-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
Funzo la Biblia la Kutaniko
Jioni moja kila juma, Mashahidi wa Yehova wanakutana tena kwenye Jumba la Ufalme kwa ajili ya programu yenye sehemu tatu ambayo inachukua muda wa saa 1 na dakika 45. Sehemu ya kwanza ni Funzo la Biblia la Kutaniko ambalo ni la dakika 25. Sehemu hiyo inawasaidia wale waliohudhuria kuijua vizuri Biblia, kubadili kufikiri na mtazamo wao, na kuwa wanafunzi wazuri zaidi wa Kristo. (2 Timotheo 3:16, 17) Funzo hilo linaongozwa kwa maswali na majibu, kama tu Funzo la Mnara wa Mlinzi. Wale wanaotoa maelezo wanafanya hivyo kwa hiari. Kwa kawaida kichapo kinachotegemea Biblia kinachotumiwa ni kitabu au broshua iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
Kwa nini vichapo vinavyotegemea Biblia vinatumiwa katika mkutano huo? Katika nyakati za Biblia, haikutosha kusoma tu Neno la Mungu. ‘Walilifafanua, na kueleza maana yake; nao waliendelea kufafanua usomaji huo.’ (Nehemia 8:8) Katika miaka ya karibuni, vichapo vinavyozungumzia vitabu vya Isaya, Danieli, na Ufunuo vimewasaidia wale wanaohudhuria mkutano huo waelewe sehemu hizo za Biblia.
-
-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 22]
Funzo la Biblia la Kutaniko
-