-
Washa Upya Upendo wa Kwanza!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Yeye Ambaye Hushinda”
13. (a) Ni baraka gani iliyongojea Waefeso ikiwa ‘wangeshinda’? (b) Wakristo Waefeso ‘wangeshindaje’?
13 Kwa kumalizia, kama afanyavyo pia katika jumbe zake nyingine, Yesu anavuta fikira kwenye roho ya Mungu kuwa inajulisha kupitia Yesu zile thawabu kwa ajili ya uaminifu. Kwa Waefeso yeye anasema hivi: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye hushinda mimi nitaruhusu ale ya mti wa uhai, uliomo katika paradiso ya Mungu.” (Ufunuo 2:7, NW) Wale walio na masikio ya kusikia wangekuwa na hamu nyingi ya kutii ujumbe huo muhimu, wakijua kwamba haukuja kwa kuanzishwa na Yesu bali kwamba huo ulishuka kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Mkuu Yehova mwenyewe kupitia roho takatifu Yake, au kani-tendaji. Wao wangeweza ‘kushindaje’? Kwa kufuata kwa ukaribu hatua za Yesu, ambaye alishika ukamilifu mpaka kifo na hivyo angeweza kusema: “Jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu!”—Yohana 8:28; 16:33; ona pia 1 Yohana 5:4.
14. Ni lazima “paradiso ya Mungu” aliyotaja Yesu iwe ilirejezea nini?
14 Kwa kuwa hao hawana tazamio la kuishi katika paradiso ya kidunia, Wakristo watiwa-mafuta, kama hao Waefeso, wanathawabishwaje kwa kula “ya mti wa uhai, uliomo katika paradiso ya Mungu”? Hiyo haingeweza kuwa Paradiso iliyorudishwa duniani, kwa kuwa Wakristo watiwa-mafuta 144,000, kutia na wale wa kundi la Efeso, wananunuliwa kutoka wanadamu wakatawale pamoja na Mwana-Kondoo, Kristo Yesu, juu ya Mlima Sayuni wa kimbingu wakiwa wana wa kiroho. (Efeso 1:5-12; Ufunuo 14:1, 4) Kwa sababu hiyo, lile rejezo hapa lazima liwe kwenye makao ya kimbingu mithili ya bustani wanayorithi hao washindi. Humo, “katika paradiso ya Mungu,” ndiyo, katika kuwapo halisi kwa Yehova mwenyewe, washindi hawa ambao wameruhusiwa wawe na kutokufa wataendelea kuishi milele, kama inavyofananishwa hapa na kula kwao ya mti wa uhai.
-
-
Kujitahidi Kuwa WashindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
6. (a) Ni kwa nini Wakristo katika Smirna hawakupaswa kuogopa? (b) Yesu alimaliziaje ujumbe wake kwa kundi katika Smirna?
6 Hata hivyo, hao Wakristo katika Smirna hawapaswi kuogopa au kuacha msimamo wao. Ikiwa wao wanabaki waaminifu mpaka mwisho, wamewekewa “taji la uhai” kuwa thawabu, kwao ikiwa ni uhai usioweza kufa katika mbingu. (1 Wakorintho 9:25; 2 Timotheo 4:6-8, NW) Mtume Paulo aliiona zawadi hii yenye thamani kubwa kuwa inastahili kudhabihiwa kila kitu kinginecho chote, hata uhai wake wa kidunia. (Wafilipi 3:8) Kwa wazi, hao waaminifu katika Smirna wanahisi jinsi iyo hiyo. Yesu anamalizia ujumbe wake kwa kusema: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye hushinda hatadhuriwa kwa vyovyote na kifo cha pili.” (Ufunuo 2:11, NW) Washindi wanahakikishiwa uhai wa kimbingu usioweza kufa ambao hauwezi kuguswa na kifo.—1 Wakorintho 15:53, 54.
-
-
Kujitahidi Kuwa WashindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Jithibitishe mwenyewe kuwa mwaminifu mpaka hata kifo, na mimi nitakupa wewe taji la uhai.” (Ufunuo 2:10, NW)
-