-
Masomo Yenye Kutumika Kutokana na Bara LililoahidiwaMnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
Kuelekea mashariki ya vilima vya Yuda kuna Nyika la Yuda, pia huitwa Yeshimoni, ikimaanisha “jangwa.” (1 Samweli 23:19, NW, kielezi chini) Katika Bahari ya Chumvi, eneo hilo kame huonyesha mabonde yenye mawe na magenge yaliyochongoka-chongoka. Ikishuka meta 1,200 katika kilometa 24 tu, Nyika ya Yuda inakingwa dhidi ya pepo zenye mvua zinazotoka magharibi, na hivyo hupata kiasi kidogo cha mvua. Bila shaka hii ndiyo nyika ambayo mbuzi wa Azazeli alipelekwa wakati wa Siku ya Kufunika ya kila mwaka. Pia ndipo Daudi alipokimbilia alipokuwa akimtoroka Sauli. Hapo Yesu alifunga kwa siku 40 na baadaye akajaribiwa na Ibilisi.—Mambo ya Walawi 16:21, 22; Zaburi 63, linganisha maelezo ya utangulizi ya NW; Mathayo 4:1-11.
-
-
Masomo Yenye Kutumika Kutokana na Bara LililoahidiwaMnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 6]
Katika Nyika ya Yuda, Daudi alitafuta makimbilio alipokuwa akimtoroka Sauli. Baadaye Yesu alijaribiwa na Ibilisi hapo
[Hisani]
Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.
-