Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kwa kuwa kuna upungufu wa ndugu waliowekwa rasmi, makutaniko fulani hayawezi kuwa na hotuba ya watu wote kila juma. Hata hivyo, kama ndugu na dada zao wa mji wa Peć, wanakutana kwa uaminifu kila juma kwa ajili ya Funzo la Mnara wa Mlinzi na mikutano mingine ya kutaniko.

  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kwa muda mrefu, Mashahidi wengi wa Yehova nchini Kosovo walikuwa Waserbia, kwa hiyo mikutano ilifanywa katika Kiserbia, na ndugu walifurahi kuwasaidia watu waliozungumza Kialbania kuelewa mikutano. Sasa hali imebadilika. Ndugu wengi nchini Kosovo ni Waalbania. Makutaniko yote yanatumia Kialbania isipokuwa kutaniko moja ndilo linalotumia Kiserbia, na ndugu wanafurahi kutafsiri hotuba ili ndugu Waserbia waelewe mikutano. Makusanyiko yote yanafanywa katika lugha zote mbili. Kwa mfano, programu yote ya kusanyiko la wilaya la 2008 ilifanywa katika Kialbania na ikatafsiriwa katika Kiserbia, na hotuba kuu zilitolewa katika Kiserbia na wazee wa Kosovo. Ndugu mmoja anaeleza hivi: “Ingawa watu wengine wanachukiana huko nje, ndani ya jumba sisi ni familia moja.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki