-
Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Epuka kuwasiliana na roho waovu
Shetani na roho waovu ni maadui wa Yehova. Wao ni adui zetu pia. Soma Luka 9:38-42, kisha mzungumzie swali hili:
Roho waovu wanawatendeaje wanadamu?
Hatungependa kujihusisha kwa vyovyote na roho waovu. Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12, kisha mzungumzie maswali haya:
Roho waovu wanatumia njia gani kujaribu kutushawishi na kuwasiliana nasi? Katika eneo unaloishi, watu hutumia njia gani kuwasiliana na roho waovu?
Yehova anatuagiza tuepuke kabisa mazoea ya kuwasiliana na roho waovu. Je, unafikiri jambo hilo linafaa? Kwa nini?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Je, unafikiri hirizi ambayo binti ya Palesa alivishwa mkononi ina madhara? Kwa nini?
Unafikiri Palesa alihitaji kufanya nini ili ajilinde dhidi ya roho waovu?
Sikuzote Wakristo wa kweli wamewapinga roho waovu. Soma Matendo 19:19 na 1 Wakorintho 10:21, kisha mzungumzie swali hili:
Kwa nini unapaswa kuharibu kitu chochote ulicho nacho ambacho kinahusiana na roho waovu?
-
-
Ni Nini Hutokea Tunapokufa?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Kwa nini ni muhimu kujua ukweli kuhusu kifo?
Watu wengi wanaogopa kifo, hata wanawaogopa watu waliokufa! Lakini mambo ambayo Biblia inasema kuhusu kifo yanaweza kukufariji. Yesu alisema: “Kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Baadhi ya dini hufundisha kwamba mtu anapokufa nafsi yake huendelea kuishi, lakini Biblia haifundishi hivyo. Basi, hakuna mtu anayeteseka baada ya kufa. Pia, kwa sababu watu waliokufa hawajui jambo lolote, hawawezi kutudhuru. Hivyo, hatuhitaji kuwatuliza au kuwaabudu watu waliokufa, wala kusali kwa ajili yao.
Watu fulani hudai kwamba wana uwezo wa kuwasiliana na watu waliokufa. Lakini hilo haliwezekani. Kama tulivyojifunza, “waliokufa hawajui jambo lolote kamwe.” Wale wanaofikiri wanawasiliana na wapendwa wao waliokufa, inawezekana kwamba wanawasiliana na roho waovu ambao hujifanya kuwa watu waliokufa. Kwa hiyo, kujua ukweli kuhusu kifo hutulinda dhidi ya roho waovu. Yehova anatuonya kwamba tusijaribu kuwasiliana na watu waliokufa kwa sababu anajua tukiwasiliana na roho waovu tutapata madhara.—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12.
-