-
Volkeno—Je, Umo Hatarini?Amkeni!—1996 | Mei 8
-
-
Wanasayansi wametambua kuwa volkeno hizo hutokea kwenye mipaka ya vipande au mabamba makubwa yaliyo mwendoni, hasa mahali ambapo bamba la bahari-kuu huingia chini ya lile la nchi kavu. Utendaji huo huitwa subduction. Joto linalotokezwa na miendo hiyo huyeyusha mawe ambayo huinuka hadi kwenye uso wa dunia. Kwa kuongezea, miendo ya ghafula kati ya mabamba husababisha matetemeko ya dunia yenye nguvu katika sehemu nyingi za maeneo yakumbwayo na milipuko ya volkeno.
Pia volkeno hutokea sehemu ambapo mabamba ya bahari-kuu huachana. Mingi ya milipuko hiyo hutukia kwenye sakafu ya bahari-kuu nayo haionekani na mwanadamu. Hata hivyo, ikiwa waishi katika nchi ya kisiwa cha Iceland, uko juu ya Mwinuko wa Reykjanes, uunganao na Mwinuko wa Atlantiki ya Kati, ambapo mabamba yanayotia ndani Amerika Kaskazini na Kusini yanaachana na yale yanayotia ndani Ulaya na Afrika. Katika visa vingine vichache, sehemu moto zilizo peke yazo chini ya mabamba ya uso wa dunia zimetokeza volkeno kubwa katika Hawaii na kwenye kontinenti ya Afrika.
-
-
Volkeno—Je, Umo Hatarini?Amkeni!—1996 | Mei 8
-
-
Kwa ujumla, milipuko iliyo hatari zaidi hutokezwa na mawe yaliyoyeyushwa yenye silika nyingi. Aina hii ya mawe yaliyoyeyushwa ni nzito, na yaweza kwa muda fulani kuziba volkeno hadi kanieneo iwe ya kutosha kulipua volkeno. Mawe yaliyoyeyushwa yenye silika nyingi hukamatana na kuwa mawe yenye rangi-nyepesi nayo ni ya kawaida kwa volkeno kwenye mipaka ya mabamba. Milipuko pia yaweza kutokea wakati mawe yaliyoyeyushwa yakutanapo na maji na kuyafanya yawe mvuke. Majivu moto yatokezwayo na milipuko yaweza kufisha—volkeno tatu katika eneo la Karibea ya Kati ya Amerika ziliua zaidi ya watu 36,000 kwa kipindi cha miezi sita katika 1902.
Kwa upande mwingine, sehemu moto za bahari-kuu na volkeno zitokeazo mabamba yaachanapo, na nyingine nyingi, kwa sehemu kubwa hufanyizwa na mawe meusi mazito, ambayo yana silika kidogo lakini yenye chuma na magnesi kwa wingi. Mawe meusi yaliyoyeyushwa kwa kawaida huwa majimaji na hutokeza milipuko midogo au mibubujiko isiyolipuka na pia mtiririko wa mawe yaliyoyeyushwa wa polepole ulio rahisi kuepukwa na watu. Hata hivyo, milipuko hiyo yaweza kudumu—volkeno ya Kilauea katika kisiwa cha Hawaii imekuwa ikilipuka kwenye hicho kisiwa kwa mfululizo tangu Januari 1983. Ingawa uharibifu wa mali nyingi umetokana na mlipuko kama huo, hiyo huumiza au kuua watu mara chache sana.
-