-
Nuru kwa MataifaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ukusanyaji Waendelea
16, 17. Ni nani wale wanaoitwa “uzao wenu” baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?
16 Idadi kamili ya huo “ukuhani wa kifalme” ni 144,000, na baada ya muda, kazi ya kuwakusanya ilimalizika. (Ufunuo 7:1-8; 14:1) Je, huo ulikuwa mwisho wa kazi ya kukusanya? Sivyo. Unabii wa Isaya unaendelea kusema hivi: “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema BWANA, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.” (Isaya 66:22)
-
-
Nuru kwa MataifaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hata hivyo, unabii huo umekuwa na utimizo wenye kutokeza sana katika siku zetu.
17 “Uzao” ambao taifa la ndugu za kiroho wanautokeza ni “umati mkubwa,” walio na tumaini la uhai wa milele duniani. Wao ‘hutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha,’ na husimama “mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.” “Wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 7:9-14; 22:17) Leo wale walio “umati mkubwa” wanaepuka giza la kiroho na kuja kwenye nuru ambayo Yehova huandaa. Wanaonyesha imani katika Yesu Kristo, na wanajitahidi kubaki wakiwa safi kiroho na kiadili kama ndugu na dada zao watiwa-mafuta. Wakiwa kikundi, wanaendelea kutumikia chini ya mwelekezo wa Kristo na ‘watakaa’ milele!—Zaburi 37:11, 29.
-