-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Happy Chisenga alipojitolea kuwa painia wa kawaida katika Mkoa wa Kati huko Zambia, alishangaa kupokea barua iliyomwomba atumike katika eneo la mbali karibu na Njombe, Tanzania. “Mimi na mke wangu tuliposoma neno ‘mbali,’ tulidhani kwamba tungeshirikiana na wahubiri fulani katika eneo la mbali. Muda mfupi baadaye tulitambua kwamba sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuhubiri kwenye eneo hilo. Watu walivutiwa tulipowaonyesha katika Biblia zao wenyewe jina Yehova, au maneno kama vile Har–Magedoni. Muda si muda, walianza kuniita Yehova na kumwita mke wangu Har–Magedoni. Baadaye tulipohamia Arusha, tuliwaacha wahubiri kadhaa thabiti katika eneo hilo.”
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha]
Happy Mwaba Chisenga
-