-
Wamejitolea Kufuata Njia ya Mungu ya MaishaMnara wa Mlinzi—1999 | Januari 15
-
-
Hotuba ya mwisho siku hiyo ilikuwa na kichwa “Utu wa Muumba na Njia Zake.” Baada ya kutaja kwamba mabilioni ya watu hawamjui Muumba, msemaji alisema: “Kusudi halisi maishani lahusu kumjua Muumba, Mungu wetu halisi; kutambua utu wake; na kushirikiana na njia zake. . . . Kuna mambo yanayohusu ulimwengu wetu na yanayotuhusu ambayo unaweza kutumia kusaidia watu wamkubali Muumba na kupata umaana kuhusiana naye.” Ndipo msemaji akazungumzia uthibitisho wa kuwepo kwa Muumba mwenye hekima na upendo. Kilele cha hotuba hiyo kilikuwa kutolewa kwa kitabu kipya—Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Wamejitolea Kufuata Njia ya Mungu ya MaishaMnara wa Mlinzi—1999 | Januari 15
-
-
Je, Kuna Muumba Anayekujali?
Kitabu kipya chenye kichwa hicho hutoa uthibitisho wenye kusadikisha wa kuwepo kwa Muumba, Yehova, na chazungumzia sifa zake. Kimekusudiwa hasa wale wenye elimu nzuri ya kilimwengu lakini hawamwamini Mungu. Pia, kitabu hiki chenye kurasa 192 kitakuza imani ya watu mmoja-mmoja ambao tayari wanamwamini Mungu, kikijenga uthamini kwa utu na njia zake.
Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? hakiamui kimbele kuwa msomaji ana imani katika Mungu. Badala ya hivyo, kinachunguza namna mawazo na mavumbuzi ya hivi majuzi ya kisayansi hushuhudia kuwepo kwa Muumba. Baadhi ya sura ni zile zenye vichwa “Ni Nini Kinachoweza Kufanya Maisha Yako Yawe na Maana Zaidi?,” “Ulimwengu Wetu Ulitokeaje?—Ubishi Uliopo,” na “Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!” Sura nyingine zazungumza juu ya kwa nini twaweza kuwa na uhakika kwamba Biblia imepuliziwa kimungu. Kitabu hicho kipya pia chatupatia maoni ya jumla kuhusu Biblia, ambayo hufunua utu na njia za Muumba. Kitabu hicho hakielezei tu kwa nini Mungu ameruhusu kuteseka bali pia chaeleza jinsi ambavyo atakomesha kuteseka milele.
-