-
“Mkutano Mkubwa” Sasa Wachukua “Njia Kuu” Kuelekea Tengenezo la MunguUsalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
Kutokeza Shamba la Edeni la Mfano
4, 5. (a) Katika nyakati za kisasa, ni wakati gani mgeuzo kama huo wa nchi kama hiyo iliyoachwa ulitukia, na kwa sababu gani? (b) Shughuli za kurudisha hali nzuri ya yale mabaki wapakwa mafuta zilileta matokeo gani? (c) Unabii wa Isaya 35:5-7 ulielezaje hali yao ya kiroho iliyofanywa upya?
4 Mlingano wa kisasa katika maana ya kiroho, wa mgeuzo huo wa nchi kutoka kwa hali inayoonyesha kwamba Mungu ameiacha na kuwa na hali inayoshuhudia kurudishwa kwa kibali cha Yehova ulianza kutukia 1919. Watu wa Yehova waliorudishwa waliazimia kutumia kwa faida kamili kipindi cha amani kilichokuwa kimeanza. Koreshi Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, na Baba yake, Yehova Mungu, waliwapa mgawo mabaki ya Waisraeli wa kiroho yaliyokombolewa kwa kufanya kazi kubwa iliyolingana na kujengwa upya hekalu la Yehova kukifanywa na mabaki ya Israeli wa kale waliorudishwa kwao baada ya 537 K.W.K. Shughuli za kurudisha hali nzuri baada ya 1919 zilikuwa na matokeo ya kutokeza shamba la Edeni la mfano.
5 Hilo lilikuwa limetabiriwa katika maneno haya ya Isaya 35: “Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba; maana katika nyika maji yatabubujika; na vijito jangwani. Na mchanga ung’aao mfano wa maji utakuwa ziwa la maji, na nchi yenye kiu itakuwa chemchemi za maji; katika makao ya mbweha, walipokuwa wamelala, patakuwa na majani, pamoja na mianzi na manyasi.”—Isaya 35:5-7.
-
-
“Mkutano Mkubwa” Sasa Wachukua “Njia Kuu” Kuelekea Tengenezo la MunguUsalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
9. Kwa njia ya kiroho, ilikuwaje kwamba maji yalibubujika nyikani?
9 Ndiyo, ilikuwa kana kwamba maji yalikuwa yamebubujika katika nchi ya kiroho ambayo hapo kwanza ilikuwa imekauka na kukaa ukiwa, hivi kwamba sasa kila kitu kikaonekana kijani kibichi kukawa na mimea mingi mibichi-mibichi—tayari kutoa mazao mengi. Si ajabu kwamba watu wa Yehova waliorudishwa walifurahi sana sana wakahisi ni wenye nguvu kama kulungu ambaye hupanda kwa nguvu nyingi vileleni! Kweli kweli, yale maji ya ukweli juu ya Ufalme wa Mungu, uliosimamishwa 1914, ukiwa mikononi mwa Yesu Kristo yalibubujika kwa kani yenye kuongezeka, yakitokeza burudisho kubwa sana.—Isaya 44:1-4.
-