Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Tunakuachisha Kazi”
    Amkeni!—2010 | Julai
    • “Tunakuachisha Kazi”

      WASIMAMIZI wa kampuni walimwona Fred kuwa mfanyakazi bora.a Mbinu zake zilikuwa zimesaidia kampuni hiyo kupata faida kubwa katika miaka sita ambayo alikuwa ameajiriwa. Kwa hiyo, alipoitwa kwenye ofisi ya meneja mmoja, Fred alitazamia kwamba angeongezwa mshahara au kupandishwa cheo. Badala yake, meneja huyo alimwambia, “Tunakuachisha kazi.”

      Fred hakuamini alichokuwa amesikia. “Nilikuwa nikipata mshahara mnono na nilikuwa nikifurahia kazi yangu, lakini kila kitu kilibadilika ghafula,” akasema. Baadaye, Fred alimwambia mke wake Adele kile kilichokuwa kimetokea, naye pia akashtuka sana. Adele anasema hivi: “Nilijihisi hoi kabisa. Nilijiuliza, ‘Sasa tutafanya nini?’”

      Mamilioni ya watu hupatwa na hali iliyompata Fred kama unavyoweza kuona katika tarakimu zilizo hapa chini. Hata hivyo, tarakimu pekee hazionyeshi jinsi watu wanavyoathiriwa kihisia wanapofutwa kazi. Fikiria kisa cha Raúl, mhamiaji kutoka Peru ambaye aliachishwa kazi katika hoteli moja kubwa huko New York City ambako alikuwa ameajiriwa kwa miaka 18. Raúl alijaribu kutafuta kazi, lakini hakufaulu. Anasema hivi: “Nilikuwa nimeiandalia familia yangu mahitaji yake kwa miaka 30 hivi. Sasa nilihisi kuwa nimeshindwa kutimiza wajibu wangu nikiwa kichwa cha familia.”

      Kisa cha Raúl kinaonyesha kwamba watu wanaopoteza kazi hupatwa na matatizo mengi zaidi ya yale ya kiuchumi. Mara nyingi, wanapatwa na maumivu makali ya kihisia. “Nilianza kuhisi kuwa sifai kitu,” anasema Renée ambaye mume wake anayeitwa Matthew alikuwa ameachishwa kazi kwa zaidi ya miaka mitatu. “Ikiwa huna pesa, watu huanza kukudharau, na baada ya muda wewe pia unaanza kujidharau.”

      Mbali na maumivu ya kihisia, mtu ambaye ameachishwa kazi huanza kukabiliana na ugumu wa kuishi kwa mapato madogo. Fred anasema: “Tulipokuwa na pesa hatukuwahi kufikiria kuhusu kupunguza matumizi. Lakini sasa tulikuwa hatuna kazi, na gharama zilikuwa zilezile, kwa hiyo, tulilazimika kupunguza matumizi yetu.”

  • “Msiwe na Wasiwasi Juu ya Kesho”
    Amkeni!—2010 | Julai
    • “Msiwe na Wasiwasi Juu ya Kesho”

      Renée alikuwa amekata tamaa. Mume wake Matthew, hakuwa ameajiriwa kwa zaidi ya miaka mitatu. “Nilikuwa nimefadhaika sana,” anasema Renée. “Nilivunjika moyo sana kwa kuwa sikujua ni nini ambacho kingetokea!” Matthew alijaribu kumtuliza mke wake kwa kumweleza kwamba hakuna wakati ambapo wamewahi kukosa kile walichohitaji. “Lakini bado huna kazi!” Renée akajibu. “Tunahitaji pesa!”

  • “Msiwe na Wasiwasi Juu ya Kesho”
    Amkeni!—2010 | Julai
    • Rebekah, ambaye mume wake alikuwa amepoteza kazi aliyokuwa ameifanya kwa miaka 12 anasema hivi: “Unapokabiliwa na hisia kali, ni vigumu kufikiria mambo kihalisi. Lakini tulilazimika kufanya hivyo. Kwa hiyo, nilijaribu kudhibiti hisia zangu. Mambo yaliyonitia wasiwasi yalipokosa kutokea, nilitambua kwamba kuhangaika hakuna faida yoyote. Tulipokazia fikira mambo ya sasa na matatizo yaliyokuwapo, tulipunguza mfadhaiko.”

  • “Msiwe na Wasiwasi Juu ya Kesho”
    Amkeni!—2010 | Julai
    • Renée alifaulu kukuza sifa ya kuridhika baada ya kuona hali yake kihalisi. Anasema hivi: “Hatujawahi kukosa umeme au gesi, wala hatujakosa makao. Tatizo kuu ni kwamba hatukuwa tumezoea kuishi kwa njia hiyo, na tamaa yangu ya kudumisha maisha tuliyokuwa nayo iliongeza tu mfadhaiko wangu.”

      Punde si punde, Renée alitambua kwamba si hali zake zilizofanya maisha yake yawe magumu bali ni mtazamo wake. Anasema hivi: “Nilihitaji kuona hali yetu kihalisi bila kukazia fikira jinsi nilivyotaka mambo yawe. Nilipoanza kuridhika na yale ambayo Mungu alituandalia kila siku, nilikuwa na furaha zaidi.”

  • “Msiwe na Wasiwasi Juu ya Kesho”
    Amkeni!—2010 | Julai
    • Hivyo, mume wa Renée alipoachishwa kazi, aliwaambia hivi watoto wake: “Akina baba wengi wameacha familia zao. Lakini baba yenu bado yuko. Mnajua kwamba anawapenda na amewasaidia mlipokuwa na matatizo. Hamwezi kupata baba mzuri kuliko yeye!”

  • Jinsi ya Kupunguza Gharama
    Amkeni!—2010 | Julai
    • Raúl alipoachishwa kazi, mke wake Bertha, alibadili mbinu yake ya kununua vitu. Anasema, “Niliangalia matangazo yaliyoonyesha mahali ambapo bidhaa zimepunguzwa bei na maduka ya mboga yaliyouza vitu viwili kwa bei ya kimoja.”

  • Jinsi ya Kupunguza Gharama
    Amkeni!—2010 | Julai
    • Fred anasema, “Tulilazimika kupanga bajeti, kwa hiyo, niliandika gharama ambazo tulihitaji kulipa mara moja na pesa za matumizi ya mwezi mzima.” Mke wake, Adele, anasema hivi: “Nilijua ni pesa ngapi nitakazotumia ninapoenda sokoni. Nyakati nyingine nilipohitaji kununua kitu cha nyumbani au kwa ajili ya watoto, niliitazama bajeti na kujiambia, ‘Sina pesa za kukinunua, kwa hiyo, tutasubiri hadi mwezi ujao.’ Kuandika kulinisaidia sana!”

  • Jinsi ya Kupunguza Gharama
    Amkeni!—2010 | Julai
    • Ili uokoe pesa unazotumia kununua vitu visivyo vya lazima, uwe mbunifu. Kwa mfano, Adele anasema hivi: “Tulikuwa na magari mawili lakini tukauza moja na kutumia hilo lingine. Ili tuokoe pesa tulizotumia kununua petroli, tulipanga kufanya shughuli nyingi kwa wakati mmoja. Tulitumia pesa kwa ajili tu ya vitu vya lazima.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki