-
Yehova Aghadhibikia MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
7. “Mbingu” ni nini, na ‘jeshi la mbinguni’ ni nini?
7 Isaya aendelea kusema, akitumia mifano iliyo wazi: “Jeshi lote la mbinguni litafumuliwa, na mbingu zitakunjwa kama karatasi [“hati-kunjo,” “NW”], na jeshi lao lote litanyauka kama vile jani la mzabibu linyaukavyo na kupukutika, na kama jani la mtini linyaukavyo na kupukutika.” (Isaya 34:4) Usemi “jeshi lote la mbinguni” haumaanishi nyota na sayari halisi. Mistari ya 5 na 6 yasema kuhusu upanga wa machinjo ulioshiba damu katika ‘mbingu’ hizo. Kwa hiyo, lazima huo ni mfano wa kitu fulani katika eneo la binadamu. (1 Wakorintho 15:50) Kwa sababu ya ukuu wake zikiwa mamlaka zilizo kubwa, serikali za wanadamu zafananishwa na mbingu zinazotawala juu ya jamii ya kibinadamu duniani. (Waroma 13:1-4) Kwa hiyo, ‘jeshi la mbinguni’ lawakilisha majeshi ya mwungano ya serikali hizo za wanadamu.
8. Mbingu za mfano zathibitikaje kuwa “kama hati-kunjo,” na ‘majeshi’ yao yapatwa na nini?
8 “Jeshi” hilo “litafumuliwa,” litaoza, kama kitu kinachoharibika upesi. (Zaburi 102:26; Isaya 51:6) Mbingu halisi zilizo juu yetu huonekana kuwa zimepindika machoni petu, kama kitabu cha kale cha hati-kunjo, ambamo kwa kawaida maandishi yalikuwa upande wa ndani. Msomaji amalizapo kusoma maandishi yaliyo upande wa ndani, yeye huikunja na kuihifadhi hati-kunjo hiyo. Vivyo hivyo, “mbingu zitakunjwa kama hati-kunjo,” ikimaanisha kwamba serikali za binadamu lazima zikome. Lazima zikomeshwe kwenye Har–Magedoni zifikapo ukurasa wa mwisho wa historia yake. ‘Majeshi’ yao yenye fahari yataanguka kama vile majani yaliyonyauka yaangukavyo kutoka kwenye mzabibu au vile “jani la mtini linyaukavyo” na kuanguka kutoka kwenye mtini. Wakati wao utakuwa umekwisha.—Linganisha Ufunuo 6:12-14.
-
-
Yehova Aghadhibikia MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 360]
“Mbingu zitakunjwa kama hati-kunjo”
-