-
Nimebarikiwa kwa Urithi wa PekeeMnara wa Mlinzi—2000 | Oktoba 1
-
-
Kesi ya Babu na Maisha Yake Gerezani
Katika sebule ya Patterson, mimi na Paul tuliona pia picha iliyo kwenye ukurasa unaofuata. Niliitambua picha hii mara moja, kwa kuwa Babu alinitumia nakala moja miaka 50 iliyopita. Ndiye aliyesimama mwisho kulia.
Wakati wa msisimko wa kizalendo uliotokea wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, hao Wanafunzi wanane wa Biblia—kutia ndani Joseph F. Rutherford (aliyeketi katikati), msimamizi wa Watch Tower Society—walitiwa gerezani kimakosa na kuzuiwa bila dhamana. Mashtaka dhidi yao yalihusu taarifa zilizo katika buku la saba la Studies in the Scriptures, lenye kichwa The Finished Mystery. Taarifa hizo zilieleweka vibaya kuwa zenye kuvunja moyo Marekani isishiriki katika Vita ya Ulimwengu ya Kwanza.
Kwa kipindi cha miaka mingi, Charles Taze Russell aliandika mabuku sita ya Studies in the Scriptures, lakini alikufa kabla hajaandika buku la saba. Kwa hiyo Babu na Mwanafunzi wa Biblia mwingine walipewa maandishi yake, nao wakaandika buku la saba. Hilo lilitolewa mwaka wa 1917, kabla ya mwisho wa vita. Kwenye kesi hiyo, Babu na wengi wa wale wenzake walihukumiwa vifungo vinne, kila mmoja kifungo cha miaka 20, vyote vikiambatana pamoja.
Maelezo ya picha kwenye sebule ya Patterson yasema: “Miezi tisa baada ya Rutherford na wenzake kuhukumiwa—na vita ikiwa imekwisha—Machi 21, 1919, mahakama ya rufani iliamuru washtakiwa wote wanane waachiliwe kwa dhamana, na Machi 26, walifunguliwa huko Brooklyn kwa dhamana ya dola 10,000 kila mmoja. Mei 5, 1920, J. F. Rutherford na wenzake waliondolewa mashtaka.”
Baada ya kuhukumiwa, lakini kabla ya kupelekwa kwenye gereza kuu la serikali la Atlanta, Georgia, ndugu hao wanane walikaa kwa siku chache kifungoni katika jela ya Raymond Street huko Brooklyn, New York. Akiwa huko Babu aliandika akieleza jinsi alivyowekwa ndani ya seli ya meta 1.8 kwa meta 2.4 “katikati ya uchafu wenye kutisha na mvurugo.” Alisema: “Unaona rundo la magazeti, na ukiyapuuza mara ya kwanza, unakuja kugundua kwamba makaratasi hayo na sabuni na kitambaa cha kuogea, humaanisha fursa yako ya kuwa safi na kujipatia heshima.”
Hata hivyo, Babu alidumisha ucheshi wake, akiita jela hiyo “Hôtel de Raymondie” na kusema, “Nitaondoka hapa siku zangu za malazi zitakapokwisha.” Pia alifafanua matembezi yake ya uani. Wakati mmoja aliposimama ili achanwe nywele zake, mnyakuzi wa mifukoni aliiba saa yake ya mfukoni, lakini kama alivyoandika, “Mnyororo wake ulikatika nami nikaiokoa.” Nilipokuwa nikitembelea Betheli ya Brooklyn mwaka wa 1958, Grant Suiter, aliyekuwa mwandishi mweka-hazina wa Watch Tower Society, aliniita kwenye ofisi yake na kunipa saa hiyo. Ningali naithamini sana.
-
-
Nimebarikiwa kwa Urithi wa PekeeMnara wa Mlinzi—2000 | Oktoba 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 27]
Wanafunzi wa Biblia wanane waliofungwa kimakosa mwaka wa 1918 (Babu akiwa amesimama mwisho kulia)
-