-
Intaneti Kutumia kwa Hekima Kifaa cha Ulimwenguni PoteMnara wa Mlinzi—2011 | Agosti 15
-
-
Tuwatumie au Tusiwatumie Wengine Habari Kupitia Intaneti?
Kutumia Intaneti kunatia ndani kupata habari na pia kuzieneza. Ingawa tuna uhuru wa kupokea na kuwatumia wengine habari, pia tuna daraka la kuhakikisha kwamba habari hizo ni za kweli na ni safi kiadili. Je, tunaweza kuthibitisha kwamba habari tunazoandika au kuwatumia wengine ni sahihi? Je, tuna ruhusa ya kueneza habari hizo?a Je, ni habari zinazofaa na zenye kujenga? Tuna nia gani tunapoeneza habari hizo? Je, tunataka kufanya hivyo ili wengine watusifu?
Barua zinazotumwa kupitia Intaneti zinaweza kuwa na faida sana zinapotumiwa kwa njia inayofaa. Tunaweza kupata pia habari nyingi sana kupitia barua hizo. Je, tunawalemea wengine kwa kueneza habari mpya au mambo yasiyofaa kwa marafiki wengi, labda tukitumia wakati wao wenye thamani? Je, hatupaswi kuchunguza nia yetu kabla ya kueneza habari kupitia Intaneti? Kwa kweli tuna kusudi gani? Zamani watu waliandika barua ili kueleza mambo yanayowahusu wao pamoja na familia na marafiki wao, wakiwajulisha wengine hali yao. Je, hatupaswi kuandika barua-pepe tukiwa na kusudi hilo? Kwa nini tuwatumie wengine habari ambazo hatuwezi kuzithibitisha?
-
-
Intaneti Kutumia kwa Hekima Kifaa cha Ulimwenguni PoteMnara wa Mlinzi—2011 | Agosti 15
-
-
a Habari hii inahusu pia picha. Ingawa tunaweza kupiga picha zetu binafsi, huenda hatuna ruhusa ya kuzieneza, wala hata kusambaza majina ya watu ambao wako katika picha hizo na kutaja mahali wanapoishi.
-