kilichotukuka cha “kimbingu” kinachoelezwa na Paulo kwenye Waefeso 2:6, 7, NW. Badala ya kutoa maji safi ya ukweli, wao walitoa “pakanga,” uwongo mchungu kama vile moto wa mateso, pargatori, Utatu, na watu kuandikiwa kimbele mwisho wao; pia waliongoza mataifa kwenye vita, wakishindwa kuwajenga wawe watumishi waadilifu wa Mungu. Tokeo? Kusumishwa kiroho kwa wale walioitikadi uwongo huo. Kisa chao kilifanana na kile cha Waisraeli wasio waaminifu wa siku ya Yeremia, ambao kwao Yehova alisema: “Hapa mimi ninafanya wao kula pakanga, na mimi nitawapa maji yaliyosumishwa wanywe. Kwa kuwa kutoka manabii wa Yerusalemu uasi-imani umetoka na kwenda kwenye bara lote.”—Yeremia 9:15; 23:15, NW.

      32. Ni lini anguko la Jumuiya ya Wakristo kutoka mbingu za kiroho lilipopata kuwa wazi, nalo lilionyeshwaje kama drama?

      32 Anguko hili kutoka mbingu za kiroho lilionekana wazi katika mwaka 1919 wakati, badala ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, baki dogo la Wakristo wapakwa-mafuta waliwekwa rasmi juu ya masilahi ya Ufalme. (Mathayo 24:45-47) Na katika 1922 anguko hilo lilionyeshwa kama drama wakati kikundi hiki cha Wakristo kilipoanza upya kampeni yacho ya kufichua wazi kushindwa kwa viongozi wa Jumuiya ya Wakristo.

      33. Ni mfichuo gani wa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo uliofanywa kwenye mkusanyiko wa 1924 katika Kolumbasi, Ohaiyo, U.S.A.?

      33 Yenye kutokeza kuhusiana na hili ni ile mbiu iliyopigwa kwenye ule ambao gazeti The Golden Age liliueleza kuwa “mkusanyiko ulio mkubwa zaidi ya yote wa Wanafunzi wa Biblia uliofanywa wakati wa enzi zilizopita.” Mkusanyiko huu ulikusanyika katika Kolumbasi, Ohaiyo, Julai 20-27, 1924. Pasipo shaka kwa mwelekezo wa malaika ambaye alivumisha ile tarumbeta ya tatu, azimio lenye kujaa kani lilikubaliwa huko na baadaye nakala milioni 50 zikagawanywa zikiwa trakti. Lilitangazwa chini ya kichwa Viongozi wa Kidini Washtakiwa. Kichwa kidogo kilitoa suala hili: “Mbegu ya Ahadi Dhidi ya Mbegu ya Nyoka.” Shtaka lenyewe lilifichua waziwazi viongozi wa kidini juu ya mambo kama vile kujitwalia kwao wenyewe majina ya cheo ya kujiweka juu sana, kufanya kwao wanabiashara wakubwa-wakubwa na wanasiasa wa kulipwa kuwa ndio wakuu wa makundi yao, kutamani kwao kung’aa mbele ya watu, na kukataa kwao kuhubiria watu ujumbe wa Ufalme wa Mesiya. Lilikazia kwamba kila Mkristo aliye wakfu amepewa utume na Mungu atangaze “siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao.”—Isaya 61:2.

      34, 35. (a) Nguvu na uvutano wa viongozi wa kidini vimekuwaje tangu malaika wa tatu aanze kupuliza tarumbeta yake? (b) Wakati ujao una nini kwa ajili ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo?

