Ukurasa wenye Kichwa/Habari za Wachapishaji
2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Kina Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2007
Kitabu hiki ni cha ․․․․․․․․․․․․․․․․․
“Simameni imara muuone wokovu wa Yehova.”—KUT. 14:13.
Ilionekana kana kwamba hakukuwa na matumaini yoyote. Wanaume, wanawake, na watoto elfu tatu hivi walikuwa wamenaswa kwenye ufuo wa magharibi wa Bahari Nyekundu! Akiwa amekasirika na kuaibishwa na yale Mapigo Kumi ambayo Yehova alileta juu ya Misri, Farao na majeshi yake walisonga mbele kwa kasi kama simba wenye njaa waliokuwa tayari kuruka na kushika windo dhaifu. Waisraeli waliogopa sana. “Msiogope,” Musa akapaaza sauti, “simameni imara muuone wokovu wa Yehova . . . Yehova mwenyewe atawapigania ninyi.”—Kut. 14:13, 14.
Akionyesha nguvu zake kwa njia yenye kustaajabisha, Yehova aliwakomboa watu wake kwa kugawanya maji ya Bahari Nyekundu. Yehova amewaokoa watu wake mara nyingi katika hali ambazo kwa maoni ya wanadamu haingewezekana kuwaokoa. Leo, Yehova anaendelea kupigania watumishi wake, kama utakavyoona katika mambo mengi yaliyoonwa yaliyo katika kitabu hiki cha mwaka. Andiko la mwaka wa 2008, ambalo limenukuliwa hapo juu, na liimarishe imani yako katika ahadi zote za Yehova na kutia nguvu tegemeo lako katika mwelekezo wake wenye upendo.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 2]
Photo Credits: Page 66: Chukchi: © B&C Alexander/Arcticphoto.com; page 254: Sunset: Photo: www.comstock.com