-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
21. Ni mbingu mpya zipi zilizotokea mwaka wa 1914?
21 Hata hivyo, kumbuka kwamba Petro alirudia maneno ya unabii wa Isaya akaonyesha kwamba ungetimizwa wakati ujao. Mtume huyo aliandika hivi: “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13) Mwaka wa 1914 zile mbingu mpya zilizokuwa zimengojewa sana zilitokea. Ufalme wa Kimesiya uliozaliwa mwaka huo unatawala kutoka mbinguni kwenyewe, na Yehova ameupa ufalme huo mamlaka ya kuitawala dunia yote. (Zaburi 2:6-8) Serikali hiyo ya Ufalme, iliyo chini ya Kristo na watawala wenzake 144,000, ndio mbingu mpya.—Ufunuo 14:1.
22. Dunia mpya itafanyizwa kwa watu gani, na watu wanatayarishwaje hata sasa ili wawe kiini cha mpango huo?
22 Namna gani dunia mpya? Kwa kufuata kielelezo cha utimizo wa kale, dunia mpya itafanyizwa kwa watu wanaofurahia kujitiisha chini ya utawala wa serikali mpya ya kimbingu. Hata sasa, mamilioni ya watu mmoja-mmoja wenye mwelekeo unaofaa wananyenyekea chini ya serikali hiyo na kujitahidi kufuata sheria zake zilizo katika Biblia. Wanatoka katika taifa zote, lugha zote, na jamii zote, nao hushirikiana kumtumikia Mfalme Yesu Kristo anayetawala. (Mika 4:1-4) Mfumo mwovu wa mambo uliopo ukiisha kupita, kikundi hicho ndicho kitakachofanyizwa kuwa kiini cha dunia mpya na hatimaye kiwe jamii ya wanadamu wenye kumhofu Mungu watakaokuwa kila mahali ulimwenguni, wakiwa warithi wa makao ya kidunia ya Ufalme wa Mungu.—Mathayo 25:34.
23. Ni habari zipi tunazozipata katika kitabu cha Ufunuo kuhusu “mbingu mpya na dunia mpya,” na unabii huo utatimizwaje?
23 Kitabu cha Ufunuo kinaelezea njozi ambayo mtume Yohana aliona kuhusu siku ya Yehova inayokuja, wakati ambao mfumo huu wa mambo utaondolewa. Halafu Shetani atafungwa ndani ya abiso. (Ufunuo 19:11–20:3) Baada ya maelezo hayo, Yohana anayarudia maneno ya kiunabii ya Isaya, akiandika hivi: “Nikaona mbingu mpya na dunia mpya.” Mistari inayofuata ya masimulizi ya njozi hii tukufu inaeleza juu ya wakati ambao Yehova Mungu atabadili kabisa hali za dunia hii ziwe nzuri zaidi. (Ufunuo 21:1, 3-5) Ni wazi kwamba ahadi ya Isaya ya “mbingu mpya na dunia mpya” itatimizwa vizuri ajabu katika ulimwengu mpya wa Mungu! Jamii mpya ya kidunia itafurahia paradiso ya kiroho na hata ya kihalisi, ikiwa chini ya mbingu mpya za kiserikali. Ile ahadi ya kwamba “maneno ya kwanza [magonjwa, mateso, na ole mwingine mwingi unaopata wanadamu] hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni” inafariji kweli kweli. Ikiwa wakati huo tutakumbuka jambo lolote lile, halitatutia madhara wala maumivu yanayolemea mioyo ya wengi wakati wa sasa.
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Kupitia Isaya, Yehova anasema hivi: “Tazama, mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya, na maneno ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.” (Isaya 65:17, “Zaire Swahili Bible”)
-