Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova, Mfanyi wa Mambo ya Ajabu
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Desemba 15
    • 8. Twaweza kuwa na ukaribu gani na Yehova, na yeye ameonyeshaje wema wake?

      8 Daudi atoa ombi jingine lenye kuhisiwa moyoni: “Wewe, Ee Yehova, ni mwema na tayari kusamehe; na fadhili-upendo kwa wale wote wanaokuitia ni nyingi. Sikiliza, Ee Yehova, sala yangu; na uelekezee fikira sauti za haja zangu. Katika siku ya taabu yangu nitakuitia, kwa kuwa utanijibu.” (Zaburi 86:5-7, NW) “Ee Yehova”—tena na tena tunasisi-muliwa na ukaribu wa msemo huo! Huo ni ukaribu uwezao kusitawishwa daima kupitia sala. Daudi alisali hivi pindi nyingine: “Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, wala maasi yangu. Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili [fadhili-upendo, NW] zako, Ee BWANA [Yehova, NW], kwa ajili ya wema wako.” (Zaburi 25:7) Yehova ndiye kielelezo bora kabisa cha wema—kwa kuandaa fidia ya Yesu, kwa kuonyesha rehema kwa watenda dhambi wenye kutubu, na kwa kuwamiminia fadhili-upendo Mashahidi wake waaminifu-washikamanifu na wenye kuthamini.—Zaburi 100:3-5; Malaki 3:10.

      9. Watenda dhambi wenye kutubu wanapaswa wafikirie kwa uzito uhakikishio gani?

      9 Je! tunapaswa kusumbuliwa na makosa ya zamani? Ikiwa sasa tunaifanyia miguu yetu vijia vilivyonyooka, tunachangamshwa tunapokumbuka uhakikishio wa mtume Petro kwa wale waliotubu wa kwamba “nyakati za kuburudishwa” zitatoka kwa Yehova. (Matendo 3:19) Acheni tuendelee kuwa karibu na Yehova katika sala kupitia Mwenye Kutufidi, Yesu, aliyesema hivi kwa upendo: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha [mtapata burudisho kwa nafsi zenu, NW].” Mashahidi waaminifu-washikamanifu wanaposali kwa Yehova leo katika jina la Yesu lenye thamani kubwa, wao kwa kweli hupata burudisho.—Mathayo 11:28, 29; Yohana 15:16.

  • Yehova, Mfanyi wa Mambo ya Ajabu
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Desemba 15
    • 13. Wazazi na watoto wao wanaweza kujinufaishaje kutokana na wema wa Yehova?

      13 Bila shaka, Daudi alikazia kikiki moyoni mwa mwana wake Sulemani uhitaji wa kutegemea wema wa Yehova. Hivyo, Sulemani angeweza kumwagiza mwana wake mwenyewe hivi: “Mtumaini BWANA [Yehova, NW] kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako. Usiwe mwenye hekima machoni pako; mche BWANA [Yehova, NW], ukajiepushe na uovu.” (Mithali 3:5-7) Wazazi leo wanapaswa vilevile wawafundishe watoto wao wadogo jinsi ya kusali kwa kumtumaini Yehova na jinsi ya kukabiliana na mashambulio ya ulimwengu usio na huruma—kama vile mbano wa marika shuleni na vishawishi vya kutenda ukosefu wa maadili. Kuzoea kanuni za Biblia pamoja na watoto wetu kila siku kwaweza kukazia kwenye mioyo yao michanga upendo kwa Yehova na kumtegemea kwa sala.—Kumbukumbu la Torati 6:4-9; 11:18, 19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki