Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Saliu Abazi, anayezungumza Kialbania, na ambaye alikuwa Mwislamu zamani anasema: “Ndugu waliokuwa Waislamu zamani hawatendewi sikuzote kwa fadhili na Waislamu, na watu wa familia zetu wanafikiri kimakosa kwamba tumewaacha kwa sababu tumechagua dini nyingine. Pia, kwa sababu ya chuki ya kikabila kati ya Waalbania na Waserbia, mara nyingi inakuwa vigumu kwa wale waliokuwa Waislamu kuwahubiria Waserbia.”

      Hata hivyo, kikundi cha watu 30 wa makabila mbalimbali kilikuwa kikikutana katika nyumba ya Saliu. “Katika miaka hiyo,” anakumbuka Saliu, “mikutano ilifanywa katika Kiserbia, na tulipata vitabu kutoka Belgrade. Siku moja polisi walikuja kwa ghafula katika nyumba yangu. Wakati huo akina ndugu kutoka Belgrade walikuwa tu wameleta vitabu, na sote tulikuwa tukifurahia ushirika. Nilipowaambia polisi kwamba hao walikuwa ndugu zangu, hawangeweza kuelewa jinsi Waserbia na Waalbania wanavyoweza kuwa ndugu.” Mwaka wa 1998, kikundi hicho cha wahubiri kilikodi mahali pa kutumia kama Jumba la Ufalme, katika mji mkubwa zaidi wa Kosovo, Priština.

      Katika majira ya masika ya 1999, chuki ya kikabila na roho ya utaifa ilipamba moto sana. Saliu anasema: “Jirani yangu alitisha kwamba ikiwa mimi na mwanangu hatungeshiriki katika vita, nyumba yetu ingeteketezwa kabisa. Hali ya kisiasa iliwachochea vibaya watu. Kwa sababu watu walipinga serikali iliyokuwa ikitawala Serbia, sheria hazingeweza kutekelezwa, watu walikuwa wajeuri, nao walifanya walichotaka.”

      Waserbia walioishi Kosovo walikabili hali ngumu zaidi kadiri hali ya kisiasa ilivyozidi kuzorota. Katika vita vya mwaka wa 1999, maelfu ya Waserbia na Waalbania walilazimika kukimbilia nchi nyingine jirani. Hata hivyo, ingawa kulikuwa na chuki kali sana ya kikabila, Saliu alihatarisha uhai wake kwa kuwaruhusu ndugu zake Waserbia wakimbilie katika nyumba yake.

  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 235]

      Saliu Abazi

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki