Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaalikwa kwa Uchangamfu
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
    • Funzo la Biblia la Kutaniko

      Jioni moja kila juma, Mashahidi wa Yehova wanakutana tena kwenye Jumba la Ufalme kwa ajili ya programu yenye sehemu tatu ambayo inachukua muda wa saa 1 na dakika 45. Sehemu ya kwanza ni Funzo la Biblia la Kutaniko ambalo ni la dakika 25. Sehemu hiyo inawasaidia wale waliohudhuria kuijua vizuri Biblia, kubadili kufikiri na mtazamo wao, na kuwa wanafunzi wazuri zaidi wa Kristo. (2 Timotheo 3:16, 17) Funzo hilo linaongozwa kwa maswali na majibu, kama tu Funzo la Mnara wa Mlinzi. Wale wanaotoa maelezo wanafanya hivyo kwa hiari. Kwa kawaida kichapo kinachotegemea Biblia kinachotumiwa ni kitabu au broshua iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

      Kwa nini vichapo vinavyotegemea Biblia vinatumiwa katika mkutano huo? Katika nyakati za Biblia, haikutosha kusoma tu Neno la Mungu. ‘Walilifafanua, na kueleza maana yake; nao waliendelea kufafanua usomaji huo.’ (Nehemia 8:8) Katika miaka ya karibuni, vichapo vinavyozungumzia vitabu vya Isaya, Danieli, na Ufunuo vimewasaidia wale wanaohudhuria mkutano huo waelewe sehemu hizo za Biblia.

  • Unaalikwa kwa Uchangamfu
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
    • [Picha katika ukurasa wa 22]

      Funzo la Biblia la Kutaniko

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki