-
Yerusalemu Na Hekalu La Sulemani‘Ona Nchi Nzuri’
-
-
Yerusalemu liko katika mwinuko wa meta 750 juu ya usawa wa bahari katika safu ya milima iliyo katikati mwa Yudea. Biblia inataja kwamba jiji hilo lilikuwa ‘limeinuka’ na waabudu ‘walipanda’ kuelekea huko. (Zb 48:2, Union Version; 122:3, 4) Jiji hilo la kale lilizungukwa na mabonde: Bonde la Hinomu upande wa magharibi na kusini, na bonde la mto la Kidroni upande wa mashariki. (2Fa 23:10; Yer 31:40) Bubujiko la maji la Gihonia katika Bonde la Kidroni na En-rogeli lililokuwa upande wa kusini, lilikuwa chemchemi muhimu ya maji safi kwa jiji hilo hasa wakati maadui waliposhambulia.—2Sa 17:17.
-
-
Yerusalemu Na Hekalu La Sulemani‘Ona Nchi Nzuri’
-
-
Lango la Bonde
-