      34 Tangu malaika wa tatu aanze kupuliza tarumbeta yake, cheo cha viongozi wa kidini cha utawala miongoni mwa aina ya binadamu kimekuwa kikichurupuka mpaka, leo hii na zamani hizi, ni wachache sana kati yao ambao wangali wana nguvu kama za mungu walizofurahia katika karne zilizopita. Kwa sababu ya Mashahidi wa Yehova kuhubiri, idadi kubwa-kubwa za watu wamekuja kung’amua kwamba mafundisho mengi ya kidini wanayofundisha viongozi wa kidini ni sumu ya kiroho—“pakanga.” Zaidi ya hilo, katika Ulaya kaskazini nguvu ya viongozi wa kidini inakaribia sana kwisha, huku katika mabara mengine, serikali inapunguza sana uvutano wao. Katika Ulaya ya Kikatoliki na katika mabara ya Amerika mwenendo wa aibu wa viongozi wa kidini katika mambo ya kifedha, kisiasa, na kiadili umechafua sifa yao. Tokea sasa na kuendelea, hali yao inaweza kuzidi tu kuwa mbaya, kwa maana karibuni watapatwa na kile kile kitakachopata wanadini bandia wengine wote.—Ufunuo 18:21; 19:2.

  • Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha katika ukurasa wa 139]

      Maji ya Jumuiya ya Wakristo Yafunuliwa Kuwa Pakanga

      Itikadi na Mielekeo ya Yanayosemwa

      Jumuiya ya Wakristo Hasa na Biblia

      Jina la kibinafsi la Mungu Yesu alisali jina la Mungu

      si la maana: “Utumizi wa jina litakaswe. Petro alisema:

      la pekee lolote kwa ajili ya “Kila mmoja ambaye huita

      Mungu mmoja tu . . . haufai juu ya jina la Yehova

      kabisa kwa imani ya ulimwengu ataokolewa.” (Matendo 2:21;

      wote mzima ya Kanisa la Kikristo.” Yoeli 2:32; Mathayo 6:9, NW;

      (Dibaji ya Revised Standard Version) Kutoka 6:3; Ufunuo 4:11;

      15:3; 19:6)

      Mungu ni Utatu: “Baba ni Biblia husema Yehova ni mkuu

      Mungu, Mwana ni Mungu, kuliko Yesu naye ni Mungu

      na Roho Mtakatifu ni Mungu, na kichwa cha Yesu.

      na hata hivyo hakuna Miungu (Yohana 14:28; 20:17; 1 Wakorintho

      watatu bali Mungu mmoja.” 11:3) Roho takatifu ni kani-

      (The Catholic Encyclopedia, tendaji ya Mungu. (Mathayo 3:11;

      chapa ya 1912) Luka 1:41; Matendo 2:4)

      Nafsi ya kibinadamu ni Mtu ni nafsi. Wakati

      isiyoweza kufa: “Mtu anapokufa wa kifo nafsi huacha kufikiri

      nafsi na mwili wake hutengana. au kuhisi na hurudia mavumbi

      Mwili wake . . . huoza . . . ambayo kwayo ilifanyizwa.

      Lakini nafsi ya kibinadamu, haifi.” (Mwanzo 2:7, 3:19; Zaburi

      (What Happens After Death, 146:3, 4; Mhubiri 3:19, 20;

      kichapo cha Roma Katoliki) 9:5, 10; Ezekieli 18:4, 20, ZSB)

      Waovu huadhibiwa baada ya Mshahara wa dhambi ni kifo,

      kufa katika hell: “Kulingana si uhai katika mateso makali.

      na itikadi ya Kikristo ya (Warumi 6:23) Wafu hupumzika

      kimapokeo, hell ni mahali pa katika kaburi (Hadesi, Sheoli)

      mateso makali na maumivu.” bila fahamu, wakingojea ufufuo.

