-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Ndugu walifurahi sana kupanga makusanyiko ya mzunguko huku wakilindwa na sheria! Jumla ya watu 11,214 walihudhuria makusanyiko ya kwanza 11 na 465 wakabatizwa.
Makanisa yalikerwa mno na makusanyiko hayo. Makasisi walifanya juu chini kuwazuia Mashahidi wa Yehova wasiandikishwe kisheria katika eneo hilo lenye watu wengi wanaopendezwa, ambalo waliliona kuwa eneo lao. Huko Gandajika katika Jimbo la Kasai, viongozi wa kidini walipeleka malalamiko kwa meya. Walipoona meya haogopi vitisho vyao, walituma vijana kuvuruga kusanyiko. Hata hivyo, sinema ya Biblia ilikuwa ikionyeshwa kwenye kusanyiko wakati huo, na umati mkubwa ulikuwa umekuja kuitazama. Vijana hao wenye fujo walipofika hapo, walitulia na kuanza kuitazama pia. Sinema hiyo iliwavutia sana. Kila mara ukanda wa sinema ulipobadilishwa, umati wa maelfu ya watu ulipaaza sauti hivi: “Mashahidi wa Yehova na waishi milele!”
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Kusafiri ili Kutumikia Kwenye Makusanyiko ya Mzunguko
Katika mwaka wa 1964, kulikuwa na mizunguko ya kutosha kuunda wilaya mbili nchini Kongo. Wilaya ya tatu ilianzishwa mwaka wa 1969 huko Kasai, na kufikia mwaka wa 1970, kulikuwa na wilaya nne. Kwa sababu ya barabara mbovu, mara nyingi ilikuwa vigumu kwa waangalizi wa wilaya na wengine kufika kwenye makusanyiko. Hebu tuandamane na mwangalizi wa wilaya, William Smith anapoenda kwenye kusanyiko la mzunguko.
“Mito ilifurika baada ya mvua kubwa sana kunyesha sehemu za mashambani. Tulikuwa tukienda Kamina kuhudhuria kusanyiko la mzunguko. Tulisafiri zaidi ya kilometa 320 ili kufika huko. Mvua hiyo kubwa iligeuza barabara fulani kuwa madimbwi ya matope, na katika sehemu nyingine maji yalifurika kabisa barabarani. Bonde moja liligeuka kuwa ziwa. Magari ya watu na ya serikali, na malori yalisimama kila mahali huku watu wakingoja maji yapungue. Wengi walitarajia safari yao kuchelewa kwa majuma mawili.
“Nilijua kwamba ndugu walikuwa wakingoja kwa hamu kusanyiko la mzunguko. Baadhi yao walitembea kwa siku kadhaa ili kuhudhuria. Niliuliza kama kuna barabara nyingine ya kuvuka bonde hilo. Nilishangaa watu waliponiambia kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa wametengeneza barabara ndogo, lakini kwa sababu udongo ulikuwa umelowa chepechepe, hawangemruhusu mtu yeyote kuitumia hadi mwangalizi wa wilaya apite kwanza na kwenda Kamina.
“Ndugu kutoka vijiji viwili walifanya kazi siku nzima, usiku kucha, na siku iliyofuata ili kutengeneza barabara mpya kuzunguka sehemu isiyopitika. Muda si muda nilifika mahali hapo na nikajitayarisha kuendesha gari langu aina ya jeep kwenye barabara waliyotengeneza. Umati mkubwa ulikuwa umekusanyika ili kuona kama gari langu lingepita. Baada ya gari hilo kwenda kwa umbali wa meta chache tu kwenye barabara hiyo mpya, tulivunjika moyo sana kuona likizama kwenye udongo uliolowa maji!
“Ndugu walilisukuma, lakini halikusogea hata kidogo. Walikuwa wamejikakamua sana, na nyuso zao zilionyesha kwamba wamekata tamaa. Hata hivyo, bado waliazimia kufanya yote wawezayo ili mwangalizi wa wilaya afike kwenye kusanyiko. Watazamaji walirudi kwenye magari yao, wakidhani kwamba barabara hiyo mpya ilikuwa balaa tupu. Ndugu waliamua kujaribu tena. Sasa walitoa kila kitu kwenye gari hilo ambalo lilikuwa limebeba vichapo, vifaa vya sauti, jenereta, na vitu vingine. Walichimba barabara na kulisukuma gari, na likaanza kusogea polepole huku magurudumu yakizunguka kwa kasi.
“Baada ya muda wa saa moja, kulikuwa na shangwe na vigelegele na nyimbo za Ufalme tulipofaulu kupita kwenye matope hayo. Ndugu walitimiza kile ambacho watu walioketi kwenye magari walidhani hakiwezekani. Kusanyiko lilifanikiwa kwa sababu ya jitihada za akina ndugu. Yehova alikuwa pamoja na watu wake na aliwasaidia kufanya mapenzi yake.”
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
[Picha katika ukurasa wa 208]
Kusanyiko huko Kolwezi, 1967
-