-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“‘Na mimi nitafanya mashahidi wangu wawili watoe unabii siku elfu moja mia mbili na sitini wakiwa wamevalia nguo za magunia.’
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
11. Ilimaanisha nini kwa Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu kutoa unabii “wakiwa wamevalia nguo za magunia”?
11 Wakristo hawa wapakwa-mafuta waaminifu walihitaji sifa ya uvumilivu, kwa kuwa walipaswa kutoa unabii “wakiwa wamevalia nguo za magunia.” Hiyo ilimaanisha nini? Katika nyakati za Biblia mara nyingi nguo ya gunia ilifananisha maombolezo. Kuivaa kulikuwa ishara ya kwamba mtu alikuwa ameshushwa katika huzuni au dhiki. (Mwanzo 37:34; Ayubu 16:15, 16; Ezekieli 27:31, NW) Nguo ya gunia ilishirikishwa na jumbe za maombolezo za maangamizi au huzuni ambazo manabii wa Mungu walipaswa kupigia mbiu. (Isaya 3:8, 24-26; Yeremia 48:37; 49:3) Kuvaa nguo ya gunia kungeweza kuonyesha unyenyekevu au toba kwa sababu ya onyo la kimungu. (Yona 3:5) Nguo za Magunia zenye kuvaliwa na mashahidi wawili huonekana kuwa zinaonyesha uvumilivu wa unyenyekevu katika kutangaza hukumu za Yehova. Wao walikuwa mashahidi wakipiga mbiu ya siku yake ya kisasi ambayo ingeleta pia maombolezo kwa mataifa hayo.—Kumbukumbu 32:41-43.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Wao walihubiri ujumbe wa “nguo za magunia” kuhusu hukumu za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo na ulimwengu.
-