      (The World Book Encyclopedia, (Zaburi 89:48; Yohana 5:28, 29;

      chapa ya 1987) 11:24, 25; Ufunuo 20:13, 14)

      “Jina la cheo Mediatriksi Mpatanishi pekee kati ya

      [mpatanishi wa kike] linatumika Mungu na wanadamu ni Yesu.

      kuhusu [Mama Yetu].” (New (Yohana 14:6; 1 Timotheo 2:5;

      Catholic Encyclopedia, Waebrania 9:15; 12:24)

      chapa ya 1967)

      Yapasa vitoto vichanga Ubatizo ni wa wale ambao

      vibatizwe: “Tangu mwanzo wamekwisha fanywa wanafunzi na

      wenyewe Kanisa limevipa wamefundishwa kutii amri za

      vitoto vichanga Sakramenti Yesu. Ili mtu astahili ubatizo

      ya Ubatizo. Zoea hili ni lazima aelewe Neno la

      halikuonwa kuwa halali Mungu na kujizoeza imani.

      kisheria tu, bali pia (Mathayo 28:19, 20; Luka 3:21-23;

      lilifundishwa kuwa la lazima Matendo 8:35, 36)

      kabisa kwa ajili ya wokovu.”

      (New Catholic Encyclopedia

      chapa ya 1967)

      Makanisa yaliyo mengi yame- Wakristo wa Kwanza wote

      gawanywa kuwa jamii ya watu walikuwa wahudumu nao walishiriki

      wasio na cheo na jamii ya kuhubiri habari njema. (Matendo

      viongozi wa kanisa, ambao 2:17, 18; Warumi 10:10-13;

      huhudumia watu wasio na cheo. Warumi 16:1) Mkristo apaswa

      Kwa kawaida viongozi wa kidini ‘kutoa bure’ si kwa ajili

      hupewa mshahara kwa kubadili- ya mshahara. (Mathayo 10:7, 8)

      shana na huduma yao na wanatu- Yesu alikataza katakata utumizi

      kuzwa juu ya hao watu wasio wa majina ya cheo ya kidini.

      na cheo kwa majina ya cheo kama (Mathayo 6:2; 23:2-12;

      vile “Reverendi,” “Baba,” “Msifiwa.” 1 Petro 5:1-3)

      Mifano, maaikoni, na misalaba, Lazima Wakristo wakimbie kila

      hutumiwa katika ibada: ‘Mifano namna ya ibada ya sanamu,

      ya Kristo, ya Bikira Mama ya kutia na ile inayoitwa eti

      Mungu, na ya watakatifu wengine, ibada ya husiano. (Kutoka

      yapasa . . . kutunzwa katika 20:4, 5; 1 Wakorintho 10:14;

      makanisa na kupewa [staha kubwa] 1 Yohana 5:21) Wao huabudu

      na heshima inayostahili. (Julisho-Wazi Mungu si kwa mwono bali

      la Baraza la Trent [1545-63]) kwa roho na kweli. (Yohana

      4:23, 24; 2 Wakorintho 5:7)

      Washiriki wa Kanisa wanafundishwa Yesu alihubiri Ufalme wa

      kwamba makusudi ya Mungu yata- Mungu, si mfumo fulani wa

      timizwa kupitia siasa. Kardinali kisiasa, kuwa ndio tumaini

      Spellman ambaye sasa amekufa kwa ajili ya aina ya binadamu.

      alitaarifu hivi: “Kuna barabara (Mathayo 4:43; 6:9, 10)

      moja tu ya kufikia amani . . . , Yeye alikataa kujihusisha

      barabara kuu ya kidemokrasia.” katika siasa. (Yohana 6:14, 15)

      Taarifa za habari huripoti juu ya Ufalme wake ulikuwa si sehemu

      kujiingiza kwa dini katika siasa za ya ulimwengu huu; kwa sababu

      ulimwengu (hata katika vitendo vya hiyo, wafuasi wake walipaswa

      kufitini serikali) na uungaji-mkono wayo wawe si sehemu ya

      wa UM kuwa “ndilo tumaini la mwisho ulimwengu. (Yohana 18:36;

      la itifaki na amani.” 17:16) Yakobo alionya juu

      ya urafiki na ulimwengu. (Yakobo 4:4)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki