-
MbinguUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Kwa hiyo, katika maandiko mengi, “mbingu” huwakilisha Mungu mwenyewe na cheo chake cha enzi kuu. Kiti chake cha ufalme kiko mbinguni, yaani, katika milki ya roho ambayo yeye hutawala juu yake pia. (Zb 103:19-21; 2Nya 20:6; Mt 23:22; Mdo 7:49) Akiwa katika cheo chake kilicho juu zaidi au kinachopita vyote, ni kana kwamba Yehova ‘hutazama chini’ kuelekea mbingu za kihalisi na dunia (Zb 14:2; 102:19; 113:6), na pia akiwa katika cheo hicho kilichoinuka yeye husema, hujibu maombi, na kutoa hukumu. (1Fa 8:49; Zb 2:4-6; 76:8; Mt 3:17) Kwa hiyo twasoma kwamba Hezekia na Isaya, wakiwa wanakabiliana na tisho kali, ‘waliendelea kusali na kuzililia mbingu ili kupata msaada.’ (2Nya 32:20; linganisha 2Nya 30:27.) Yesu, pia, alitumia mbingu kuwakilisha Mungu alipokuwa akiwauliza viongozi wa kidini ikiwa chanzo cha ubatizo wa Yohana kilikuwa ni kutoka “mbinguni au kwa wanadamu.” (Mt 21:25; linganisha Yoh 3:27.) Yule mwana mpotevu alikiri kuwa ametenda dhambi “juu ya mbingu” na vilevile dhidi ya baba yake mwenyewe. (Lu 15:18, 21) Kwa hiyo, “ufalme wa mbinguni,” haumaanishi tu kwamba makao yake ni mbingu za kiroho na unatawala kutoka huko, bali pia kwamba huo ndio “ufalme wa Mungu.”—Da 2:44; Mt 4:17; 21:43; 2Ti 4:18.
-
-
UnyenyekevuUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Sifa ya Mungu. Unyenyekevu ni moja kati ya sifa za Yehova Mungu. Lakini si kwamba amepungukiwa au anajitiisha kwa yeyote. Badala yake, anaonyesha unyenyekevu kwa kuwa mwenye rehema na huruma nyingi kuelekea watenda dhambi wanyenyekevu. Unyenyekevu wa Yehova unaonekana kwa kushughulika na wanadamu watenda dhambi na kwa kumtoa Mwana wake kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Yehova Mungu ameruhusu uovu kwa karibu miaka 6,000 na ameruhusu wanadamu kuendelea kuwapo ingawa baba yao Adamu alitenda dhambi. Kupitia fadhili zisizostahiliwa, wazao wa Adamu walionyeshwa rehema, hilo likiwapa fursa ya kupata uzima wa milele. (Ro 8:20, 21) Mambo hayo yote yanafunua unyenyekevu wa Mungu, na pia sifa zake nyingine.
Mfalme Daudi aliona na kuthamini sifa hiyo ambayo Mungu alimwonyesha kupitia fadhili zake zisizostahiliwa. Baada ya Yehova kumkomboa kutoka kwenye mikono ya maadui wake wote, aliimba hivi: “Wewe hunipa ngao yako ya wokovu, na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.” (2Sa 22:36; Zb 18:35) Ingawa ana utukufu mwingi na anaketi mahali pake palipokwezwa katika mbingu zilizo juu zaidi, bado inaweza kusemwa hivi kumhusu Yehova: “Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu, anayekaa juu? Huinama chini ili atazame mbingu na dunia, akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini. Humwinua juu maskini kutoka kwenye rundo la majivu ili amketishe pamoja na viongozi, pamoja na viongozi wa watu wake.”—Zb 113:5-8.
-