Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutumia Maneno Yanayofaa
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Kutumia Semi Tofauti-Tofauti na Sahihi. Kuna maneno mazuri tele ya kutumia. Tumia semi tofauti-tofauti badala ya kutumia semi zilezile katika kila hali. Ukifanya hivyo, maneno yako yatapendeza na kujaa maana. Unawezaje kuongeza misamiati?

      Unaposoma, tia alama maneno ambayo huelewi vizuri kisha uyachunguze katika kamusi. Chagua maneno machache kati ya yale ambayo huelewi vizuri na ujitahidi kuyatumia unapopata nafasi. Yatamke vizuri na uyatumie kwa njia ambayo yanaeleweka kwa urahisi na wala si kwa kujielekezea tu fikira. Kuongeza misamiati kutakuwezesha kutumia semi tofauti-tofauti. Lakini jihadhari kwa sababu mtu anapotamka maneno vibaya au anapoyatumia vibaya, wengine watadhani kwamba hajui analosema.

      Kusudi la kuongeza misamiati ni kuweza kuwasiliana, wala si kujitukuza. Maneno yanayotatanisha na maneno marefu huelekeza fikira kwa msemaji. Tunapaswa kuwa na hamu ya kuwaeleza wengine habari muhimu na kufanya ipendeze wasikilizaji. Kumbuka ile mithali ya Biblia isemayo hivi: “Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri.” (Mit. 15:2) Kutumia maneno mazuri, yanayofaa na kueleweka kwa urahisi, hufanya maneno yetu yafurahishe na kuchochea badala ya kuwa yenye kuchosha na yasiyopendeza.

      Unapoongeza misamiati, fikiria sana kutumia maneno yanayofaa. Maneno mawili yanaweza kuwa na maana moja lakini yatofautiane kidogo yakitumiwa katika hali tofauti. Ukitambua jambo hilo, unaweza kufanya usemi wako uwe wazi zaidi na kuepuka kuudhi wasikilizaji. Wasikilize kwa makini watu wanaoongea vizuri. Kuna kamusi ambazo huorodhesha kila neno na visawe vyake (maneno tofauti yanayokaribiana sana katika maana) na pia vitabu ambavyo vinaonyesha maneno ya kinyume. Kwa njia hiyo, mbali na kupata maneno tofauti-tofauti yanayofafanua wazo lilelile, pia unapata maana tofauti ndogo-ndogo ya wazo hilo. Jambo hilo linasaidia sana unapotafuta neno linalofaa hali fulani. Lakini, kabla ya kuanza kutumia neno jipya, hakikisha unafahamu maana yake, matamshi yake, na jinsi linavyotumiwa.

  • Kutumia Maneno Yanayofaa
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Maneno Yanayoonyesha Mkazo, Hisia, na Yanayovutia. Unapoongeza misamiati, mbali na kufikiria maneno mapya fikiria pia maneno yenye miundo fulani hususa. Kwa mfano, fikiria vitenzi vinavyotia mkazo; vivumishi vinavyopendeza; na maneno yanayoonyesha uchangamfu, fadhili, au bidii.

      Biblia imejaa mifano ya lugha iliyojaa maana. Kupitia nabii Amosi, Yehova alihimiza hivi: “Tafuteni mema, na wala si mabaya . . . Yachukieni mabaya; yapendeni mema.” (Amo. 5:14, 15, italiki ni zetu.) Nabii Samweli alimtangazia Mfalme Sauli hivi: “Leo, BWANA amekurarulia ufalme wa Israeli.” (1 Sam. 15:28, italiki ni zetu.) Yehova alitumia maneno yasiyoweza kusahaulika kwa urahisi alipokuwa akizungumza na Ezekieli: “Nyumba yote ya Israeli wana vipaji vigumu, na mioyo yenye ukaidi.” (Eze. 3:7, italiki ni zetu.) Yehova alikazia uzito wa makosa ya Israeli kwa kuuliza hivi: “Je! mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi.” (Mal. 3:8, italiki ni zetu.) Danieli alipokuwa akieleza juu ya jaribu la imani kule Babiloni, alikoleza usemi wake aliposema kwamba ‘Nebukadreza alijaa ghadhabu’ kwa sababu Shadraka, Meshaki, na Abednego walikataa kuabudu sanamu yake, akaamuru wafungwe na kutupwa ndani ya “tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.” Danieli anatusaidia kufahamu ukali wa moto ule anaposema kwamba mfalme aliamuru watu wake “watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto,” ikawa moto hivi kwamba watu wa mfalme wakafa walipoikaribia tanuru hiyo. (Dan. 3:19-22, italiki ni zetu.) Yesu alipozungumza na watu wa Yerusalemu siku chache kabla ya kifo chake, alisema hivi kwa hisia nyingi: “Ni mara nyingi kadiri gani nilitaka kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku hukusanya vifaranga vyake pamoja chini ya mabawa yake! Lakini nyinyi watu hamkutaka hilo. Tazameni! Nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.”—Mt. 23:37, 38.

      Maneno ambayo yamechaguliwa vizuri yanaweza kutokeza picha dhahiri akilini mwa wasikilizaji. Ukitumia maneno yanayogusa hisia, ni kana kwamba wasikilizaji wanaona na kugusa mambo unayosema, wanaonja na kunusa vyakula unavyotaja, na kusikia sauti unazofafanua na watu unaonukuu. Wasikilizaji watakusikiliza kwa makini kwa sababu unafanya mambo yawe halisi.

      Maneno yanayotokeza mambo kwa njia dhahiri yanaweza kufanya watu wacheke au walie. Yanaweza kumpa mtu tumaini, na kumfanya aliyeshuka moyo awe na hamu ya kuishi na kumchochea ampende Muumba. Watu ulimwenguni kote wamevutiwa sana na tumaini linalotokezwa na maandiko ya Biblia kama Zaburi 37:10, 11, 34; Yohana 3:16; na Ufunuo 21:4, 5.

      Unaposoma Biblia pamoja na vichapo vya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” utaona unamna-namna wa maneno. (Mt. 24:45) Usiyasome tu na kuyasahau. Chagua yale yanayokufurahisha, uyaongeze kwenye msamiati wako.

  • Kutumia Maneno Yanayofaa
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • MAZOEZI: Unapotayarisha Funzo la Mnara wa Mlinzi au Funzo la Kitabu la Kutaniko juma hili, chagua maneno machache ambayo huwezi kuyafafanua vizuri. Yatafute katika kamusi ikiwa inapatikana, au jadiliana maana yake na mtu ambaye anafahamu maneno vizuri.

      Misamiati ninayotaka kutumia

      Ili nisitumie maneno yaleyale na ili niwe sahihi Ili kuonyesha mkazo, hisia, au usemi unaopendeza

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki