-
Vita vya Kidini Katika UfaransaAmkeni!—1997 | Aprili 22
-
-
Wawaldensi walipata mshindo kamili wa upinzani rasmi. Wao walikuwa kikundi cha watu wachache waliokaza fikira kwenye Biblia ambao waliishi katika vijiji maskini kusini-mashariki mwa nchi hiyo. Wengine walichomwa kwenye miti ya mateso, mamia yakachinjwa, na vijiji 20 hivi vikaangamizwa.—Ona sanduku kwenye ukurasa wa 6.
-
-
Vita vya Kidini Katika UfaransaAmkeni!—1997 | Aprili 22
-
-
“Kadinali de Tournon, akidai kwamba Wawaldense walikuwa na njama ya kupindua serikali, alimshawishi Mfalme mgonjwa mwenye kusitasita atie sahihi agizo (Januari 1, 1545) kwamba Wawaldense wote waliopatikana na hatia ya kuasi mafundisho ya kidini wauawe. . . . Kwa kipindi cha juma moja (Aprili 12-18) vijiji kadhaa viliteketezwa kabisa; katika kimoja wanaume, wanawake, na watoto 800 walichinjwa; katika miezi miwili 3,000 waliuawa, vijiji 22 kuteketezwa, na wanaume 700 wakapelekwa kwenye merikebu za kwenda vitani. Wanawake 25 waliopigwa na hofu, wakitafuta kimbilio uvunguni mwa ardhi, walisongwa pumzi kwa kukosa oksijeni kwa sababu ya moto uliowashwa kwenye kiingilio.”
Kuhusu matukio kama hayo ya kihistoria, Durant alisema hivi: “Minyanyaso hii ndiyo iliyokuwa kutofaulu kabisa kwa utawala wa akina Francis.” Lakini hilo lilikuwa na matokeo gani kwa wale waliotazama uthabiti wa Wawaldense wakati wa minyanyaso iliyoamriwa na mfalme? Durant aliandika: “Moyo mkuu wa wafia-imani hao ulipatia mwendo wao adhama na fahari; ni lazima maelfu ya watazamaji yalipendezwa na kusumbuliwa, ambayo bila hukumu hizo zenye kutazamisha, huenda hayangeshughulika kamwe kubadili imani yao iliyorithiwa.”
-