-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Lakini mmoja wa wale wazee asema kwangu mimi: ‘Acha kutoa machozi. Tazama! Simba ambaye ni wa kabila la Yuda, mzizi wa Daudi, ameshinda ili kufungua hati-kunjo na vifungo saba vyayo.’” (Ufunuo 5:5, NW)
-
-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
7. Ni nini kinachomstahilisha Yesu kuchukua hati-kunjo kutoka mkono wa Mmoja anayeketi juu ya kiti cha ufalme?
7 Yesu ndiye mmoja ambaye kwa kutokeza sana, akiwa binadamu mkamilifu, alitumikia Yehova katika ukamilifu na chini ya majaribu yenye maumivu makali sana. Yeye alitoa jawabu kamili kwa dai la Shetani. (Mithali 27:11) Hivyo, yeye angeweza kusema kama alivyosema katika ule usiku kabla ya kifo chake cha dhabihu, “mimi nimeshinda ulimwengu.” (Yohana 16:33, NW) Kwa sababu hiyo, Yehova alimwaminisha Yesu aliyefufuliwa “mamlaka yote katika mbingu na juu ya dunia.”
-
-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
11. Ni kwa nini si utovu wa adhama kumwakilisha Yesu aliyetukuzwa kuwa “mwana-kondoo kana kwamba alikuwa amechinjwa”?
11 Je! kwa vyovyote ni kumfanya mdogo au utovu wa adhama kuwakilisha Yesu aliyetukuzwa kuwa “mwana-kondoo kana kwamba alikuwa amechinjwa”? Sivyo kabisa! Ule uhakika wa kwamba Yesu alibaki akiwa mwaminifu mpaka kifo ulikuwa ushinde mkuu kwa Shetani na ushindi mkubwa wenye shangwe kwa Yehova Mungu. Kumwakilisha Yesu katika njia hii huonyesha waziwazi ushindi wake juu ya ulimwengu wa Shetani na ni kikumbusho cha ule upendo wenye kina walio nao Yehova na Yesu kwa aina ya binadamu. (Yohana 3:16; 15:13; linga Wakolosai 2:15.) Hivyo Yesu anaonyeshwa kuwa ile Mbegu iliyoahidiwa, akiwa na sifa zinazofaa zenye kutokeza kufungua ile hati-kunjo.—Mwanzo 3:15.
-