Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kurudi kwa Kristo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Maneno “anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona” yanamaanisha nini?

      Ufu. 1:7: “Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, na wale waliomchoma; na makabila yote ya dunia yatajipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake.” (Ona pia Mathayo 24:30; Marko 13:26; Luka 21:27.)

  • Kurudi kwa Kristo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • “Kila jicho litamwona” jinsi gani? Watatambua kutokana na matukio duniani kwamba yeye yupo ijapokuwa haonekani kwa macho. Pia likielekezea kuona ambako si kwa macho halisi, andiko la Yohana 9:41 linasema hivi: “Yesu akawaambia [Mafarisayo]: ‘Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na dhambi. Lakini sasa mnasema, “Tunaona.” Dhambi yenu inabaki.’” (Linganisha na Waroma 1:20.) Baada ya kurudi kwa Kristo, watu fulani wanaamini; wanaitambua ishara ya kuwapo kwake. Wengine wanakataa uthibitisho, lakini Kristo atakapoanza kutenda akiwa yule aliyewekwa na Mungu kuwaangamiza waovu, wataona nguvu zake na kutambua kwamba uharibifu huo hautoki kwa wanadamu bali unatoka mbinguni. Watajua linalotukia kwa sababu walikuwa wameonywa mapema. Kwa sababu ya jambo linalowapata, ‘watajipiga-piga kwa kuomboleza.’

      “Wale waliomchoma” ni nani? Kihalisi, askari wa Roma ndio waliomchoma Yesu alipouawa. Lakini walikufa zamani. Kwa hiyo, maneno hayo yanamaanisha watu wanaowatendea vibaya jinsi hiyohiyo, au ‘wanaowachoma,’ wafuasi wa kweli wa Kristo wakati wa “siku za mwisho.”—Mt. 25:40, 45.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki