-
Kumkumbuka Muumba Wetu Kutoka Ujanani KuendeleaMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
-
-
Muda mfupi baada ya hapo, walitembelewa na William Evans, mmoja wa Wanafunzi wa Biblia, kama vile Mashahidi wa Yehova walivyoitwa wakati huo. Baba, ambaye wakati huo alikuwa katika miaka yake ya kati ya 20 na mama ambaye alikuwa mchanga kwa miaka mitano, walimsikiliza mwanamume huyo mwenye urafiki kutoka Wales na kumwalika kwa mlo. Punde si punde wakakubali kweli za Biblia walizokuwa wakijifunza.
-
-
Kumkumbuka Muumba Wetu Kutoka Ujanani KuendeleaMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
-
-
Hata ingawa Ndugu Evans na mke wake Miriam hawakuwa na watoto, walikuja kuwa wazazi na babu na nyanya wa kiroho kwa familia yetu. Kwa kawaida William alimwita Baba “Mwanangu,” na yeye pamoja na Miriam walitia ndani ya familia yetu roho ya kueneza evanjeli. Mapema katika karne ya 20, Ndugu Evans alikuwa amefunga safari kadhaa kurudi huko Wales ili kujulisha kweli ya Biblia katika eneo linalozunguka Swansea. Huko alijulikana kama yule mhubiri kutoka Marekani.
Katika mwaka wa 1928, Ndugu Evans aliacha kazi yake ya kuajiriwa akaanza kuhubiri katika milima ya West Virginia. Kaka zangu wawili Clarence aliyekuwa na umri wa miaka 21 na Carl aliyekuwa na umri wa miaka 19, waliandamana naye. Sisi sote wavulana wanne tulitumia miaka mingi katika huduma ya wakati wote. Kwa hakika, sisi sote tulitumikia tukiwa waangalizi-wasafirio wa Mashahidi wa Yehova tukiwa vijana. Muda mfupi uliopita dada mchanga zaidi wa Mama, Mary, ambaye ana umri wa miaka ya 90, aliniandikia hivi: “Tu wenye shukrani kama nini kwamba Ndugu Evans alikuwa na bidii kwa ajili ya huduma na akatembelea Grove City!” Shangazi Mary pia amemkumbuka Muumba wake tangu ujana.
-