-
Mngojee YehovaMnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 15
-
-
Soma Zaburi 58 mpaka 64. Kwa kuhangaishwa na udhalimu, Daudi alisali ili adhabu ya kimungu itolewe kwa waovu. (Zaburi 58, 59) Alipotishwa kupatwa na ushinde, yeye alisihi aokolewe na alikuwa na uhakika wa kwamba Mungu angewakanyagia chini maadui. (Zaburi 60) Yehova tayari alikuwa amekwisha kuwa kimbilio kwa Daudi; kwa hiyo yeye angengojea kimya apate wokovu. (Zaburi 61,62) Alipolazimika kwenda nyikani, labda wakati Absalomu alipoasi, Daudi alipata furaha ‘uvulini mwa mabawa ya Mungu.’ (Zaburi 63) Mtungu zaburi alisali pia alindwe na “ghasia ya watu wafanyao maovu” na alikuwa na uhakika wa kwamba mwadilifu angepata kimbilio katika Yehova.—Zaburi 64.
-
-
Mngojee YehovaMnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 15
-
-
Somo Kwetu Sisi: Daudi alitosheka ‘kumngojea Mungu katika kimya’ ili atende kwa ajili yake. (Zaburi 62:1-7) Akiwa amejitiisha kwa mapenzi ya Yehova, alijisikia akiwa salama na alikuwa na uhakika katika Mungu kwa kunyamaza. Tukiwa na tumaini la namna hiyo katika Yehova, “amani ya Mungu” itahifadhi mioyo yetu na nguvu za akili zetu huku tukingojea kupata ukombozi wa kimungu kati ya adui zetu na dhiki.—Wafilipi 4:6, 7; Zaburi 33:20.
-