-
Kukusanyika Kwenye “Kitovu cha Ulimwengu”Mnara wa Mlinzi—2004 | Februari 15
-
-
Mwanamke mmoja mzee mwenye wana na mabinti wanane aliwaambia Mashahidi kwamba hangeweza kuzungumza nao kwa sababu alikuwa Mkatoliki. Baada ya kumwambia kwamba walitaka kuzungumza naye kuhusu matatizo yanayokabili kila mtu, kama vile matumizi ya dawa za kulevya na matatizo ya kifamilia, alikubali kuwasikiliza.
Mwanamke mmoja mzee mwenyeji aliwakaribisha kwa ubaridi mume na mke Mashahidi. Aliwaambia waende wakazungumze na watu kwenye bara ambao ni wakatili sana. Mashahidi hao walimwambia kwamba ujumbe wa “habari njema ya ufalme” unatolewa kwa wote na kwamba kusudi lao la kuja katika kisiwa hicho lilikuwa kuhudhuria kusanyiko ambalo lingewasaidia wote wampende Mungu zaidi. (Mathayo 24:14) Walimwuliza kama angefurahia maisha marefu katika hali za kiparadiso, zinazofanana na za kisiwa hicho lakini bila magonjwa na kifo. Baada ya Mashahidi hao kujadiliana naye kuhusu miaka ambayo mashimo ya volkeno yamekuwako, alitafakari kuhusu ufupi wa maisha kisha akauliza: “Kwa nini tunaishi kwa muda mfupi tu?”Alishangaa aliposoma Zaburi 90:10.
Ndipo Mashahidi hao wakasikia kelele kutoka katika nyumba jirani. Ingawa hawakuelewa kelele hizo, mwanamke huyo aliwaambia kwamba majirani walikuwa wakitoa matusi na kusema wazi kwamba hawakutaka kutembelewa na Mashahidi. Hata hivyo, mwanamke huyo alikuwa nua, au binti mkubwa katika familia hiyo. Tangu baba yake afe, alikuwa na daraka la kuamulia familia hiyo mambo yenye manufaa kwao. Aliwatetea Mashahidi hao mbele ya jamaa zake katika lugha yake ya asili na kukubali kwa upole vichapo alivyopewa. Baadaye juma hilo, alipokuwa akipita barabara fulani, aliwaona Mashahidi na kumwambia ndugu yake asimamishe gari. Ingawa ilikuwa wazi kwamba ndugu yake alikasirika, mwanamke huyo aliwaaga ndugu hao na kuwatakia mema katika huduma yao.
-
-
Kukusanyika Kwenye “Kitovu cha Ulimwengu”Mnara wa Mlinzi—2004 | Februari 15
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 24]
Kuhubiri Katika Kisiwa cha Easter
Miaka miwili hivi kabla ya kusanyiko hilo lisilosahaulika, mwangalizi mmoja wa mzunguko na mke wake walitembelea kisiwa hicho na kujionea mambo mengi yenye kupendeza. Kwa mfano, wazia jinsi walivyoshangaa wakati dada mmoja aliyewapeleka mahali pa kulala alipowakumbusha kwamba walijifunza Biblia pamoja naye akiwa tineja huko kusini mwa Chile, miaka 16 hivi iliyopita. Baadaye, mbegu hiyo ilizaa matunda huko Rapa Nui.
Pia walijionea jambo hili lenye kuchekesha: Mwenye duka la bidhaa za kumbukumbu alikubali Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya pamoja na kitabu cha kujifunzia Biblia, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, ambavyo vinachapishwa na Mashahidi wa Yehova. Walipomrudia aliwaambia kwamba hangeweza kusoma Biblia hiyo. Walikuwa wamemwachia Biblia ya Kifaransa wala si ya Kihispania! Tatizo hilo lilitatuliwa haraka, na kwa msaada wa Mashahidi wenyeji, na bila shaka kwa kutumia Biblia katika lugha yake mwenyewe, akatambua kwamba haikuwa vigumu kuielewa Biblia.
-