Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sifuni Yah kwa Hukumu Zake!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Acheni sisi tushangilie na tufurikwe na shangwe, na acheni sisi tumpe yeye utukufu, kwa sababu ndoa ya Mwana-Kondoo imewasili na mke wake amejitayarisha mwenyewe.

  • Sifuni Yah kwa Hukumu Zake!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Ufunuo 19:7,

  • Sifuni Yah kwa Hukumu Zake!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 15. Kutiwa muhuri hutukiaje, na ni jambo gani linalotakwa kwa Wakristo wapakwa-mafuta?

      15 Basi sasa, baada ya karibu miaka 2,000, wote 144,000 wa jamii ya bibi-arusi wamejiweka wenyewe tayari. Lakini ni kwenye pindi gani ya wakati inaweza kusemwa kwamba ‘mke wa Mwana-Kondoo amejitayarisha’? Kwa kuendelea, kutoka Pentekoste 33 W.K. wapakwa-mafuta wenye kuitikadi “walitiwa muhuri kwa roho takatifu iliyoahidiwa,” hii ni kwa kutazamia “siku ya kuachiliwa kupitia ukombozi” iliyokuwa ikija. Kama mtume Paulo alivyolisema jambo hilo, Mungu “pia ameweka muhuri wake juu yetu na ametupa sisi ishara ya kitakachokuja, yaani, roho, katika mioyo yetu.” (Waefeso 1:13; 4:30; 2 Wakorintho 1:22, NW) Kila Mkristo aliyepakwa mafuta ‘ameitwa na akachaguliwa,’ na amejithibitisha mwenyewe kuwa ‘mwaminifu.’—Ufunuo 17:14, NW.

      16. (a) Kutiwa muhuri kwa mtume Paulo kulitimilizwa wakati gani, na sisi tunajuaje? (b) Ni wakati gani mke wa Mwana-Kondoo atakuwa ‘amejitayarisha’ kikamili?

      16 Baada ya miongo ya mtihani, Paulo mwenyewe angeweza kujulisha wazi: “Mimi nimepiga vita njema, mimi nimekimbia mwendo hadi mwisho, mimi nimeshika imani. Kutoka wakati huu na kuendelea taji la uadilifu limehifadhiwa kwa ajili yangu mimi, ambalo Bwana, hakimu mwadilifu, atanipa mimi ikiwa thawabu katika siku hiyo, hata hivyo si mimi pekee, bali pia wale wote ambao wamependa udhihirisho wake.” (2 Timotheo 4:7, 8, NW) Kutiwa muhuri kwa mtume kunaonekana kulikuwa kumekamilika, hata ingawa alikuwa angali katika mnofu na bado angekabili ufia-imani. Hali moja na hiyo, wakati lazima uje ambao wale wote wanaobaki duniani wa wale 144,000 watakuwa wamekwisha kutiwa muhuri mmoja mmoja kuwa wao ni wa Yehova. (2 Timotheo 2:19) Huo utakuwa ndio wakati ambao mke wa Mwana-Kondoo atakuwa amekwisha jitayarisha kabisa—walio wengi sana wa 144,000 wakiwa wamekwisha pokea thawabu yao ya kimbingu na wale ambao wangali duniani wakiwa wamekwisha kukubaliwa mwishowe na kutiwa muhuri kuwa ni waaminifu.

      17. Ni lini ndoa ya Mwana-Kondoo inapoweza kutukia?

      17 Kufikia hapa katika jedwali ya wakati ya Yehova, wakati kutiwa muhuri kwa wale 144,000 kumefikia ukamilisho, malaika huachilia pepo nne za dhiki kubwa. (Ufunuo 7:1-3) Kwanza, hukumu inatekelezwa juu ya Babuloni Mkubwa aliye mithili ya kahaba. Kisha Kristo mwenye ushindi anasonga kwa haraka kwenye Har–Magedoni kuharibu sehemu inayobaki ya tengenezo la Shetani lililo duniani na, mwishowe, kutia Shetani na roho waovu wake ndani ya abiso. (Ufunuo 19:11–20:3) Ikiwa bado kuna wapakwa-mafuta wowote ambao wanaokoka wakiwa duniani, pasipo shaka wataingia ndani ya thawabu yao ya kimbingu upesi baada ya Kristo kukamilisha ushindi wake, wakajiunge na washiriki wenzao wa jamii ya bibi-arusi. Ndipo wakati uliowekwa na Mungu ufikapo, ndoa ya Mwana-Kondoo yaweza kutukia!

      18. Zaburi ya 45 huthibitishaje mfuatano wa matukio kwa habari ya ndoa ya Mwana-Kondoo?

      18 Simulizi la kiunabii katika Zaburi 45 (NW) linaeleza utaratibu wa matukio. Kwanza Mfalme aliyetawazwa apanda akawashinde maadui wake. (Mistari 1-7) Kisha ndoa yafanywa, bibi-arusi wa kimbingu akiwa anaandamana duniani na waandamani wake mabikira, umati mkubwa. (Mistari 8-15) Halafu ndoa yazaa matunda, aina ya binadamu iliyofufuliwa yainuliwa kwenye ukamilifu chini ya uangalizi wa “wana-wafalme katika dunia yote.” (Mistari 16, 17) Lo! ni baraka zilizoje zinazoandamana na ndoa ya Mwana-Kondoo!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki