-
Mungu Yumo Katika Hekalu Lake TakatifuUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
1, 2. (a) Nabii Isaya apata ono lake la hekalu lini? (b) Kwa nini Mfalme Uzia alipoteza upendeleo wa Yehova?
“KATIKA mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana [“Yehova,” “NW”] ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.” (Isaya 6:1)
-
-
Mungu Yumo Katika Hekalu Lake TakatifuUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
3. (a) Je, Isaya amwona Yehova kihalisi? Eleza. (b) Isaya aona mandhari gani, na kwa kusudi gani?
3 Hatuelezwi mahali alipo Isaya aonapo ono hilo. Lakini kwa wazi yale ayaonayo kwa macho yake halisi ni ono, wala hamwoni Mweza Yote kihalisi, kwa kuwa “hakuna mtu ambaye amemwona Mungu wakati wowote.” (Yohana 1:18; Kutoka 33:20) Ijapokuwa hivyo, bado ni jambo lenye kutisha kumwona Muumba, Yehova, hata katika ono. Aketiye katika kiti cha ufalme, kinachowakilisha daraka lake la kuwa Mfalme na Hakimu adumuye milele, ndiye Mtawala wa Ulimwengu Wote na aliye Chanzo cha utawala wote wa kiserikali wenye haki! Pindo za kanzu yake ndefu na yenye kuning’inia zalijaza hekalu. Isaya apewa wito wa kufanya utumishi wa unabii utakaotukuza nguvu kuu na haki ya Yehova. Ili kujitayarishia hilo, ataonyeshwa ono la utakatifu wa Mungu.
4. (a) Kwa nini hapana shaka kwamba ufafanuzi mbalimbali juu ya Yehova unaoonekana katika maono na kurekodiwa katika Biblia ni ufananisho? (b) Twajifunza nini juu ya Yehova kupitia ono la Isaya?
4 Isaya haelezi kuonekana kwa Yehova katika ono lake—tofauti na maono yaliyoripotiwa na Ezekieli, Danieli, na Yohana. Na masimulizi hayo yote yatofautiana juu ya mambo yanayoonekana huko mbinguni. (Ezekieli 1:26-28; Danieli 7:9, 10; Ufunuo 4:2, 3) Hata hivyo, lazima tuzingatie hali na kusudi za maono hayo. Hayo si ufafanuzi halisi wa kuwapo kwa Yehova. Jicho halisi haliwezi kuona kilicho cha kiroho, wala akili hafifu ya mwanadamu haiwezi kuelewa milki ya roho. Kwa hiyo, maono hayo yapasha habari inayopasa kuwasilishwa kwa maneno ya kibinadamu. (Linganisha Ufunuo 1:1.) Katika ono la Isaya, ufafanuzi wa sura ya Mungu si wa lazima. Ono hilo lamwarifu Isaya kuwa Yehova yumo katika hekalu lake takatifu na kwamba yeye ni mtakatifu na hukumu zake ni kamilifu.
-