-
“Njia na Kweli na Uzima”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
“Mimi Ndiye Njia”
11. (a) Kwa nini tunaweza kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu kupitia Yesu tu? (b) Andiko la Yohana 14:6 linakazia jinsi gani cheo cha pekee cha Yesu? (Ona maelezo ya chini.)
11 Tayari tumejifunza kwamba hatuwezi kumfikia Mungu isipokuwa kupitia Yesu. Fikiria jinsi sisi binafsi tunavyohusika. Yesu ndiye “njia” katika maana ya kwamba tunaweza kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu kupitia kwake tu. Kwa nini? Yesu alikuwa mwaminifu mpaka alipokufa, naye aliutoa uhai wake uwe dhabihu ya fidia. (Mathayo 20:28) Bila fidia hiyo, hatuwezi kumfikia Mungu. Dhambi inawazuia wanadamu wasimfikie Mungu, kwa kuwa Yehova ni mtakatifu naye hawezi kukubali dhambi. (Isaya 6:3; 59:2) Lakini dhabihu ya Yesu iliondolea mbali kizuizi hicho; ilifunika dhambi, au kutupatanisha na Mungu. (Waebrania 10:12; 1 Yohana 1:7) Tukiukubali mpango huo wa Mungu kupitia Kristo na kuuamini, tunaweza kupata kibali cha Yehova. Hakuna njia nyingine ya ‘kupatanishwa na Mungu.’c—Waroma 5:6-11.
12. Yesu “ndiye njia” katika maana gani?
12 Yesu “ndiye njia” ya kumfikia Mungu katika sala. Ni kupitia Yesu tu tunaweza kumfikia Yehova katika sala tukiwa na uhakika kwamba maombi yetu ya kutoka moyoni yatasikiwa vizuri. (1 Yohana 5:13, 14) Yesu mwenyewe alisema: “Mkimwomba Baba jambo lolote atawapa katika jina langu. . . . Ombeni nanyi mtapokea, ili shangwe yenu ipate kujazwa.” (Yohana 16:23, 24) Kwa hiyo, tukitumia jina la Yesu, tunaweza kumfikia Yehova katika sala na kumwita “Baba yetu.” (Mathayo 6:9) Yesu “ndiye njia” katika maana nyingine, yaani, alituwekea mfano wa kufuata. Kama ilivyokwisha kutajwa, Yesu alimwiga Baba yake kikamili. Hivyo, mfano wa Yesu unaonyesha jinsi tunavyoweza kumpendeza Yehova katika maisha yetu. Basi ili kumfikia Yehova, lazima tutembee katika hatua za Yesu.—1 Petro 2:21.
-
-
“Njia na Kweli na Uzima”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
c Kwenye Yohana 14:6, maneno “mimi ndiye” yanakazia cheo cha pekee cha Yesu, kwamba yeye ndiye njia. Tunaweza kumfikia Baba kupitia kwake tu.
-