Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kondoo Wengine na Agano Jipya
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
    • Katika ono hilohilo, Yohana aliona “umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha . . . , [waki]lia kwa sauti kubwa, wakisema: ‘Sisi tunawiwa wokovu na Mungu wetu, aketiye juu ya hicho kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.’” (Ufunuo 7:9, 10) Katika kusema, ‘Sisi tunawiwa wokovu na Mwana-Kondoo,’ umati mkubwa waonyesha kwamba wao pia hubarikiwa kwa njia ya Mbegu ya Abrahamu.

      2. Umati mkubwa ulitokea wakati gani, na huo watambulishwaje?

      2 Umati huo mkubwa ulitambuliwa huko nyuma mwaka wa 1935, na leo idadi yake ni watu zaidi ya milioni tano. Ukiwa umeteuliwa kuokoka dhiki kubwa, washiriki wake watawekwa kando kwa ajili ya uhai udumuo milele Yesu agawanyapo “kondoo” na “mbuzi.” Wakristo wa umati mkubwa wamo miongoni mwa “kondoo wengine” katika kielezi cha Yesu cha mazizi ya kondoo. Wao hutumaini kuishi milele katika dunia iliyo paradiso.—Mathayo 25:31-46; Yohana 10:16; Ufunuo 21:3, 4.

  • Kondoo Wengine na Agano Jipya
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
    • Washiriki wa umati mkubwa si washiriki katika agano jipya. Hata hivyo, wao hushirikiana na Israeli wa Mungu na huishi pamoja nao katika “nchi” yao. (Isaya 66:8) Kwa hiyo ni jambo la akili kusema kwamba wao pia huja chini ya fadhili isiyostahiliwa ya Yehova na chini ya sheria kuelekea Kristo. Ingawa si washiriki katika agano jipya, wao hunufaika nalo.

  • Kondoo Wengine na Agano Jipya
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
    • “Wageni” na “Israeli wa Mungu”

      4, 5. (a) Kulingana na Isaya ni kikundi kipi ambacho kingemhudumu Yehova? (b) Isaya 56:6, 7 hutimizwaje juu ya umati mkubwa?

      4 Nabii Isaya aliandika hivi: “Wageni, walioandamana na BWANA ili wamhudumu, na kulipenda jina la BWANA, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu.” (Isaya 56:6, 7) Katika Israeli, hili lilimaanisha kwamba “wageni,” watu wasio Waisraeli, wangemwabudu Yehova—wakilipenda jina lake, wakitii masharti ya agano la Sheria, wakishika Sabato, na kutoa dhabihu kwenye hekalu, “nyumba ya sala” ya Mungu.—Mathayo 21:13.

      5 Katika siku yetu, ‘wageni ambao wameandamana na BWANA’ ni ule umati mkubwa. Hao humhudumu Yehova kwa ushirikiano na Israeli wa Mungu. (Zekaria 8:23) Wao hutoa dhabihu zilezile zenye kukubalika watoazo Israeli wa Mungu. (Waebrania 13:15, 16) Wao huabudu katika hekalu la Mungu la kiroho, “nyumba [yake] ya sala.” (Linganisha Ufunuo 7:15.) Je, wao hushika Sabato ya kila juma? Wala watiwa-mafuta wala kondoo wengine hawaamuriwi kufanya hivyo. (Wakolosai 2:16, 17) Hata hivyo, Paulo aliwaambia Wakristo watiwa-mafuta Waebrania hivi: “Kumebaki pumziko la sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana mtu ambaye ameingia ndani ya pumziko la Mungu amepumzika pia mwenyewe kutokana na kazi zake mwenyewe, kama vile Mungu alivyofanya kutokana na zake mwenyewe.” (Waebrania 4:9, 10) Waebrania hao waliingia katika “pumziko la sabato” walipojitiisha kwa “uadilifu wa Mungu” na kupumzika kutoka hali ya kujaribu kujitetea kwa kazi za Sheria. (Waroma 10:3, 4) Wakristo watiwa-mafuta Wasio Wayahudi huonea shangwe pumziko lilelile kwa kujitiisha kwa uadilifu wa Yehova. Umati mkubwa hujiunga nao katika pumziko hilo.

      6. Kondoo wengine leo hujiwekaje chini ya agano jipya?

      6 Zaidi, kondoo wengine hujiweka chini ya agano jipya kama vile wageni wa zamani walivyojiweka chini ya agano la Sheria. Katika njia gani? Si kwa kuwa washiriki katika hilo bali kwa kujinyenyekeza kwa sheria zinazoshirikishwa nalo na kunufaika kutokana na mipango yake. (Linganisha Yeremia 31:33, 34.) Kama waandamani wao watiwa-mafuta, kondoo wengine wana sheria ya Yehova ikiwa imeandikwa ‘katika moyo wao.’ Wao huzipenda sana na kuzitii amri na kanuni za Yehova. (Zaburi 37:31; 119:97) Kama Wakristo watiwa-mafuta, wao wamjua Yehova. (Yohana 17:3) Vipi juu ya tohara? Miaka ipatayo 1,500 kabla ya kufanywa kwa agano jipya, Musa aliwahimiza Waisraeli hivi: “Zitahirini govi za mioyo yenu.” (Kumbukumbu la Torati 10:16; Yeremia 4:4) Ingawa tohara ya kimwili ya lazima ilipitilia mbali pamoja na Sheria, watiwa-mafuta na pia kondoo wengine lazima ‘watahiri’ mioyo yao. (Wakolosai 2:11) Mwishowe, Yehova husamehe kosa la kondoo wengine kwa msingi wa “damu [ya Yesu] ya agano” iliyomwagwa. (Mathayo 26:28; 1 Yohana 1:9; 2:2) Mungu hawafanyi kuwa wana wa kiroho, kama vile ambavyo huwafanya wale 144,000. Lakini yeye huwatangaza kondoo wengine kuwa waadilifu, katika maana ambayo Abrahamu alitangazwa kuwa mwadilifu akiwa rafiki ya Mungu.—Mathayo 25:46; Waroma 4:2, 3; Yakobo 2:23.

      7. Ni tazamio gani liwezekanalo kwa ajili ya kondoo wengine leo, ambao hutangazwa kuwa waadilifu kama vile Abrahamu?

      7 Kwa wale 144,000, kutangazwa kuwa waadilifu huwafungulia njia kulikubali tumaini la kutawala na Yesu katika Ufalme wa kimbingu. (Waroma 8:16, 17; Wagalatia 2:16) Kwa kondoo wengine, kutangazwa kuwa waadilifu wakiwa rafiki za Mungu huwawezesha kuwa na tumaini la uhai udumuo milele katika dunia iliyo paradiso—ama kwa kuokoka Har–Magedoni wakiwa sehemu ya umati mkubwa ama kupitia “ufufuo wa waadilifu.” (Matendo 24:15) Ni pendeleo lililoje kuwa na tumaini la namna hiyo na kuwa rafiki ya Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima, kuwa “mgeni-mwalikwa katika hema [lake]”! (Zaburi 15:1, 2, NW) Ndiyo, watiwa-mafuta na kondoo wengine hubarikiwa katika njia ya ajabu kupitia Yesu, Mbegu ya Abrahamu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki