Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wenye Shangwe Sasa na Milele
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Februari 15
    • 17, 18. Ni katika maana gani kwamba paradiso iko sasa, na hilo lina tokeo gani juu yetu?

      17 Kwa hiyo twaweza kuangalia Isaya sura ya 35, tukifikiria utimizo wa wakati huu wa mstari wa 1 hadi wa 8. Je, si wazi kwamba tumepata ile ambayo huitwa kwa kufaa paradiso ya kiroho? La, haijakamilika—bado. Lakini kwa kweli ni paradiso, kwa maana, hapa twaweza tayari ‘kuona utukufu wa Yehova, uzuri wa Mungu wetu,’ kama vile isemwavyo katika mstari wa 2, (NW). Na tokeo ni nini? Mstari wa 10 (NW) wasema hivi: “Wale wenyewe waliokombolewa na Yehova watarudi na kwa hakika watakuja Zayoni kwa kilio chenye shangwe; na kushangilia hadi wakati usio dhahiri kutakuwa juu ya kichwa chao. Wao watapata mchachawo na kushangilia, na huzuni na kupiga kite lazima zikimbie mbali.” Kwa kweli, kule kutoka kwetu katika dini bandia na kufuatia kwetu ibada ya kweli chini ya upendeleo wa Mungu ni jambo lenye kuchochea shangwe.

  • Wenye Shangwe Sasa na Milele
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Februari 15
    • 24. Kwa nini waweza kukubaliana na usemi katika Isaya 35:10 (NW)?

      24 Isaya atuhakikishia hivi: “Wale wenyewe waliokombolewa na Yehova watarudi na kwa hakika watakuja Zayoni kwa kilio chenye shangwe; na kushangilia hadi wakati usio dhahiri kutakuwa juu ya kichwa chao.” Kwa hiyo twaweza kukubali kwamba tuna sababu ya kulia kwa shangwe. Shangwe juu ya yale ambayo tayari Yehova anawafanyia watu wake katika paradiso yetu ya kiroho, na shangwe juu ya yale tuwezayo kutazamia katika ile Paradiso halisi iliyo karibu. Kuhusu wale wenye shangwe—kuhusu sisi—Isaya aandika hivi: “Wao watapata mchachawo na kushangilia, na huzuni na kupiga kite lazima zikimbie mbali.”—Isaya 35:10, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki