-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kusanyiko la kimataifa la mwaka wa 1965 lenye kichwa “Neno la Kweli” lililofanywa katika uwanja wa michezo wa Ullevål, jijini Oslo lilikuwa la pekee sana. Hata hivyo, kulikuwa na tatizo fulani. Timu ya kandanda ya Norway ilikuwa icheze na timu nyingine ya kitaifa katika uwanja huohuo jioni iliyotangulia programu. Umati wa Mashahidi ulisubiri nje ya malango hadi mashabiki wa kandanda walipoondoka, kisha wakaingia ili kutayarisha uwanja huo kwa ajili ya kusanyiko. Walifanya kazi usiku kucha wakisafisha, kuondoa taka, na kujenga mahema ya vyakula. Pia, walijenga majukwaa, kibanda cha muziki, na kwa ajili ya mapambo, wakajenga bohari, na vibanda vingine vitatu, vyote vikiwa na paa za nyasi. Gazeti la Dagbladet lilisema: “Muujiza wakati wa usiku. Uwanja wa michezo wa Ullevål umebadilishwa na kuwa mahali patulivu penye kuvutia . . . Bidii yenye kustaajabisha ya Mashahidi wa Yehova.”
Akina ndugu na dada wa Norway waliwakaribisha manyumbani mwao wajumbe zaidi ya 7,000, wengi wao kutoka nchi ya Denmark. Mahema yalijengwa katika uwanja fulani nje ya jiji. Yalifaa hali ya hewa ilipokuwa nzuri. Hata hivyo, wajumbe 6,000 waliokaa katika mahema hayo hawatasahau kamwe mvua iliyonyesha na kufanya uwanja huo ujae matope siku za kwanza za kusanyiko hilo. Kila mtu alifurahi hali ya hewa ilipobadilika siku mbili za mwisho. Licha ya hali mbaya ya hewa, wenyeji na wageni walifurahia ushirika wa Kikristo, na programu hiyo ya wakati unaofaa iliwaburudisha. Walishangilia sana kuona watu 199 wakibatizwa, na kilele cha wahudhuriaji 12,332 wakati wa hotuba ya watu wote iliyotolewa na Ndugu Knorr!
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 138]
Kambi ya mahema kwa ajili ya kusanyiko la kimataifa lenye kichwa “Neno la Kweli”
-