-
Nilipata Majaribu Makali SanaMnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
-
-
Mateso Makali Yaanza
Mimi na ndugu wengine wawili tulikamatwa. Mke wangu hata hakunitembelea kwenye kituo cha polisi. Kwanza tulipelekwa hadi gereza moja huko Iráklion. Kama nilivyoeleza mwanzoni, nilihisi upweke na nilikuwa nimevunjika moyo. Nilikuwa nimemwacha mke mchanga asiyekubali imani yangu na watoto wawili wachanga. Nilimwomba Yehova msaada kwa bidii. Nikakumbuka maneno haya ya Mungu katika Waebrania 13:5: “Hakika sitakuacha kwa vyovyote wala kukuachilia mbali kwa vyovyote.” Nilitambua kwamba jambo la hekima ni kumtegemea Yehova kabisa.—Mithali 3:5.
-
-
Nilipata Majaribu Makali SanaMnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
-
-
Nilipokuwa uhamishoni niliendelea kumwandikia mke wangu mpendwa, lakini yeye hakuniandikia hata barua moja. Hata hivyo, niliendelea kumwandikia kwa upendo ili kumfariji na kumhakikishia kwamba hali hiyo ilikuwa ya muda tu na hatimaye tungeishi kwa furaha tena.
-
-
Nilipata Majaribu Makali SanaMnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
-
-
Baraka Isiyotarajiwa, Kisha Mateso Mengine
Mwishoni mwa mwaka 1950 niliachiliwa. Nilirudi nyumbani nikiwa mgonjwa na nimekonda sana, na sikujua kama ningekaribishwa. Nilifurahi sana kumwona mke wangu na watoto wangu tena! Na nilishangaa kuona kwamba uhasama wa Frosini ulikuwa umepunguka. Barua nilizoandika nikiwa gerezani zilikuwa na matokeo. Frosini alikuwa ameguswa na uvumilivu na ustahimilivu wangu. Muda mfupi baadaye nilikuwa na mazungumzo marefu pamoja naye yaliyotupatanisha. Alikubali kujifunza Biblia na kumwamini Yehova na ahadi zake. Mojawapo ya siku zenye furaha zaidi maishani mwangu ilikuwa siku moja mwaka wa 1952 nilipombatiza Forsini aliyekuwa amejiweka wakfu kwa Yehova!
-