-
Mbingu Mpya na Dunia MpyaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Wale Wanaoshinda
11. Ni ahadi gani ambayo Yehova anafanya, na maneno hayo yanatumika kwa nani kwanza?
11 Wale wanaokunywa ya hayo “maji” yenye kuburudisha lazima pia washinde, kama Yehova aendeleavyo kusema: “Yeyote ambaye anashinda atarithi vitu hivi, na mimi nitakuwa Mungu wake na yeye atakuwa mwana wangu.” (Ufunuo 21:7, NW)
-
-
Mbingu Mpya na Dunia MpyaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
12. Ahadi ya Yehova kwenye Ufunuo 21:7 itatimizwaje kuelekea umati mkubwa?
12 Umati mkubwa kutoka mataifa yote pia watazamia ahadi hii. Lazima wao pia washinde, wakitumikia Mungu kishikamanifu mpaka watoke katika dhiki kubwa. Ndipo wao watakapoingia katika urithi wao wa kidunia, ‘ufalme uliotayarishwa kwa ajili yao tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.’ (Mathayo 25:34, NW) Hawa pamoja na wengine wa kondoo wa Bwana wa kidunia ambao hupita mtihani mwishoni mwa miaka elfu huitwa “watakatifu.” (Ufunuo (20:9) Watafurahia uhusiano mtakatifu na wa kibaba na kimwana pamoja na Muumba wao, Yehova Mungu, wakiwa washiriki wa tengenezo lake la ulimwengu wote mzima.—Isaya 66:22; Yohana 20:31; Warumi 8:21.
13, 14. Ili kurithi ahadi tukufu za Mungu, ni mazoea gani ambayo ni lazima sisi tuepuke kwa dhati, na kwa nini?
13 Wakiwa na tazamio tukufu hili, ni jambo la maana kama nini kwamba Mashahidi wa Yehova sasa wabaki wakiwa safi bila vitu vyenye kunajisi vya ulimwengu wa Shetani! Sisi twahitaji kuwa imara, wenye dhati, na wenye kuazimia kwamba Ibilisi hatatuburuta kamwe na kutuingiza ndani ya kampuni ambayo Yehova mwenyewe anaeleza hapa? “Lakini kwa habari ya waoga na wale bila imani na wale ambao ni wenye kunyarafisha kwa uchafu wao na wauaji kimakusudi na waasherati na wale ambao huzoea uwasiliano na roho na waabudu sanamu na waongo wote, aria yao itakuwa katika ziwa ambalo huwaka moto na salfa. Hii humaanisha kifo cha pili.” (Ufunuo 21:8, NW) Ndiyo, yeye ambaye angekuwa mrithi lazima aepuke mazoea ambayo yamechafua huu mfumo wa mambo wa kale. Lazima yeye ashinde kwa kubaki akiwa mwaminifu usoni mwa mibano yote na vishawishi.—Warumi 8:35-39.
14 Jumuiya ya Wakristo, ijapokuwa inadai kuwa bibi-arusi wa Kristo, inatambuliwa kwa mazoea yenye kunyarafisha ambayo Yohana anaeleza hapa. Kwa hiyo inaenda kwenye uharibifu wa milele pamoja na sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa. (Ufunuo 18:8, 21) Hali kadhalika, wowote wa wapakwa-mafuta au wa umati mkubwa ambao huchukua mazoea kama hayo ya kufanya maovu, au kuanza kutia moyo yafanywe, wakabili uharibifu wa milele. Wakiendelea na matendo haya, hawatarithi ahadi hizi. Na katika dunia mpya, wowote wanaojaribu kuleta mazoea kama hayo wataharibiwa kwa kasi sana, wakiingia ndani ya kifo cha pili bila tumaini la ufufuo.—Isaya 65:20.
-