-
Yehova, Mfanyi wa Mambo ya AjabuMnara wa Mlinzi—1992 | Desemba 15
-
-
8. Twaweza kuwa na ukaribu gani na Yehova, na yeye ameonyeshaje wema wake?
8 Daudi atoa ombi jingine lenye kuhisiwa moyoni: “Wewe, Ee Yehova, ni mwema na tayari kusamehe; na fadhili-upendo kwa wale wote wanaokuitia ni nyingi. Sikiliza, Ee Yehova, sala yangu; na uelekezee fikira sauti za haja zangu. Katika siku ya taabu yangu nitakuitia, kwa kuwa utanijibu.” (Zaburi 86:5-7, NW) “Ee Yehova”—tena na tena tunasisi-muliwa na ukaribu wa msemo huo! Huo ni ukaribu uwezao kusitawishwa daima kupitia sala. Daudi alisali hivi pindi nyingine: “Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, wala maasi yangu. Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili [fadhili-upendo, NW] zako, Ee BWANA [Yehova, NW], kwa ajili ya wema wako.” (Zaburi 25:7) Yehova ndiye kielelezo bora kabisa cha wema—kwa kuandaa fidia ya Yesu, kwa kuonyesha rehema kwa watenda dhambi wenye kutubu, na kwa kuwamiminia fadhili-upendo Mashahidi wake waaminifu-washikamanifu na wenye kuthamini.—Zaburi 100:3-5; Malaki 3:10.
-
-
Yehova, Mfanyi wa Mambo ya AjabuMnara wa Mlinzi—1992 | Desemba 15
-
-
11. Utendaji wa wazee unaweza kusaidiaje kuondoa hisia za hatia?
11 Huenda kukawa pindi ambazo tunakwazwa na wengine. Kutendwa vibaya kihisiamoyo au kimwili wakati wa utoto kumewaacha wengine wakiwa na hisia za hatia au za kutofaa kitu kabisa. Mtu aliyetendwa hivyo aweza kumwitia Yehova, akiwa na uhakika kwamba atamjibu. (Zaburi 55:16, 17) Mzee mwenye fadhili aweza kuonyesha kupendezwa na kumsaidia mtu kama huyo akubali uhakika wa kwamba hilo halikuwa kosa la mwenye kutendwa hivyo. Baadaye, mzee akimpigia simu ya kirafiki mara kwa mara hiyo yaweza kumsaidia mtu huyo aweze hatimaye ‘kuuchukua mzigo.’—Wagalatia 6:2, 5.
12. Taabu zimeongezekaje, lakini tunaweza kukabilianaje nazo kwa mafanikio?
12 Kuna hali nyinginezo nyingi zenye kutaabisha ambazo watu wa Yehova wamelazimika kung’ang’ana nazo leo. Tangu Vita ya Ulimwengu 1 katika 1914, maafa makuu yalianza kuikumba dunia hii. Kama ilivyotabiriwa na Yesu, huo ulikuwa “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” Taabu zimeongezeka kadiri tumeendelea kuingia “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3, 8, NW) “Wakati mchache” wa Ibilisi unapungua kuelekea mwisho wao wa upeo. (Ufunuo 12:12) “Kama simba angurumaye” akitafuta mawindo, Adui huyo mkubwa anatumia kila hila ipatikanayo ili atutenganishe na kundi la kondoo la Mungu na kutuharibu. (1 Petro 5:8) Lakini hatafaulu! Kwani, kama vile Daudi, tunakaza tumaini letu kikamili katika Mungu wetu mmoja, Yehova.
13. Wazazi na watoto wao wanaweza kujinufaishaje kutokana na wema wa Yehova?
13 Bila shaka, Daudi alikazia kikiki moyoni mwa mwana wake Sulemani uhitaji wa kutegemea wema wa Yehova. Hivyo, Sulemani angeweza kumwagiza mwana wake mwenyewe hivi: “Mtumaini BWANA [Yehova, NW] kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako. Usiwe mwenye hekima machoni pako; mche BWANA [Yehova, NW], ukajiepushe na uovu.” (Mithali 3:5-7) Wazazi leo wanapaswa vilevile wawafundishe watoto wao wadogo jinsi ya kusali kwa kumtumaini Yehova na jinsi ya kukabiliana na mashambulio ya ulimwengu usio na huruma—kama vile mbano wa marika shuleni na vishawishi vya kutenda ukosefu wa maadili. Kuzoea kanuni za Biblia pamoja na watoto wetu kila siku kwaweza kukazia kwenye mioyo yao michanga upendo kwa Yehova na kumtegemea kwa sala.—Kumbukumbu la Torati 6:4-9; 11:18, 19.
-