-
Walimu wa Neno la Mungu Wahimizwa Watimize Kazi YaoMnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
-
-
Jambo jingine kuu la mkusanyiko lilikuwa drama iliyoigizwa na watu waliovalia mavazi maalum “Heshimu Mamlaka ya Yehova,” iliyoonyesha wana wa Kora. Licha ya baba yao kumwasi Musa na Aroni, wao walidumisha uaminifu kwa Yehova na wawakilishi wake. Ingawa Kora na wafuasi wake waliangamia, wana wake waliokoka. Hotuba iliyofuata “Nyenyekea kwa Uaminifu Mamlaka ya Kimungu,” ilionyesha jinsi kila mmoja wetu anavyoweza kutumia habari zilizokuwa katika drama. Msemaji alitoa onyo kuhusu sehemu sita ambazo Kora na wafuasi wake walipungukiwa: hawakuunga mkono kwa uaminifu mamlaka ya Yehova; waliruhusu kiburi, kujitakia makuu, na wivu uwashinde; walikazia fikira hali za kutokamilika za wale walioteuliwa na Yehova; walisitawisha mtazamo wa kulalamika; hawakutosheka na mapendeleo yao ya utumishi; na wakaruhusu urafiki au uhusiano wa familia utangulie uaminifu kwa Yehova.
-
-
Walimu wa Neno la Mungu Wahimizwa Watimize Kazi YaoMnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 29]
Wahudhuriaji walichochewa na drama yenye kichwa “Heshimu Mamlaka ya Yehova”
-